Mhubiri
9 Kwa maana nilitia yote haya moyoni mwangu, na kutafuta yote haya,+ kwamba waadilifu na wenye hekima na kazi zao, wako katika mkono wa Mungu wa kweli.+ Wanadamu hawajui upendo wala chuki ambazo zimekuwa kabla yao.+ 2 Wote ni sawa katika lile ambalo wote wanalo.+ Kuna mwisho mmoja+ kwa mwadilifu+ na kwa mwovu,+ mtu mwema na mtu safi na mtu asiye safi, na mtu anayetoa dhabihu na mtu ambaye hatoi dhabihu. Mtu mwema ni sawa na mtenda-dhambi;+ mtu anayekula kiapo ni sawa na yeyote yule ambaye ameogopa kiapo rasmi.+ 3 Hili ndilo jambo lenye msiba katika yote ambayo yamefanywa chini ya jua, ya kwamba, kwa sababu wote hufikiwa na mwisho uleule,+ moyo wa wana wa binadamu pia umejaa mabaya;+ na kuna wazimu+ mioyoni mwao wakati wa maisha yao, na baada ya hayo—ni kwenda kwa wafu!+
4 Kwa maana kwa yeyote yule ambaye ameunganishwa na wote walio hai kuna uhakika, kwa sababu mbwa aliye hai+ ni afadhali kuliko simba aliyekufa.+ 5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa;+ lakini wafu, hawajui lolote kamwe,+ wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa.+ 6 Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea,+ na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.+
7 Nenda, ukale chakula chako kwa kushangilia na kunywa divai yako kwa moyo mchangamfu,+ kwa sababu tayari Mungu wa kweli amependezwa na kazi zako.+ 8 Katika kila pindi, mavazi yako na yawe meupe,+ wala kichwa chako kisikose mafuta.+ 9 Furahia maisha pamoja na mke unayempenda+ siku zote za maisha yako yaliyo ya ubatili ambayo umepewa na Yeye chini ya jua, siku zote za hali yako iliyo ya ubatili, kwa maana hilo ndilo fungu lako maishani+ na katika kazi yako ngumu unayoifanya kwa bidii chini ya jua. 10 Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote,+ kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi+ wala hekima+ katika Kaburi,*+ mahali unapokwenda.+
11 Nilirudi, nikaona chini ya jua kwamba si wenye mbio wanaoshinda katika mbio,+ wala wenye nguvu wanaoshinda katika pigano,+ wala pia wenye hekima wanaopata chakula,+ wala pia wenye uelewaji wanaokuwa na utajiri,+ wala wenye ujuzi wanaopata kibali;+ kwa sababu wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.+ 12 Kwa maana mwanadamu+ pia hajui wakati wake.+ Kama vile samaki wanaonaswa katika wavu mbovu,+ na kama ndege wanaonaswa katika mtego,+ ndivyo wana wa binadamu wenyewe wanavyonaswa wakati wenye msiba,+ unapowaangukia ghafula.+
13 Pia nikaona jambo hili kuhusu hekima chini ya jua—nalo lilikuwa kuu kwangu: 14 Kulikuwa na jiji dogo, na wanaume waliokuwamo walikuwa wachache; mfalme mkuu akaja juu yake, akalizunguka na kujenga ngome+ zilizo kubwa ili kulishambulia. 15 Ndani yake mkapatikana mtu mwenye uhitaji lakini mwenye hekima, naye akaliokoa jiji hilo kwa sababu ya hekima yake.+ Lakini hakuna mtu aliyemkumbuka yule mtu mhitaji.+ 16 Na mimi mwenyewe nikasema: “Hekima ni bora kuliko uwezo;+ hata hivyo hekima ya mtu mwenye uhitaji hudharauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.”+
17 Maneno ya wenye hekima yanayosemwa kwa utulivu husikiwa+ zaidi kuliko kelele za mtu anayetawala kati ya wajinga.+
18 Hekima ni bora kuliko silaha za vita, na mtenda-dhambi mmoja tu anaweza kuharibu mambo mengi mema.+