11 Na watakapokuwa wakiwapeleka kuwashtaki, msihangaike kuhusu jambo mtakalosema; bali semeni jambo mtakalopewa saa hiyo, kwa maana si ninyi mnaosema, bali ni roho takatifu.+
11 Mtakapopelekwa mbele ya makusanyiko ya watu wote,* maofisa wa serikali, na mamlaka, msihangaike kuhusu jinsi mtakavyojitetea au jambo mtakalosema,+12 kwa maana saa hiyohiyo roho takatifu itawafundisha mambo mnayopaswa kusema.”+
14 Kwa hiyo, azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema kuhusu jinsi mtakavyojitetea,+15 kwa maana nitawapa maneno na hekima, ambayo wapinzani wenu wote kwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+