2 Atapanda kama tawi+ mbele yake, kama mzizi kutoka katika nchi iliyokauka.
Hana umbo la kifahari, wala utukufu wowote;+
Na tunapomwona, sura yake haituvutii.
3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+
Mtu aliyekusudiwa kupata maumivu na aliyezoea magonjwa.
Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu.
Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.+