-
“Kuna Thawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu”Mnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
-
-
Kwa sababu ya rekodi ya Asa, haishangazi kwamba alisali alipokabili jeshi kubwa zaidi la kibinadamu linalotajwa katika Maandiko. Asa alijua kwamba Mungu anathawabisha matendo ya imani. Katika sala yake, mfalme huyo alimsihi Yehova amsaidie. Asa alitambua kwamba ikiwa angemtegemea Mungu na kupata msaada wake, angeshinda vita haidhuru maadui walikuwa wengi au wenye nguvu kadiri gani. Jina la Yehova lilihusika katika vita hivyo, na hivyo Asa alimsihi Mungu amsaidie kwa msingi huo. Mfalme huyo alisali hivi: “Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana sisi tunakuegemea wewe, nasi kwa jina lako tumekuja kupigana na umati huu. Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa apate nguvu juu yako.” (2 Nya. 14:11) Ni kana kwamba alikuwa akisema: ‘Uvamizi wa Waethiopia ni shambulizi dhidi yako, Yehova. Usiache jina lako lidharauliwe kwa kuruhusu wanadamu walio dhaifu wawashinde wale wanaoitwa kwa jina lako.’
-
-
“Kuna Thawabu kwa Ajili ya Kazi Yenu”Mnara wa Mlinzi—2012 | Agosti 15
-
-
Leo, watu wa Yehova wanakabili wapinzani wengi wenye nguvu. Hatutapigana nao kwa kutumia silaha halisi katika uwanja halisi wa kivita. Hata hivyo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atawathawabisha watu wake wote waaminifu kwa kuwapa ushindi wanapopigana vita vya kiroho kwa ajili ya jina lake. Mapambano yetu huenda yakatia ndani kujitahidi kuishinda roho ya upotovu wa maadili iliyoenea, udhaifu wetu, au kujitahidi kuilinda familia yetu kutokana na uvutano unaopotosha. Hata tukabili matatizo ya aina gani, tunaweza kutiwa moyo na sala ya Asa. Ushindi wake ulikuwa ushindi wa Yehova. Ushindi huo unaonyesha kile ambacho wote wanaomtegemea Yehova wanaweza kutazamia. Hakuna mwanadamu anayeweza kushindana na Yehova.
-