-
Kuna Wakati wa Kila KituMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 1
-
-
Baada ya kutaja mambo mengi yanayoonekana kuwa na “wakati uliowekwa,” Sulemani aliandika hivi: “Nimeona shughuli ambayo Mungu amewapa wana wa binadamu wajishughulishe nayo. Amefanya kila kitu kiwe chenye kupendeza kwa wakati wake.”—Mhubiri 3:10, 11.
Mungu amewapa wanadamu shughuli nyingi, au mambo mengi ya kufanya, naye Sulemani aliorodhesha baadhi ya mambo hayo. Pia, Mungu ametupa uhuru wa kuchagua tunachotaka kufanya. Hata hivyo, kwa kila jambo kuna wakati unaofaa wa kulifanya ili kupata matokeo bora zaidi. Kwa mfano, fikiria maneno ya Sulemani “wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa kilichopandwa,” yanayopatikana kwenye Mhubiri 3:2. Wakulima wanajua kwamba kuna wakati unaofaa zaidi wa kupanda kila mmea. Namna gani ikiwa mkulima angepuuza jambo hilo na kupanda mimea wakati au katika majira yasiyofaa? Je, atasema hakupata mazao mazuri kwa sababu ya majaliwa, hata kama amefanya kazi ngumu? La hasha! Hakupanda kwa wakati unaofaa. Mkulima angepata mazao mazuri ikiwa angefuata mpangilio wa mambo uliowekwa na Muumba.
Kwa hiyo, Mungu hajapanga mapema mambo yatakayompata kila mtu au jinsi mambo yote yatakavyotukia, bali ameweka kanuni za kuongoza utendaji wa wanadamu kupatana na kusudi lake. Ili wanadamu wafanikiwe katika shughuli zao, lazima watambue na kutenda kupatana na mapenzi ya Mungu na wakati wake uliowekwa.
-
-
Kuna Wakati wa Kila KituMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 1
-
-
Kuelewa Wakati wa Mungu
Baada ya kusema, “[Mungu] amefanya kila kitu kiwe chenye kupendeza kwa wakati wake,” Sulemani anatusaidia kuelewa maneno hayo kwa kusema, “Tena wakati usio na kipimo ameuweka ndani ya moyo wao, ili mwanadamu asiweze kugundua kazi ambazo Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mpaka mwisho.” Zaire Swahili Bible inasema hivi katika mstari huo: “Ameweka milele vilevile ndani ya mioyo yao, lakini hata mutu asiweze kutambua kazi Mungu aliyofanya tangu mwanzo hata mwisho.”—Mhubiri 3:11.
Mambo mengi yameandikwa kuhusu mstari huo. Lakini ukweli ni kwamba kila mmoja wetu amejiuliza wakati mmoja au mwingine kuhusu kusudi la maisha na wakati wetu ujao. Katika historia yote ya wanadamu, watu wameshindwa kukubali kwamba kusudi pekee la maisha ni kufanya kazi ngumu na kisha kufa. Kati ya viumbe wote, sisi wanadamu ni wa pekee kwa sababu tunafikiri si kuhusu wakati huu tu, bali pia kuhusu wakati wetu ujao. Hata tunatamani kuishi milele. Kwa nini? Kama andiko hilo linavyoonyesha, Mungu “ameweka milele . . . ndani ya mioyo” ya wanadamu.
Ili kutosheleza tamaa hiyo, watu wamejiuliza mara nyingi ikiwa kuna uhai baada ya kifo. Wengine wamekata kauli kwamba kitu fulani ndani yetu kinaendelea kuishi tunapokufa. Wengine wanaamini kwamba tutazaliwa upya tena na tena katika mwili mwingine. Wengine nao wanaamini kwamba kila kitu maishani kimepangiwa mapema au ni mapenzi ya Mungu na kwamba hatuwezi kubadili chochote. Kwa kusikitisha, maelezo yote hayo hayajatoa majibu yenye kuridhisha. Hiyo ni kwa sababu “mwanadamu [hawezi] kugundua kazi ambazo Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mpaka mwisho,” inasema Biblia.
Ukweli wa kwamba wanadamu wana tamaa ya kujua mambo ya wakati ujao na hawawezi kupata majibu kumewasumbua wanafalsafa kwa muda mrefu sana. Hata hivyo, kwa kuwa Mungu ndiye ameweka tamaa hiyo katika mioyo yetu, je, si jambo linalopatana na akili kutazamia kwamba atatupa kile tunachohitaji ili kutosheleza tamaa hiyo? Biblia inasema hivi kumhusu Yehova: “Unaufumbua mkono wako na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.” (Zaburi 145:16) Kwa kujifunza Neno la Mungu, Biblia, tunaweza kupata maelezo yenye kuridhisha kuhusu uhai na kifo na kuhusu kusudi la milele la Mungu kwa ajili ya dunia na jamii ya wanadamu.—Waefeso 3:11.
-
-
Wakati wa Kufanya UamuziMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 1
-
-
“Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.”—Mwanzo 1:27.
MANENO hayo yanayojulikana sana yaliyo katika kurasa za kwanza za Biblia yanaonyesha moja kati ya mambo makuu zaidi ambayo Mungu ‘amefanya yawe yenye kupendeza kwa wakati wake,’ yaani, kuwaumba wenzi wawili wakamilifu, Adamu na Hawa. (Mhubiri 3:11)
-