-
Furaha ya Kweli Yaweza Kupatikana Wapi?Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 15
-
-
Katika Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu Kristo alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye kuona uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbingu ni wao.” (Mathayo 5:3) Yesu pia alisema hivi: “Fulizeni kufungua macho yenu na mlinde dhidi ya kila namna ya tamaa, kwa sababu hata wakati mtu ana wingi uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”—Luka 12:15.
-
-
Furaha ya Kweli Yaweza Kupatikana Wapi?Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 15
-
-
Wengine hugeukia utu wa ndani katika kutafuta kwao furaha kwa kujaribu kujenga heshima yao wenyewe. Maktaba na duka za vitabu zimejaa vitabu vyenye kutoa mwongozo wa kufanya maendeleo ya kibinafsi, lakini vichapo hivyo haviwaletei watu furaha idumuyo. Hivyo, basi, ni wapi tuwezapo kupata furaha halisi?
Ili kuwa wenye furaha kikweli, twapaswa kutambua uhitaji wetu wa kiroho tuliozaliwa nao. Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale wenye kuona uhitaji wao wa kiroho.” Bila shaka, haingetunufaisha kama tungeufahamu uhitaji huo kisha tushindwe kufanya jambo lolote juu yao. Kwa kutoa kielezo: Ni nini kingempata mkimbiaji wa shindano la mbio la mwendo mrefu ambaye baada ya shindano angeshindwa kuitikia uhitaji wa mwili wake wa kupata maji? Je, asingekabili upesi upungufu wa maji mwilini na matokeo mengine mazito? Hali kadhalika, tukishindwa kuitikia uhitaji wetu wa kupata lishe la kiroho, hatimaye tutanyauka kiroho. Hilo litaongoza kwenye hali ya kupoteza shangwe na furaha.
-