-
Ni Nani Ambaye Huongoza Kufikiri Kwako?Mnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 1
-
-
Kwa hiyo, Paulo aliomba Wakristo wenzake ‘wakome kufanyizwa kulingana na mtindo wa mfumo huu wa mambo.’ (Waroma 12:2) Mtafsiri mmoja wa Biblia alisimulia kwa maneno mengine maneno ya Paulo kwa njia hii: “Msiache ulimwengu unaowazunguka uwasonge katika muundo wake.” (Waroma 12:2, Phillips) Shetani atajaribu kila njia kukuelekeza kwa nguvu kama atakavyo, kama vile mfinyanzi wa zamani aliyeufinyanga udongo kwa nguvu na kuutandaza ili kutia alama alizotaka juu ya udongo. Shetani anatumia siasa za ulimwengu, biashara, dini, na vitumbuizo kufanya hivyo.
-
-
Ni Nani Ambaye Huongoza Kufikiri Kwako?Mnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 1
-
-
Uchaguzi ni wako. Waweza kuchagua “kufanyizwa kulingana na mtindo wa mfumo huu wa mambo” kwa kuacha falsafa na kanuni za ulimwengu zitawale kufikiri kwako. (Waroma 12:2) Lakini ulimwengu huu haupendezwi kikweli na masilahi yako. Kwa hiyo, “jihadharini,” aonya mtume Paulo, “labda huenda kukawa na mtu fulani ambaye atawachukua nyinyi kama windo lake kupitia falsafa na udanganyo mtupu kulingana na mapokeo ya wanadamu.” (Wakolosai 2:8) Kusongwa kuwa katika muundo wa Shetani kwa njia hii, au ‘kuchukuliwa kama windo lake,’ hakuhitaji jitihada. Ni kama moshi wenye kupita. Waweza kuathiriwa kwa kupumua tu hewa iliyochafuka.
-