-
Matendo 10:30-33Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
30 Basi Kornelio akasema: “Siku ine (4) zenye zilipita kuanzia saa hii, nilikuwa ninasali katika nyumba yangu saa ya kenda (9);* wakati huo mwanaume mwenye kuvaa nguo yenye kungaa akasimama mbele yangu 31 na kusema: ‘Kornelio, sala yako imesikiwa na kukubaliwa, na Mungu amekumbuka zawadi zako za rehema. 32 Kwa hiyo, tuma watu waende Yopa wamuite Simoni mwenye kuitwa Petro. Mutu huyu ni mugeni katika nyumba ya Simoni, mutengenezaji wa ngozi, pembeni ya bahari.’+ 33 Kwa hiyo, mara moja nikatuma watu wakuite, na umefanya muzuri kuja hapa. Basi sisi wote tuko mbele ya Mungu ili kusikia mambo yote yenye Yehova* amekuamuru useme.”
-