Maelezo ya Chini
c Maneno “kuzikomesha falme hizi zote” kwenye Danieli 2:44 yanahusu falme, ao serikali kubwa za ulimwengu, zinazofananishwa na sehemu za sanamu. Hata hivyo, unabii mwengine wa Biblia unaonyesha kama “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watajipanga ili kupigana na Yehova katika ‘vita ya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.’ (Ufu. 16:14; 19:19-21) Kwa hiyo, falme zinazofananishwa na sanamu hiyo na falme zingine zote zitaharibiwa kwenye Har-Magedoni.