Methali
31 Maneno ya Lemueli mfalme, ujumbe mzito+ ambao mama yake alimwambia ili kumrekebisha:+
2 Niseme nini, ewe mwanangu, niseme nini, ewe mwana wa tumbo langu,+ niseme nini, ewe mwana wa nadhiri zangu?+
3 Usiwape wanawake nguvu zako za uhai,+ wala njia zako kwa kitu ambacho hufanya wafalme wafutiliwe mbali.+
4 Haifai wafalme, ewe Lemueli, haifai wafalme kunywa divai wala maofisa wakuu kuuliza: “Kileo kiko wapi?”+ 5 ili mtu asinywe na kusahau jambo lililoagizwa na kupotosha haki ya yeyote wa wana wa mateso.+ 6 Mpeni kileo mtu yeyote anayekaribia kuangamia+ na kuwapa divai watu wenye uchungu katika nafsi.+ 7 Acheni mtu anywe na kuusahau umaskini wake, na mtu asiikumbuke taabu yake tena.
8 Fungua kinywa chako kwa ajili ya mtu asiyeweza kusema,+ ili kutetea watu wote wanaopitilia mbali.+ 9 Fungua kinywa chako, hukumu kwa uadilifu na kutetea mtu mwenye kuteseka na maskini.+
א [ʼAʹleph]
10 Mke mwenye uwezo, ni nani anayeweza kumpata?+ Thamani yake inapita sana ile ya marijani.
ב [Behth]
11 Moyo wa mume wake umemtegemea, wala hakuna faida inayokosekana.+
ג [Giʹmel]
12 Amemthawabisha mume wake kwa mema, wala si kwa mabaya, siku zote za maisha yake.+
ד [Daʹleth]
13 Ametafuta sufu na kitani, naye hufanya kazi yoyote inayopendeza mikono yake.+
ה [Heʼ]
14 Amekuwa kama meli za mfanyabiashara.+ Huleta chakula chake kutoka mbali.
ו [Waw]
15 Tena huamka kabla usiku haujaisha,+ na kuwapa watu wa nyumbani mwake chakula na kuwapa vijana wake wa kike fungu lao lililoamriwa.+
ז [Zaʹyin]
16 Amefikiria shamba, akalinunua;+ amepanda shamba la mizabibu kutokana na matunda ya mikono yake.+
ח [Chehth]
17 Amejifunga nguvu viunoni, naye ameitia nguvu mikono yake.+
ט [Tehth]
18 Ametambua kwamba biashara yake ni nzuri; taa yake haizimiki usiku.+
י [Yohdh]
19 Amenyoosha mikono yake kushika kijiti cha kusokotea uzi, nayo mikono yake mwenyewe imeshika gurudumu la kusokota nyuzi.+
כ [Kaph]
20 Amewanyooshea mkono wenye kuteseka, na mikono yake amemkunjulia maskini.+
ל [Laʹmedh]
21 Hana wasiwasi juu ya watu wa nyumbani mwake kwa sababu ya theluji, kwa maana watu wote wa nyumbani mwake wamevaa mavazi mawili.+
מ [Mem]
22 Amejitengenezea matandiko yenye mapambo.+ Mavazi yake ni ya kitani na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau.+
נ [Nun]
23 Mume wake+ ni mtu anayejulikana malangoni,+ anapoketi pamoja na wanaume wazee wa nchi.
ס [Saʹmekh]
24 Hata ametengeneza mavazi ya ndani+ na kuyauza, nao wafanya-biashara amewapa mishipi.
ע [ʽAʹyin]
25 Nguvu na fahari ndiyo mavazi yake,+ naye anaucheka wakati ujao.+
פ [Peʼ]
26 Hufungua kinywa chake kwa hekima,+ na sheria ya fadhili zenye upendo ziko katika ulimi wake.+
צ [Tsa·dhehʹ]
27 Anaangalia shughuli za nyumba yake, wala hali mkate wa uvivu.+
ק [Qohph]
28 Wanawe wamesimama na kumtangaza kuwa mwenye furaha,+ mume wake husimama, naye humsifu.+
ר [Rehsh]
29 Kuna binti wengi+ ambao wameonyesha uwezo, lakini wewe—wewe umewapita hao wote.+
ש [Shin]
30 Uvutio unaweza kudanganya,+ nayo sura yenye kupendeza inaweza kuwa ubatili;+ lakini mwanamke anayemwogopa Yehova ndiye anayejiletea sifa.+
ת [Taw]
31 Mpeni baadhi ya matunda ya mikono yake,+ nazo kazi zake na zimsifu malangoni.+