Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumapili, Mei 18

Nitawasikiliza.—Yer. 29:12.

Yehova anaahidi kusikiliza sala zetu. Mungu wetu anawapenda waabudu wake waaminifu, hivyo hatapuuza kamwe sala zao. (Zab. 10:17; 37:28) Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba atatupatia kila kitu tunachomwomba. Huenda tukapata baadhi ya mambo tunayoomba katika ulimwengu mpya. Yehova anazingatia jinsi maombi yetu yanavyohusiana na kusudi lake. (Isa. 55:​8, 9) Mojawapo ya mambo anayotaka ni kwamba dunia ijae watu wanaomtii yeye kwa shangwe akiwa Mtawala wao. Lakini Shetani alidai kwamba wanadamu wangekuwa na maisha mazuri zaidi ikiwa wangejitawala. (Mwa. 3:​1-5) Yehova aliwaruhusu wanadamu wajitawale ili kuthibitisha kwamba madai ya Ibilisi ni ya uwongo. Hata hivyo, serikali za wanadamu zimesababisha matatizo mengi ambayo tunakabili leo. (Mhu. 8:9) Tunajua kwamba Yehova hataondoa sasa matatizo haya yote. w23.11 21 ¶4-5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Mei 19

Nimekuweka uwe baba ya mataifa mengi.—Rom. 4:17.

Yehova aliahidi kwamba kupitia Abrahamu mataifa mengi yangebarikiwa. Lakini Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 100 na Sara miaka 90, mwana aliyeahidiwa hakuwa amezaliwa. Kwa maoni ya wanadamu, ilionekana kwamba haiwezekani kwa Abrahamu na Sara kuwa na mwana. Hilo lilikuwa jaribu kubwa kwa Abrahamu. “Lakini kwa kutegemea tumaini, alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi.” (Rom. 4:​18, 19) Na hatiMeie, tumaini la Abrahamu lilitimia. Alikuja kuwa baba ya Isaka, mwana aliyemsubiri kwa muda mrefu. (Rom. 4:​20-22) Tunaweza kuwa na kibali cha Mungu, kuhesabiwa kuwa waadilifu, na kuwa rafiki za Mungu kama Abrahamu. Hilo ndilo jambo ambalo Paulo alikazia alipoandika hivi: “Maneno ‘ilihesabiwa kwake’ hayakuandikwa kwa ajili [ya Abrahamu] tu, bali pia kwa ajili yetu ambao itahesabiwa, kwa sababu tunamwamini Yeye aliyemfufua Yesu.” (Rom. 4:​23, 24) Kama Abrahamu, tunahitaji kuwa na imani, matendo, pamoja na tumaini. w23.12 7 ¶16-17

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Mei 20

Umeona dhiki yangu; unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.—Zab. 31:7.

Unapokabili jaribu linalokufanya uogope, kumbuka kwamba Yehova anajua jaribu unalokabili na jinsi linavyokufanya uhisi. Kwa mfano, Yehova aliona jinsi Waisraeli walivyotendewa isivyo haki nchini Misri na pia ‘alijua maumivu yao.’ (Kut. 3:7) Hata hivyo, huenda usitambue jinsi Yehova anavyokusaidia unapokabili jaribu linalokuogopesha. Basi, unaweza kufanya nini? Mwombe Yehova akusaidie uone jinsi anavyokutegemeza. (2 Fal. 6:​15-17) Kisha fikiria maswali haya: Je, kuna hotuba yoyote au maelezo katika mkutano wa kutaniko yaliyokuimarisha? Je, kuna chapisho lolote, video, au wimbo uliotungwa ambao umekutia moyo? Je, kuna mtu yeyote ambaye amekueleza jambo au kukusomea andiko lililokutia moyo? Inaweza kuwa rahisi kusahau jinsi ndugu na dada wanavyotupenda na jinsi chakula cha kiroho kinavyotunufaisha. Hata hivyo, hizo ni zawadi za pekee kutoka kwa Yehova. (Isa. 65:13; Marko 10:​29, 30) Zinathibitisha kwamba Yehova anakujali. (Isa. 49:​14-16) Na zinathibitisha kwamba anastahili kutumainiwa. w24.01 4-5 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki