Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1950-2021)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatatu, Februari 22

Hawa . . . [ni] wafanyakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, nao wamekuwa chanzo cha faraja nyingi kwangu.​—Kol. 4:11.

Mtume Paulo alikabili mambo mengi yaliyohatarisha maisha yake. (2 Kor. 11:23-28) Pia, alilazimika kuvumilia “mwiba katika mwili,” ambao huenda ulikuwa tatizo fulani la afya. (2 Kor. 12:7) Alilazimika pia kukabiliana na hali yenye kuvunja moyo wakati Dema, ambaye pindi fulani alikuwa mfanyakazi mwenzake, alimwacha “kwa sababu aliupenda mfumo wa mambo wa sasa.” (2 Tim. 4:10) Paulo alikuwa Mkristo jasiri aliyetiwa mafuta kwa roho ambaye aliwasaidia wengine bila ubinafsi, lakini nyakati nyingine hata yeye alivunjika moyo. (Rom. 9:1, 2) Paulo alipata faraja na msaada aliohitaji. Jinsi gani? Bila shaka, Yehova alitumia roho yake takatifu ili kumtia nguvu. (2 Kor. 4:7; Flp. 4:13) Pia, Yehova alimfariji kupitia Wakristo wenzake. Paulo aliwataja baadhi ya wafanyakazi wenzake kuwa “chanzo cha faraja nyingi.” (Kol. 4:11) Miongoni mwa wafanyakazi hao aliowataja kwa majina ni Aristarko, Tikiko, na Marko. Walimtia nguvu Paulo na kumsaidia aendelee kuvumilia. w20.01 8 ¶2-3

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2021

Jumanne, Februari 23

Ameyatia nuru macho ya moyo wenu.​—Efe. 1:18.

Yesu alionyesha kwamba ni vigumu kumweleza kihususa mtu ambaye hajatiwa mafuta jinsi mtu ‘aliyezaliwa tena’ au ‘aliyezaliwa kwa roho’ anavyohisi. (Yoh. 3:3-8) Mkristo anapotiwa mafuta, njia yake ya kufikiri hubadilika jinsi gani? Kabla ya kutiwa mafuta na Yehova, Wakristo hao walikuwa na tumaini la kuishi milele duniani. Walikuwa wakitazamia kwa hamu kubwa sana wakati ambapo Yehova ataondoa uovu wote na kuifanya dunia kuwa paradiso. Huenda waliwazia jinsi watakavyowakaribisha watu wa familia au marafiki watakaofufuliwa. Lakini baada ya kutiwa mafuta, walianza kufikiri kwa njia tofauti. Kwa nini? Si kwa sababu hawakuridhishwa na tumaini la kuishi duniani. Wala hawakubadili njia yao ya kufikiri kwa sababu ya mkazo au matatizo ya kihisia. Na hawakuhisi ghafla kwamba kuishi milele duniani kungekuwa jambo lenye kuchosha. Badala yake, Yehova alitumia roho yake takatifu kubadili njia yao ya kufikiri na tumaini walilotazamia kwa hamu. w20.01 22 ¶9-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2021

Jumatano, Februari 24

Kila mtu na ajitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa.​—Rom. 13:1.

Chini ya Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli, wanaume waliowekwa rasmi hawakushughulikia tu mambo ya kiroho, bali pia walishughulikia kesi za madai na za uhalifu. Lakini chini ya “sheria ya Kristo,” wazee wana jukumu la kushughulikia mambo ya kiroho tu inapohusu visa vya ukosaji. (Gal. 6:2) Wanatambua kwamba mamlaka za serikali zimekabidhiwa na Mungu wajibu wa kushughulikia kesi za madai na za uhalifu. Wajibu huo unatia ndani mamlaka ya kumtoza mhusika faini au kumfunga gerezani. (Rom. 13:2-4) Wazee wa kutaniko hushughulikiaje visa vya dhambi nzito? Wao hutumia Maandiko kuchanganua mambo na kufanya maamuzi. Wanazingatia akilini kwamba upendo ndio msingi wa sheria ya Kristo. Upendo huwachochea wazee kufikiria maswali haya: Ni jambo gani linalohitaji kufanywa ili kumsaidia yeyote kutanikoni ambaye ametendewa isivyo haki? Upendo huwachochea wazee wa kutaniko wachunguze mambo yafuatayo kuhusu mkosaji: Je, mkosaji ametubu? Je, tunaweza kumsaidia awe tena na uhusiano mzuri pamoja na Yehova? w19.05 7 ¶23-24

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2021
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2021 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki