23 kwa sababu wametenda upumbavu katika Israeli,+ nao wanaendelea kufanya uzinzi pamoja na wake za wenzao+ na kuendelea kusema uwongo kwa jina langu mwenyewe neno ambalo mimi sikuwaamuru.+
“‘“Mimi ndiye ninayejua nami ni shahidi,”+ asema Yehova.’”
3 Hivyo, basi, mume wake anapokuwa hai, mwanamke huyo ataitwa mzinzi ikiwa atakuwa wa mwanamume mwingine.+ Lakini mume wake akifa, yeye yuko huru kutoka katika sheria ya mume, hivi kwamba mwanamke huyo si mzinzi akiwa wa mwanamume mwingine.+