Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 19:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Nao Mlima Sinai ukatoa moshi kila mahali,+ kwa kuwa Yehova alikuwa ameshuka juu yake katika moto;+ na moshi wake ukawa ukipaa kama moshi wa tanuru,+ na mlima wote ulikuwa ukitetemeka sana.+

  • Kutoka 20:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Naye Yehova akaendelea kumwambia Musa:+ “Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘Ninyi wenyewe mmeona kwamba nilisema nanyi kutoka mbinguni.+

  • Kumbukumbu la Torati 4:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Naye Yehova akaanza kusema nanyi kutoka katikati ya moto.+ Sauti ya maneno ndiyo mliyokuwa mkiisikia, bali hamkuwa mkiona umbo+ lolote—mlisikia sauti tu.+

  • Kumbukumbu la Torati 4:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Nanyi mjiangalie vema nafsi zenu,+ kwa sababu hamkuona umbo+ lolote katika siku ambayo Yehova alisema nanyi katika Horebu kutoka katikati ya moto,

  • Kumbukumbu la Torati 4:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Je, kundi lingine lolote la watu limesikia sauti ya Mungu ikisema kutoka katikati ya moto jinsi ambavyo wewe mwenyewe umeisikia, nao wakaendelea kuishi?+

  • Nehemia 9:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nawe ukashuka chini kwenye Mlima Sinai+ na kusema nao kutoka mbinguni+ na kuwapa maamuzi ya hukumu+ yaliyo manyoofu na sheria za kweli,+ masharti+ na amri+ nzuri.

  • Waebrania 12:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kwa maana ninyi hamkukaribia kile kinachoweza kuguswa+ na ambacho kimewashwa kwa moto,+ na wingu jeusi na giza zito na tufani,+

  • Waebrania 12:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Angalieni kwamba msimkatae yeye anayesema.+ Kwa maana ikiwa hawakuponyoka, wale waliomkataa yeye aliyekuwa akitoa onyo la kimungu duniani,+ sisi hatutaponyoka hata kidogo tukigeukia mbali kutoka kwake yeye anayesema kutoka mbinguni.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki