4 Na ikawa kwamba Yezebeli+ alipowakatilia mbali manabii+ wa Yehova, Obadia aliwachukua manabii 100, akawaficha wakiwa vikundi viwili vya watu 50 pangoni, naye akawapa mkate na maji.)+
19 Na sasa tuma watu, unikusanyie Israeli wote katika Mlima Karmeli+ na pia wale manabii 450 wa Baali+ na wale manabii 400 wa ule mti mtakatifu,+ wanaokula mezani pa Yezebeli.”+
7 Ndipo Yezebeli mke wake akamwambia: “Je, ni wewe unayetawala ukiwa mfalme juu ya Israeli?+ Amka, ule mkate na moyo wako ufurahi. Mimi mwenyewe nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.”+
25 Hakuna kamwe mtu yeyote ambaye amepata kuwa kama Ahabu,+ aliyejiuza ili kufanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova, ambaye Yezebeli+ mke wake alimchochea.+
30 Mwishowe Yehu akafika Yezreeli,+ na Yezebeli+ akasikia habari hizo. Naye akapaka macho yake wanja+ na kukipamba kichwa chake,+ akatazama chini kupitia dirishani.+
20 “ ‘Hata hivyo, nina hili dhidi yako, kwamba unamvumilia yule mwanamke Yezebeli,+ anayejiita mwenyewe nabii, naye anafundisha+ na kuwapotosha watumwa wangu+ wafanye uasherati+ na kula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu.+