13 Naye Yakobo akalala huko usiku huo. Kisha akachukua baadhi ya mali zake ili ampe zawadi Esau ndugu yake:+ 14 mbuzi jike 200, mbuzi dume 20, kondoo jike 200, kondoo dume 20, 15 ngamia 30 wanaonyonyesha, ng’ombe 40, ng’ombe dume 10, punda jike 20, na punda dume 10 waliokomaa.+