Kutoka 29:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 “Utamleta Haruni na wanawe kwenye mlango wa hema la mkutano+ na kuwaosha kwa maji.+ Kutoka 29:7 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 7 kisha chukua mafuta yanayotumiwa kutia mafuta+ na uyamimine juu ya kichwa chake na kumtia mafuta.+ Kutoka 30:30 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 30 Nawe utamtia mafuta Haruni+ na wanawe+ na kuwatakasa ili wanitumikie wakiwa makuhani.+ Kutoka 40:13 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 13 Utamvisha Haruni mavazi matakatifu+ na kumtia mafuta+ na kumtakasa, naye atanitumikia akiwa kuhani. Mambo ya Walawi 21:10 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 10 “‘Kuhani mkuu miongoni mwa ndugu zake, aliyetiwa mafuta kichwani+ na kuwekwa rasmi ili avae mavazi ya kuhani,+ anapaswa kutunza nywele zake na hapaswi kurarua mavazi yake.+ Zaburi 133:2 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 2 Ni kama mafuta bora yanayomiminwa kichwani+Yanayotiririka kwenye ndevu,Ndevu za Haruni,+Na kutiririka mpaka kwenye ukosi wa mavazi yake.
13 Utamvisha Haruni mavazi matakatifu+ na kumtia mafuta+ na kumtakasa, naye atanitumikia akiwa kuhani.
10 “‘Kuhani mkuu miongoni mwa ndugu zake, aliyetiwa mafuta kichwani+ na kuwekwa rasmi ili avae mavazi ya kuhani,+ anapaswa kutunza nywele zake na hapaswi kurarua mavazi yake.+
2 Ni kama mafuta bora yanayomiminwa kichwani+Yanayotiririka kwenye ndevu,Ndevu za Haruni,+Na kutiririka mpaka kwenye ukosi wa mavazi yake.