-
2 Mambo ya Nyakati 28:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Ahazi+ alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Hakutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova kama alivyotenda Daudi babu yake.+ 2 Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli,+ na hata alitengeneza sanamu za chuma*+ za Mabaali. 3 Isitoshe, alifukiza moshi wa dhabihu katika Bonde la Mwana wa Hinomu* na kuwateketeza wanawe motoni,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli. 4 Aliendelea pia kutoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu,+ kwenye vilima, na chini ya kila mti wenye majani mengi.+
-