-
Waebrania 10:5-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Basi anapokuja katika ulimwengu anasema: “‘Hukutaka dhabihu na toleo, bali ulinitayarishia mwili. 6 Hukukubali dhabihu nzima za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.’+ 7 Kisha nikasema: ‘Tazama! nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu) kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”+ 8 Kwanza aliposema: “Hukutaka wala hukukubali dhabihu, matoleo, dhabihu nzima za kuteketezwa, na dhabihu za dhambi”—dhabihu zinazotolewa kulingana na Sheria— 9 kisha anasema: “Tazama! nimekuja kufanya mapenzi yako.”+ Anaondoa la kwanza ili asimamishe la pili.
-