Mwanzo 4:5 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 5 lakini hakupendezwa hata kidogo na Kaini na dhabihu yake. Basi Kaini akawaka hasira kali na kusononeka.* Esta 5:9 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 9 Siku hiyo Hamani aliondoka akiwa na shangwe na uchangamfu moyoni. Lakini Hamani alipomwona Mordekai katika lango la mfalme na kutambua kwamba hakusimama wala kutetemeka alipomwona, Hamani alimkasirikia sana Mordekai.+ Methali 14:17 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 17 Yule anayekasirika upesi hutenda kipumbavu,+Lakini mtu anayechanganua mambo* huchukiwa. Methali 14:29 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 29 Mtu asiyekasirika upesi ana utambuzi mwingi,+Lakini asiye na subira hudhihirisha upumbavu.+ Methali 29:11 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Mtu mpumbavu humwaga hisia zake zote,*+Lakini mwenye hekima huzizuia kwa utulivu.+
5 lakini hakupendezwa hata kidogo na Kaini na dhabihu yake. Basi Kaini akawaka hasira kali na kusononeka.*
9 Siku hiyo Hamani aliondoka akiwa na shangwe na uchangamfu moyoni. Lakini Hamani alipomwona Mordekai katika lango la mfalme na kutambua kwamba hakusimama wala kutetemeka alipomwona, Hamani alimkasirikia sana Mordekai.+