-
Mathayo 21:23-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Baada ya kuingia hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakaja alipokuwa akifundisha, wakamuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”+ 24 Yesu akawajibu: “Nami nitawauliza swali. Mkinijibu basi nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani: 25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”* Lakini wakaanza kujadiliana kati yao wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Kwa nini hamkumwamini?’+ 26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunaogopa umati, kwa maana wote wanamwona Yohana kuwa nabii.” 27 Basi wakamjibu: “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia: “Nami siwaambii ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.
-
-
Luka 20:1-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Siku moja alipokuwa akifundisha watu hekaluni na kutangaza habari njema, wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wakaja, 2 nao wakasema: “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Au ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”+ 3 Akawajibu: “Mimi pia nitawauliza swali, nanyi mnijibu: 4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”* 5 Wakaanza kujadiliana kati yao wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Kwa nini hamkumwamini?’ 6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini Yohana alikuwa nabii.”+ 7 Basi wakamjibu kwamba hawajui chanzo chake. 8 Yesu akawaambia: “Nami siwaambii ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
-