26 Na yule atakayeshinda na kushika matendo yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,+27 kama vile nilivyopokea kutoka kwa Baba yangu, naye atawachunga watu kwa fimbo ya chuma+ hivi kwamba watavunjwa vipandevipande kama vyombo vya udongo.
21 Yule atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha ufalme.
6 Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza;+ kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka 1,000.+