AYUBU
1 Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi aliyeitwa Ayubu.*+ Alikuwa mtu mnyoofu na mtimilifu;*+ alimwogopa Mungu na kuepuka uovu.+ 2 Alikuwa na wana saba na mabinti watatu. 3 Mifugo yake ilikuwa kondoo 7,000, ngamia 3,000, ng’ombe 1,000,* na punda 500, naye alikuwa na watumishi wengi sana, na hivyo akawa mkuu kuliko watu wote wa Mashariki.
4 Kila mmoja wa wanawe alikuwa akifanya karamu katika nyumba yake siku yake iliyopangwa.* Nao walikuwa wakiwaalika dada zao watatu ili wale na kunywa pamoja nao. 5 Baada ya vipindi vya siku za karamu kwisha, Ayubu alikuwa akiwaita ili awatakase. Naye alikuwa akiamka asubuhi na mapema na kutoa dhabihu za kuteketezwa+ kwa ajili ya kila mmoja wao. Kwa maana Ayubu alisema: “Labda wanangu wametenda dhambi na kumtukana Mungu moyoni mwao.” Hivyo ndivyo Ayubu alivyofanya sikuzote.+
6 Basi siku ilifika ambayo wana wa Mungu*+ wa kweli waliingia na kusimama mbele za Yehova,+ Shetani+ pia akaingia kati yao.+
7 Ndipo Yehova akamuuliza Shetani: “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Yehova: “Nimetoka kuzururazurura na kutembeatembea duniani.”+ 8 Yehova akamwambia Shetani: “Je, umemwona* mtumishi wangu Ayubu? Hakuna yeyote aliye kama yeye duniani. Yeye ni mtu mnyoofu na mtimilifu,*+ anayemwogopa Mungu na kuepuka uovu.” 9 Ndipo Shetani akamjibu Yehova: “Je, Ayubu anamwogopa Mungu bure?+ 10 Je, wewe hukuweka ukuta wa ulinzi kumzunguka yeye+ na nyumba yake na kila kitu alicho nacho? Umeibariki kazi ya mikono yake,+ na mifugo yake imeenea nchini. 11 Lakini, ili mambo yabadilike, nyoosha mkono wako na upige kila kitu alicho nacho, na kwa hakika atakutukana mbele za uso wako mwenyewe.” 12 Kisha Yehova akamwambia Shetani: “Tazama! Kila kitu alicho nacho kimo mikononi mwako.* Ila tu usimguse mwanamume huyo!” Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele za* Yehova.+
13 Sasa siku ambayo wanawe na mabinti zake walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,+ 14 mjumbe akaja kwa Ayubu na kusema: “Ng’ombe walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha kando yao 15 Wasabea walipotushambulia na kuwachukua, wakawaua watumishi kwa upanga. Nimeponyoka mimi peke yangu, nami nimekuletea habari.”
16 Alipokuwa bado anaongea, mwingine akaja na kusema: “Moto kutoka kwa Mungu ulianguka kutoka mbinguni ukawateketeza* kabisa kondoo na watumishi! Nimeponyoka mimi peke yangu, nami nimekuletea habari.”
17 Alipokuwa bado anaongea, mwingine akaja na kusema: “Wakaldayo+ walijipanga katika makundi matatu, wakavamia ngamia na kuwachukua, nao wakawaua watumishi kwa upanga. Nimeponyoka mimi peke yangu, nami nimekuletea habari.”
18 Alipokuwa bado anaongea, mwingine akaja na kusema: “Wana wako na mabinti wako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa. 19 Kwa ghafla upepo mkali ukaja kutoka nyikani, ukapiga pembe nne za nyumba hiyo, ikawaangukia vijana hao, nao wakafa. Nimeponyoka mimi peke yangu, nami nimekuletea habari.”
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua vazi lake na kunyoa nywele za kichwa chake; kisha akaanguka chini, akainama 21 na kusema:
“Nilitoka tumboni mwa mama yangu nikiwa uchi,
Nami nitarudi nikiwa uchi.+
Yehova ametoa,+ na Yehova amechukua.
Jina la Yehova na liendelee kusifiwa.”
22 Katika hayo yote, Ayubu hakutenda dhambi wala hakumlaumu Mungu kwa kutenda jambo lolote baya.*
2 Baadaye siku ilifika ambayo wana wa Mungu wa kweli*+ waliingia na kusimama mbele za Yehova,+ na Shetani pia akaingia kati yao na kusimama mbele za Yehova.+
2 Ndipo Yehova akamuuliza Shetani: “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Yehova: “Nimetoka kuzururazurura na kutembeatembea duniani.”+ 3 Yehova akamwambia Shetani: “Je, umemwona* mtumishi wangu Ayubu? Hakuna yeyote aliye kama yeye duniani. Yeye ni mtu mnyoofu na mtimilifu,*+ anayemwogopa Mungu na kuepuka uovu. Bado anashika kabisa utimilifu+ wake, hata ingawa unajaribu kunichochea dhidi yake+ ili nimwangamize* bila sababu.” 4 Lakini Shetani akamjibu Yehova: “Ngozi kwa ngozi. Mtu atatoa kila kitu alicho nacho ili aokoe uhai wake.* 5 Lakini, ili mambo yabadilike, nyoosha mkono wako upige mfupa na nyama yake, na kwa hakika atakutukana mbele za uso wako mwenyewe.”+
6 Ndipo Yehova akamwambia Shetani: “Tazama! Yumo mikononi mwako! Ila tu usiondoe uhai wake!”* 7 Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele za* Yehova, akampiga Ayubu kwa majipu yenye maumivu makali*+ kuanzia wayo wa mguu mpaka utosini. 8 Na Ayubu akachukua kigae na kukitumia kujikuna, naye aliketi kwenye majivu.+
9 Hatimaye mke wake akamwambia: “Je, bado unashika kabisa utimilifu wako? Mtukane Mungu, ufe!” 10 Lakini akamwambia: “Unazungumza kama mmojawapo wa wanawake wapumbavu. Je, tukubali tu mambo mema kutoka kwa Mungu wa kweli, tusikubali pia mambo mabaya?”+ Licha ya hayo yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa midomo yake.+
11 Marafiki watatu wa Ayubu wakasikia kuhusu misiba yote iliyompata Ayubu, kila mmoja wao akaja kutoka nyumbani kwake—Elifazi+ Mtemani, Bildadi+ Mshua,+ na Sofari+ Mnaamathi. Basi wakakubaliana kukutana ili waende kumpa pole na kumfariji Ayubu. 12 Walipomwona kwa mbali, hawakumtambua. Wakaanza kulia kwa sauti kubwa na kurarua mavazi yao, wakarusha mavumbi hewani na juu ya vichwa vyao.+ 13 Kisha wakaketi ardhini pamoja naye kwa siku saba, mchana na usiku. Hakuna yeyote kati yao aliyemwambia neno lolote kwa sababu waliona kwamba alikuwa na maumivu makali sana.+
3 Baada ya hayo Ayubu alianza kuongea na kuilaani siku aliyozaliwa.*+ 2 Ayubu akasema:
4 Siku hiyo na iwe giza.
Mungu aliye juu asiihangaikie siku hiyo;
Na nuru isiiangazie.
5 Na imilikiwe na giza zito sana.*
Wingu la mvua na litande juu yake.
Na chochote kinacholeta giza mchana kiitie hofu siku hiyo.
6 Usiku huo—na ushikwe na giza;+
Na isishangilie miongoni mwa siku nyingine za mwaka,
Nayo isihesabiwe miongoni mwa siku za miezi.
7 Kwa kweli! Usiku huo na uwe tasa;
Kelele za shangwe zisisikiwe usiku huo.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza;
Usiku huo ungojee nuru bila mafanikio,
Nao usione miale ya mapambazuko.
10 Kwa maana haukufunga milango ya tumbo la uzazi la mama yangu;+
Wala haukuficha taabu kutoka machoni pangu.
11 Kwa nini sikufa nilipozaliwa?
Kwa nini sikuangamia nilipotoka tumboni?+
12 Kwa nini mama yangu alinipakata mapajani
Na kuninyonyesha?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimelala chini bila usumbufu;+
Ningekuwa nimelala na kupumzika+
14 Pamoja na wafalme wa dunia na washauri wao,
Waliojijengea majengo ambayo sasa ni magofu,*
15 Au pamoja na wakuu waliomiliki dhahabu,
Ambao nyumba zao zilijaa fedha.
16 Au kwa nini sikuwa kama mimba iliyoharibika ambayo imefichika,
Kama watoto ambao hawajawahi kamwe kuona nuru?
18 Humo wafungwa hukaa pamoja kwa utulivu;
Hawasikii sauti ya mtu anayewalazimisha kufanya kazi.
21 Kwa nini wanatamani sana kifo, lakini hakiji?+
Wanachimba wakikitafuta kuliko hazina zilizofichika,
22 Wale wanaoshangilia sana,
Wanaofurahi wanapopata kaburi.
24 Kwa maana badala ya chakula changu majonzi hunijia,+
Na kilio changu cha uchungu+ humwagika kama maji.
25 Kwa maana ninachoogopa sana kimenijia,
Na ninachohofu kimenipata.
26 Sijawa na amani, wala utulivu, wala sijapumzika,
Lakini taabu inaendelea kuniandama.”
4 Kisha Elifazi+ Mtemani akajibu:
2 “Mtu akijaribu kuongea nawe, je, utakosa subira?
Kwa maana ni nani anayeweza kujizuia kuongea?
3 Ni kweli, umewarekebisha wengi,
Nawe ulikuwa ukiimarisha mikono iliyo dhaifu.
4 Maneno yako yalimwinua yeyote aliyejikwaa,
Nawe uliwatia nguvu waliokuwa na magoti dhaifu.
5 Lakini sasa yamekupata wewe, nawe unalemewa;*
Yanakugusa, nawe unashuka moyo.
6 Je, hofu yako kwa Mungu haikupi ujasiri?
Je, njia yako ya utimilifu+ haikupi tumaini?
7 Kumbuka, tafadhali: Ni mtu gani asiye na hatia ambaye amewahi kuangamia?
Tangu lini wanyoofu wakaangamizwa?
8 Jambo ambalo nimeona ni kwamba wale wanaolima* madhara
Na wale wanaopanda taabu watavuna mambo hayohayo.
9 Kwa pumzi ya Mungu wanaangamia,
Na kwa mlipuko wa hasira yake wanafikia mwisho wao.
11 Simba hufa kwa kukosa mawindo,
Na wanasimba hutawanyika.
12 Sasa niliambiwa neno kwa siri,
Na sikio langu lilisikia mnong’ono wake.
13 Katika maono ya usiku yenye kufadhaisha,
Watu wanapolala usingizi mzito,
14 Nilitetemeka kwelikweli,
Mifupa yangu yote ikajaa hofu.
15 Roho fulani alipita mbele ya uso wangu;
Nywele za mwili wangu zikasimama.
16 Kisha akasimama tuli,
Lakini sikutambua sura yake.
Umbo fulani lilikuwa mbele ya macho yangu;
Kulikuwa na utulivu, kisha nikasikia sauti:
17 ‘Je, mwanadamu anayeweza kufa anaweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu?
Je, mtu anaweza kuwa safi kuliko Muumba wake?’
19 Sembuse wale wanaokaa katika nyumba za udongo,
Ambao msingi wao umo mavumbini,+
Wanaopondwa kwa urahisi kama nondo!*
20 Wanapondwa kabisa kuanzia asubuhi mpaka jioni;
Wanaangamia milele, na hakuna yeyote anayetambua hilo.
21 Je, wao si kama hema ambalo kamba yake imeng’olewa?
Wanakufa bila hekima.
5 “Ita, tafadhali! Je, kuna yeyote anayekujibu?
Ni mtakatifu gani utakayemlilia?
2 Kwa maana kinyongo kitamuua mpumbavu,
Na wivu utamwangamiza mjinga.
3 Nimemwona mpumbavu akitia mizizi,
Lakini kwa ghafla makao yake yanalaaniwa.
5 Mwenye njaa hula anachovuna,
Hukichukua hata katikati ya miiba,
Na mtego umetegwa ili kunasa mali zao.
6 Kwa maana mambo yenye kudhuru hayaoti mavumbini,
Na taabu haichipuki ardhini.
7 Kwa maana mwanadamu huzaliwa ili ataabike,
Hilo ni hakika kama cheche za moto zinavyoruka juu.
8 Lakini mimi ningemsihi Mungu,
Nami ningewasilisha kesi yangu kwa Mungu,
9 Kwa Yule anayetenda mambo makuu na yasiyochunguzika,
Mambo yenye kustaajabisha yasiyohesabika.
10 Yeye huleta mvua duniani
Na kupeleka maji mashambani.
11 Humwinua juu mtu wa hali ya chini,
Humwinua aliyehuzunika na kumwokoa.
12 Huvuruga njama za wenye hila,
Ili kazi ya mikono yao isifanikiwe.
14 Wao hukutana na giza wakati wa mchana,
Nao hupapasa-papasa wakati wa adhuhuri kana kwamba ni usiku.
15 Huokoa kutokana na upanga wa kinywa chao,
Humwokoa maskini kutoka katika mkono wa mwenye nguvu,
16 Hivi kwamba kuna tumaini kwa mtu wa hali ya chini,
Lakini kinywa cha uovu hufumbwa.
17 Tazama! Mwenye furaha ni mtu ambaye Mungu humkaripia;
Basi usikatae nidhamu ya Mweza-Yote!
18 Kwa maana yeye husababisha maumivu, lakini hufunga jeraha;
Huvunja, lakini huponya kwa mikono yake.
19 Atakuokoa katika misiba sita,
Hata wa saba hautakudhuru.
20 Wakati wa njaa kali atakukomboa kutoka katika kifo,
Na kutoka katika nguvu za upanga wakati wa vita.
22 Utacheka maangamizi na njaa,
Wala hutawaogopa wanyama wa mwituni walio duniani.
25 Utakuwa na watoto wengi,
Na wazao wako watakuwa wengi kama mimea duniani.
26 Utaingia kaburini ukiwa bado na nguvu,
Kama masuke ya nafaka yanayokusanywa wakati wa mavuno.
27 Tazama! Tumechunguza jambo hili, na ndivyo lilivyo.
Sikiliza na ulikubali.”
6 Kisha Ayubu akajibu:
3 Kwa maana sasa ni mazito kuliko mchanga wa bahari.
Ndiyo sababu maneno yangu yamekuwa mazungumzo ya ovyoovyo.*+
4 Kwa maana mishale ya Mweza-Yote imenichoma,
Na roho yangu inakunywa sumu yake;+
Vitisho vya Mungu vinaniandama.
6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi,
Au maji ya mholi yana ladha?
7 Nimekataa kugusa vitu vya aina hiyo.
Ni kama uchafu katika chakula changu.
8 Laiti ombi langu lingejibiwa
Na laiti Mungu angenipa ninachotamani!
10 Kwa maana hata hilo lingenifariji;
Ningeruka kwa shangwe licha ya maumivu yangu yasiyokwisha,
Kwa maana sijayakana maneno ya Aliye Mtakatifu.+
11 Je, nina nguvu za kuendelea kungoja?+
Na ni mwisho gani unaonisubiri, hivi kwamba niendelee kuishi?*
12 Je, nguvu zangu ni kama za mwamba?
Au mwili wangu umetengenezwa kwa shaba?
13 Je, kuna njia yoyote ninayoweza kujisaidia mwenyewe
Wakati nimenyang’anywa njia zangu zote za kujitegemeza?
14 Yeyote anayekataa kumtendea mwanadamu mwenzake kwa upendo mshikamanifu+
Ataacha kumwogopa Mweza-Yote.+
15 Ndugu zangu wenyewe wamekuwa na hila+ kama kijito cha majira ya baridi kali,
Kama maji ya vijito vya majira ya baridi kali yanayokauka.
16 Vimekuwa vyeusi kwa sababu ya barafu,
Na theluji inayoyeyuka imejificha ndani yake.
17 Lakini katika majira ya kiangazi vinakauka na kutoweka;
Joto linapoongezeka, vinakauka.
18 Mikondo yake hugeuka;
Navyo huelekea jangwani na kutoweka.
20 Wameaibika kwa sababu hawakupata walichotumaini;
Wanafika hapo na kukata tamaa tu.
22 Je, nimewaambia, ‘Nipeni kitu fulani,’
Au kuwaomba zawadi yoyote kutoka katika mali zenu?
25 Maneno ya unyoofu hayaumizi!+
Lakini karipio lenu lina faida gani?+
26 Je, mnapanga njama ya kukosoa maneno yangu,
Maneno ya mtu aliyekata tamaa,+ yanayopeperushwa mbali na upepo?
28 Basi sasa geukeni mnitazame,
Kwa maana siwezi kusema uwongo mbele yenu.
29 Fikirieni tena, tafadhali—msinielewe vibaya—
Naam, fikirieni tena, kwa maana mimi bado ni mwadilifu.
30 Je, ulimi wangu unasema jambo lisilo la haki?
Je, mdomo wangu hautambui* kwamba kuna jambo ambalo si sawa?
7 “Je, maisha ya mwanadamu anayeweza kufa si kama kazi ya kulazimishwa,
Na siku zake kama siku za kibarua?+
4 Ninapolala mimi huuliza, ‘Nitaamka wakati gani?’+
Lakini kadiri usiku unavyojikokota, ndivyo ninavyogaagaa hadi alfajiri.*
11 Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu.
12 Je, mimi ni bahari au mnyama mkubwa sana wa baharini,
Hivi kwamba uniwekee mlinzi?
13 Ninaposema, ‘Kochi langu litanifariji;
Kitanda changu kitasaidia kupunguza mateso yangu,’
14 Kisha unanitisha kwa ndoto
Na kuniogopesha kwa maono,
15 Hivi kwamba natamani kusongwa pumzi,
16 Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi.
Niache, kwa maana siku zangu ni kama pumzi.+
20 Ikiwa nimetenda dhambi, ninawezaje kukudhuru wewe, Mchunguzaji wa wanadamu?+
Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?
Je, nimekuwa mzigo kwako?
21 Kwa nini husamehi dhambi yangu
Na kuachilia kosa langu?
Kwa maana hivi punde nitalala mavumbini,+
Nawe utanitafuta, lakini nitakuwa nimeenda zangu.”
8 Kisha Bildadi+ Mshua+ akajibu:
2 “Utaendelea kuongea kwa njia hiyo mpaka lini?+
Maneno ya kinywa chako ni upepo wenye nguvu!
3 Je, Mungu atapotosha haki,
Au, je, Mweza-Yote atapotosha uadilifu?
Na kumsihi Mweza-Yote upate kibali chake,
6 Na ikiwa kwa kweli ungekuwa safi na mnyoofu,+
Angekusikiliza*
Na kukurudisha mahali unapostahili.
9 Kwa maana tulizaliwa jana tu, nasi hatujui lolote,
Kwa sababu siku zetu duniani ni kivuli.
11 Je, mafunjo yanaweza kusitawi katika eneo lisilo na umajimaji?
Je, utete unaweza kusitawi bila maji?
12 Hata kabla haujachanua, kabla haujakatwa,
Utakauka kabla ya mmea mwingine wowote.
13 Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa* wote wanaomsahau Mungu,
Kwa maana tumaini la wanaomkataa Mungu* litapotea,
14 Ambao tegemeo lao ni ubatili
Na ambao tumaini lao ni hafifu kama utando wa* buibui.
15 Ataegemea nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;
Atajaribu kuishikilia, lakini haitadumu.
18 Lakini anapong’olewa* kutoka mahali pake,
Mahali hapo patamkana na kusema, ‘Sijawahi kamwe kukuona.’+
20 Kwa hakika Mungu hatawakataa watu wanaoshika utimilifu;*
Wala hatawaunga mkono* waovu,
21 Kwa maana bado atakijaza kinywa chako kicheko
Na midomo yako kelele za shangwe.
22 Wale wanaokuchukia watavishwa aibu,
Na hema la waovu halitakuwapo tena.”
9 Ayubu akajibu:
2 “Kwa kweli ninajua hivyo ndivyo ilivyo.
Lakini mwanadamu anayeweza kufa anawezaje kuwa mwadilifu katika kesi na Mungu?+
3 Mtu akitaka kubishana Naye,*+
Mtu huyo hawezi kujibu hata swali moja kati ya maswali Yake elfu moja.
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni na ana nguvu nyingi sana.+
Ni nani anayeweza kumpinga na asipate madhara?+
7 Huliamuru jua lisiangaze
Naye huziba kabisa nuru ya nyota;+
8 Huzitandaza mbingu akiwa peke yake,+
Naye hukanyaga mawimbi makubwa ya bahari.+
9 Aliumba kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+
Na makundi ya nyota yaliyo katika anga la kusini;*
10 Hufanya mambo makuu yasiyochunguzika,+
Mambo yenye kustaajabisha yasiyoweza kuhesabiwa.+
11 Yeye hupita karibu nami, lakini siwezi kumwona;
Hupita mbele yangu, lakini siwezi kumtambua.
12 Anapochukua kitu kwa ghafla, ni nani anayeweza kumzuia?
Ni nani anayeweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+
14 Sembuse ninapomjibu
Ni lazima nichague maneno yangu kwa uangalifu ili kujadiliana naye!
15 Hata kama singekuwa na kosa, singemjibu.+
Ningemsihi tu mwamuzi* wangu anionyeshe rehema.
16 Nikimwita, je, atanijibu?
Siamini kwamba atasikiliza sauti yangu,
17 Kwa maana yeye huniponda kwa dhoruba
Naye huzidisha majeraha yangu bila sababu.+
18 Haniruhusu nipumue;
Huendelea kunijaza mambo machungu.
19 Kama ni nguvu, yeye ndiye mwenye nguvu.+
Kama ni haki, anauliza: ‘Ni nani anayeweza kunishtaki?’*
20 Kama singekuwa na kosa, kinywa changu mwenyewe kingenishutumu;
Hata nikishika utimilifu wangu,* atanitangaza kuwa mwenye hatia.*
21 Hata nikishika utimilifu wangu,* sijiamini;*
Ninakataa* maisha haya yangu.
23 Mafuriko ya ghafla yakisababisha kifo ghafla,
Ataidhihaki hali ya kukata tamaa ya watu wasio na hatia.
Kama si yeye, ni nani basi?
26 Zinanyiririka kama mashua za matete,
Kama tai wanaoshuka kwa ghafla kukamata mawindo yao.
27 Nikisema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,
Nitabadili hali ya uso wangu na kuwa mchangamfu,’
28 Bado nitaogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+
Nami najua hutanipata bila hatia.
Basi kwa nini nitaabike bure?+
30 Nikioga kwa maji ya theluji inayoyeyuka,
Na kunawa mikono yangu kwa sabuni,*+
31 Wewe utanitumbukiza shimoni,
Hivi kwamba hata mavazi yangu mwenyewe yatanichukia.
Na kuacha kuniogopesha kwa vitisho vyake,+
35 Ndipo ningeongea naye bila woga,
Kwa sababu sijazoea kuongea kwa woga.
10 “Nayachukia sana* maisha yangu.+
Nitamwaga malalamiko yangu.
Nitasema waziwazi katika mateso yangu makali!*
2 Nitamwambia Mungu: ‘Usinitangaze kuwa mwenye hatia.
Niambie kwa nini unapambana nami.
3 Je, unafaidika unaponikandamiza,
Unapodharau kazi ya mikono yako+
Huku ukipendelea ushauri wa waovu?
4 Je, una macho ya kimwili,
Au je, unaona kama mwanadamu anayeweza kufa anavyoona?
5 Je, siku zako ni kama siku za wanadamu wanaoweza kufa,
Au je, miaka yako ni kama ya mwanadamu,+
6 Hivi kwamba utafute kosa langu
Na kuendelea kutafuta dhambi yangu?+
10 Je, hukunimwaga kama maziwa
Na kunigandisha kama jibini?
13 Lakini ulikusudia kwa siri kufanya mambo haya.*
Najua kwamba mambo haya yametoka kwako.
15 Kama nina hatia, ole wangu!
17 Unaleta mashahidi wapya dhidi yangu
Na kuzidisha hasira yako dhidi yangu,
Huku shida baada ya shida ikinikabili.
18 Basi kwa nini ulinitoa katika tumbo la mama yangu?+
Laiti ningekufa kabla ya jicho lolote kuniona.
19 Ingekuwa kana kwamba sikuwahi kuwepo;
Ningetolewa moja kwa moja tumboni na kupelekwa kaburini.’
20 Je, siku zangu si chache?+ Naomba aniache;
Na ayageuze macho yake mbali nami, ili nipate kitulizo kidogo*+
21 Kabla sijaenda zangu—nami sitarudi+—
Katika nchi yenye giza zito kabisa,*+
22 Kwenye nchi yenye giza totoro,
Nchi ya kivuli kizito na vurugu,
Ambako hata nuru ni kama giza.”
3 Je, maneno yako yasiyo na maana yatawanyamazisha watu?
Unadhani hakuna atakayekukemea kwa sababu ya maneno yako ya dhihaka?+
6 Ndipo angekufunulia siri za hekima,
Kwa maana hekima inayotumika ina vipengele vingi.
Kisha ungetambua kwamba Mungu huruhusu baadhi ya makosa yako yasahauliwe.
8 Hekima yake iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kutimiza nini?
Ina kina kuliko Kaburi.* Wewe unaweza kujua nini?
9 Ni ndefu kuliko dunia
Na pana kuliko bahari.
10 Akipita na kumkamata mtu na kuweka kikao cha mahakama,
Ni nani anayeweza kumpinga?
11 Kwa maana anajua watu wanapokuwa wadanganyifu.
Akiona uovu, je, hatautambua?
13 Laiti ungeutayarisha moyo wako
Na kumnyooshea mikono yako.
14 Ikiwa mkono wako unatenda mabaya, utupilie mbali,
Nawe usiruhusu uovu ukae katika mahema yako.
15 Ndipo utakapoinua uso wako bila lawama;
Utaweza kusimama imara, bila woga.
16 Ndipo utakapoisahau taabu yako;
Utaikumbuka kama maji yaliyopita karibu nawe na kwenda zake.
17 Maisha yako yatang’aa kuliko adhuhuri;
Hata giza lake litakuwa kama asubuhi.
18 Utakuwa na ujasiri kwa sababu kuna tumaini,
Nawe utatazama huku na huku na kulala kwa usalama.
19 Utalala na hakuna yeyote atakayekuogopesha,
Na watu wengi watajipendekeza kwako.
20 Lakini macho ya waovu yatadhoofika;
Nao hawatapata mahali pa kukimbilia,
Na tumaini lao pekee litakuwa kifo.”+
12 Kisha Ayubu akajibu:
3 Lakini mimi pia nina uelewaji.*
Mimi si duni kwenu.
Ni nani asiyejua mambo haya?
Mtu mwadilifu na asiye na lawama ni kichekesho.
5 Mtu asiye na mahangaiko hudharau msiba,
Akifikiri kwamba msiba huwajia tu wale ambao miguu yao inayumbayumba.*
Na wale wanaomkasirisha Mungu wako salama,+
Wale wanaobeba mungu wao mikononi mwao.
7 Lakini, tafadhali, waulize wanyama, nao watakufundisha;
Pia ndege wa angani, nao watakwambia.
9 Ni nani kati ya hao wote asiyejua
Kwamba mkono wa Yehova umefanya haya?
12 Je, hekima haipatikani miongoni mwa waliozeeka,+
Na je, uelewaji hauji kwa sababu ya kuishi muda mrefu?
16 Ana nguvu na hekima inayotumika;+
Anayepotosha na anayepotoshwa wote ni wake;
17 Huwafanya washauri watembee bila viatu,*
Naye huwafanya waamuzi waonekane wapumbavu.+
19 Huwafanya makuhani watembee bila viatu,+
Naye huwapindua walio imara kabisa katika mamlaka;+
20 Huwanyamazisha washauri wanaotegemeka
Na kuwapokonya wanaume wazee* busara;
Naye huwafanya wenye nguvu wawe dhaifu;*
22 Hufunua mambo yenye kina kutoka gizani,+
Naye huleta giza zito kwenye nuru;
23 Huyafanya mataifa yawe na nguvu ili ayaangamize;
Huyafanya mataifa yawe makubwa ili ayapeleke uhamishoni.
13 “Naam, jicho langu limeona hayo yote,
Sikio langu limesikia na kuyaelewa.
2 Mnayojua, mimi pia nayajua;
Mimi si duni kwenu.
6 Tafadhali, sikilizeni hoja zangu,
Na msikilize ninapojitetea kwa midomo yangu.
7 Je, mtasema mambo yasiyo ya haki kwa niaba ya Mungu,
Na je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa ajili yake?
9 Je, mambo yatawaendea vyema akiwachunguza?+
Je, mtamdanganya kama mnavyomdanganya mwanadamu anayeweza kufa?
11 Je, adhama yake mwenyewe haitawaogopesha
Na hofu yake haitawaangukia?
13 Nyamazeni mbele yangu, ili niongee.
Kisha na yanipate yatakayonipata!
16 Ndipo atakapokuwa wokovu wangu,+
Kwa maana hakuna mtu aliyemkataa Mungu* anayeweza kuja mbele zake.+
17 Sikilizeni kwa makini neno langu;
Sikilizeni tangazo langu.
18 Sasa tazameni, nimetayarisha kesi yangu;
Najua sina kosa.
19 Ni nani atakayepambana nami?
Nitakufa, ikiwa nitanyamaza!*
22 Niite nami nitakujibu,
Au acha nizungumze, nawe unijibu.
23 Nimefanya makosa na dhambi gani?
Nifunulie kosa langu na dhambi yangu.
25 Je, utajaribu kulitisha jani linalopeperushwa na upepo
Au kuyakimbiza majani makavu?
26 Kwa maana unaendelea kuandika mashtaka makali dhidi yangu,
Nawe unanifanya niwajibike kwa sababu ya dhambi nilizofanya nilipokuwa kijana.
27 Umeitia miguu yangu katika mikatale,
Unavichunguza kwa makini vijia vyangu vyote,
Nawe unafuata kila wayo wa mguu wangu.
2 Huchanua kama ua na kisha hunyauka;*+
Hukimbia kama kivuli na kutoweka.+
4 Ni nani anayeweza kutokeza mtu safi kutokana na mtu asiye safi?+
Hakuna awezaye!
5 Ikiwa siku zake zinajulikana,
Basi unajua idadi ya miezi yake;
Umemwekea mpaka ambao hawezi kuvuka.+
7 Kwa maana hata mti una tumaini.
Ukikatwa, utachipuka tena,
Na matawi yake yataendelea kukua.
8 Mizizi yake ikizeekea ardhini
Na kisiki chake kikifia udongoni,
9 Utachipuka unaponusa maji;
Nao utatokeza matawi kama mmea mpya.
11 Maji hutoweka baharini,
Na maji ya mto hupungua na kukauka.
12 Mwanadamu pia hulala naye haamki.+
Mpaka mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka,
Wala hawataamshwa kutoka katika usingizi wao.+
13 Laiti ungenificha Kaburini,*+
Ungenificha mpaka hasira yako ipite,
Laiti ungenipimia wakati hususa na kunikumbuka!+
14 Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?+
Nitangojea sikuzote za utumishi wangu wa kulazimishwa
Mpaka kitulizo changu kitakapokuja.+
Utaitamani sana* kazi ya mikono yako.
16 Lakini sasa, unaendelea kuhesabu kila hatua yangu;
Unatafuta tu dhambi zangu.
17 Kosa langu limefungiwa katika mfuko,
Nawe unaufunga uovu wangu kwa gundi.
18 Kama mlima unavyoanguka na kuporomoka
Na mwamba unavyong’oka mahali pake,
19 Kama maji yanavyomomonyoa mawe
Na mafuriko yanavyosomba udongo,
Ndivyo ulivyoharibu tumaini la mwanadamu anayeweza kufa.
2 “Je, mtu mwenye hekima atajibu kwa hoja zisizo na maana,*
Au, je, atajaza tumbo lake upepo wa mashariki?
3 Kukaripia kwa maneno matupu ni jambo lisilo na maana,
Na kuzungumza tu hakuna faida yoyote.
4 Kwa maana unafanya watu wasimwogope Mungu,
Na kuwazuia wasitafakari kamwe kumhusu Mungu.
6 Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si mimi;
Midomo yako mwenyewe inatoa ushahidi dhidi yako.+
7 Je, wewe ndiye mwanadamu wa kwanza kuzaliwa,
Au ulizaliwa kabla ya vilima?
8 Je, wewe husikiliza mazungumzo ya siri ya Mungu,
Au ni wewe peke yako mwenye hekima?
9 Unajua nini ambacho sisi hatujui?+
Unaelewa nini ambacho sisi hatuelewi?
11 Je, hutosheki na faraja za Mungu,
Au maneno ya upole unayoambiwa?
12 Kwa nini moyo wako unakupeperusha,
Na kwa nini macho yako yanawaka kwa hasira?
13 Kwa maana unaifanya roho yako imkasirikie Mungu,
Nawe unaruhusu maneno ya aina hiyo yatoke katika kinywa chako mwenyewe.
14 Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hata awe safi,
Au yeyote anayezaliwa na mwanamke ni nini hata awe mwadilifu?+
17 Nitakujulisha; nisikilize!
Nitasimulia mambo niliyoona,
18 Mambo ambayo watu wenye hekima wamejifunza kutoka kwa baba zao,+
Mambo ambayo hawakuficha.
19 Ni wao peke yao waliopewa nchi,
Na hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao.
20 Mtu mwovu huteseka siku zake zote,
Miaka yote aliyotengewa mkandamizaji.
23 Hutangatanga akitafuta chakula*—kiko wapi?
Anajua vizuri kwamba siku ya giza iko karibu.
24 Taabu na maumivu makali huendelea kumtisha;
Humshinda nguvu kama mfalme aliye tayari kushambulia.
25 Kwa maana yeye huunyoosha mkono wake dhidi ya Mungu mwenyewe
Na kujaribu kumpinga* Mweza-Yote;
26 Hukimbia kwa ukaidi kumshambulia Yeye,
Akiwa na ngao yake nene, iliyo imara;*
27 Uso wake umefunikwa kwa mafuta,
Na kiuno chake kimepanuka kwa mafuta;
28 Hukaa katika majiji yatakayoangamizwa,
Katika nyumba ambazo hazitakaliwa na yeyote,
Ambazo zitakuwa marundo ya mawe.
29 Hatatajirika, na mali zake hazitaongezeka,
Wala vitu anavyomiliki havitaenea nchini.
30 Hatakimbia kutoka gizani;
Mwali wa moto utakausha tawi lake,*
Naye atatoweka kwa kishindo cha pumzi ya kinywa cha Mungu.*+
31 Hapaswi kukengeushwa na kutumaini mambo yasiyo na thamani,
Kwa sababu atakachopata badala yake hakitakuwa na thamani;
32 Hilo litatendeka kabla ya siku yake,
Na matawi yake hayatasitawi kamwe.+
33 Atakuwa kama mzabibu unaoangusha zabibu zake mbichi,
Na kama mzeituni unaoangusha maua yake.
35 Wanatunga mimba ya matatizo na kuzaa uovu,
Na tumbo lao la uzazi huzaa udanganyifu.”
16 Ayubu akajibu:
2 “Nimeshasikia mambo mengi kama hayo.
Ninyi nyote ni wafariji wasumbufu!+
3 Je, maneno yasiyo na maana* yana mwisho?
Ni nini kinachowachochea kujibu hivi?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi.
Ikiwa mngekuwa katika hali yangu,*
Ningetoa hoja zenye kusadikisha dhidi yenu
Na kuwatikisia kichwa changu.+
5 Hata hivyo, badala yake, ningewaimarisha kwa maneno ya kinywa changu,
Na faraja ya midomo yangu ingewatuliza.+
6 Nikiongea, maumivu yangu mwenyewe hayatulii,+
Nami nikiacha kuongea, maumivu yangu yanapungua kwa kadiri gani?
8 Pia unanikamata, na wengine wameshuhudia jambo hilo,
Hivi kwamba kukonda kwangu kumezidi na kunatoa ushahidi mbele yangu.
9 Hasira yake imenirarua vipandevipande, naye ana chuki kunielekea.+
Hunisagia meno yake.
Adui yangu hunitoboa kwa macho yake.+
10 Wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yangu,+
Nao wameyapiga mashavu yangu kwa dharau;
Wanakusanyika kwa wingi dhidi yangu.+
12 Nilikuwa na amani, lakini akanivunjavunja;+
Alinikamata nyuma shingoni na kunipondaponda;
Kisha akanifanya shabaha yake.
13 Wapiga mishale wake wananizunguka;+
Huzichoma figo+ zangu bila huruma;
Humwaga nyongo yangu ardhini.
14 Hunitoboa tena na tena kama ukuta;
Hunishambulia kama shujaa.
16 Uso wangu ni mwekundu kwa sababu ya kulia,+
Na kuna kivuli kizito* juu ya kope zangu,
17 Ingawa mikono yangu haijatenda ukatili wowote
Na sala yangu ni safi.
18 Ee dunia, usiifunike damu yangu!+
Acha kilio changu kisiwe na mahali pa kupumzikia!
19 Hata sasa, shahidi wangu yuko mbinguni;
Yule anayeweza kunitetea yuko juu.
21 Acha mtu fulani awe mwamuzi kati ya mwanadamu na Mungu,
Kama anavyoweza kuwa mwamuzi kati ya mtu mmoja na mwenzake.+
3 Tafadhali ikubali dhamana yangu, na ukae nayo.
Ni nani mwingine atakayenipa mkono wake na kutoa dhamana kwa niaba yangu?+
5 Huenda akajitolea kushiriki vitu vyake na rafiki zake,
Huku macho ya watoto wake yakidhoofika.
6 Amenifanya niwe kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+
Hivi kwamba nikawa mtu wanayemtemea mate usoni.+
8 Watu wanyoofu wananitazama kwa mshangao,
Na asiye na hatia anasumbuka kwa sababu ya mtu anayemkataa Mungu.*
10 Hata hivyo, nyote mnaweza kuja na kuendelea kunishambulia kwa hoja zenu,
Kwa maana sijamwona yeyote mwenye hekima miongoni mwenu.+
12 Wanaendelea kufanya usiku uwe mchana,
Wakisema, ‘Bila shaka mwangaza unakaribia kwa sababu kuna giza.’
14 Nitaliambia shimo*+ kwa sauti, ‘Wewe ni baba yangu!’
Na mabuu, ‘Ninyi ni mama yangu na dada yangu!’
15 Basi, tumaini langu liko wapi?+
Ni nani anayeweza kuona tumaini hilo?
2 “Utaendelea kusema maneno haya mpaka lini?
Onyesha uelewaji kidogo ili nasi tuseme.
4 Hata ukijirarua* vipandevipande kwa hasira,
Je, dunia itaachwa kwa ajili yako,
Au mwamba kuhama mahali pake?
6 Hakika nuru iliyo ndani ya hema lake itakuwa giza,
Na taa iliyo juu yake itazimwa.
8 Kwa maana miguu yake itamwongoza kwenye wavu,
Naye atatangatanga kwenye kamba za wavu.
10 Kamba imefichwa ardhini kwa ajili yake,
Na mtego uko kwenye kijia chake.
16 Chini yake, mizizi yake itakauka,
Na juu yake, matawi yake yatanyauka.
20 Siku yake itakapofika, watu wa Magharibi watashtuka sana
Na watu wa Mashariki watashikwa na hofu.
21 Hivyo ndivyo inavyokuwa kwa mahema ya mkosaji
Na kwa makao ya mtu ambaye hajamjua Mungu.”
19 Ayubu akajibu:
4 Na ikiwa kwa kweli nilifanya kosa,
Ni kosa langu mimi mwenyewe.
5 Ikiwa mnasisitiza kujikweza juu yangu,
Mkidai kwamba mna haki ya kunishutumu,
6 Basi, jueni kwamba Mungu ndiye amenipotosha,
Naye ameninasa katika wavu wake wa kuwindia.
7 Tazameni! Naendelea kulia kwa sauti, ‘Ukatili!’ lakini sijibiwi;+
Naendelea kulilia msaada, lakini hakuna haki.+
9 Amenivua utukufu wangu
Na kunivua taji kichwani.
10 Hunibomoa kila upande na kuniangamiza;
Anang’oa tumaini langu kama mti.
12 Majeshi yake hukusanyika na kunizingira,
Nayo hupiga kambi kuzunguka hema langu.
16 Ninamwita mtumishi wangu, lakini hajibu;
Namsihi kwa kinywa changu anihurumie.
18 Hata watoto wachanga wananidharau;
Ninaposimama, wanaanza kunifanyia mzaha.
20 Mifupa yangu inashikamana na ngozi yangu na mwili wangu,+
Nami ninaponyoka kwa ngozi ya meno yangu.
21 Nionyesheni rehema, rafiki zangu, nionyesheni rehema,
Kwa maana mkono wa Mungu mwenyewe umenigusa.+
23 Laiti maneno yangu yangeandikwa,
Laiti yangeandikwa katika kitabu!
24 Laiti yangechongwa milele kwenye mwamba,
Kwa kalamu ya chuma na risasi!
26 Baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi,
Nikiwa bado hai, nitamwona Mungu,
27 Ambaye mimi mwenyewe nitamwona,
Ambaye macho yangu mwenyewe yatamwona, si ya mwingine.+
Lakini ndani kabisa ninahisi nimelemewa!*
28 Kwa maana mnauliza, ‘Tunamtesa kwa njia gani?’+
Kwa maana mimi ndiye mzizi wa tatizo hili.
29 Ninyi wenyewe ogopeni upanga,+
Kwa kuwa upanga huwaadhibu wakosaji;
Mnapaswa kujua kwamba kuna mwamuzi.”+
2 “Ndiyo sababu mawazo yangu mwenyewe yanayonifadhaisha yananichochea kujibu
Kwa sababu ya mahangaiko niliyo nayo.
4 Bila shaka unajua jambo hili tangu zamani,
Kwa maana imekuwa hivyo tangu mtu* alipoumbwa duniani,+
5 Kwamba kelele za shangwe za mwovu ni za muda mfupi
Na kushangilia kwa mtu anayemkataa Mungu* ni kwa kipindi kifupi.+
6 Ingawa ukuu wake hupanda mpaka mbinguni
Na kichwa chake hufika mawinguni,
7 Ataangamia milele kama kinyesi chake mwenyewe;
Wale waliozoea kumwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
8 Atatoweka kama ndoto, nao hawatampata;
Atafukuzwa mbali kama maono ya usiku.
10 Watoto wake mwenyewe watawaomba maskini msaada,
Na mikono yake mwenyewe itarudisha mali aliyochukua.+
11 Mifupa yake ilijaa nguvu za ujana,
Lakini nguvu hizo zitalala pamoja naye mavumbini.
12 Ikiwa uovu ni mtamu kinywani mwake,
Ikiwa anauficha chini ya ulimi wake,
13 Ikiwa anauonja na hautemi
Lakini anauacha ukae kinywani mwake,
14 Chakula chake kitageuka na kuwa kichungu ndani yake;
Kitakuwa kama sumu* ya swila ndani yake.
15 Amemeza mali, lakini ataitapika;
Mungu ataitoa yote tumboni mwake.
17 Hataona kamwe vijito vya maji,
Mafuriko ya asali na siagi.
18 Atarudisha mali zake bila kuzitumia;*
Hatafurahia utajiri wa biashara yake.+
19 Kwa maana amewaponda na kuwaacha maskini;
Amenyakua nyumba ambayo hakujenga.
20 Lakini hatakuwa na amani ndani yake;
Mali zake hazitamsaidia kuokoka.
21 Hakuna chochote kinachobaki cha kunyafua;
Ndiyo sababu ufanisi wake hautadumu.
22 Mali zake zitakapofikia kilele, mahangaiko yatamkumba;
Misiba itamshambulia kwa nguvu zote.
23 Atakapokuwa akijaza tumbo lake,
Mungu atammwagia hasira yake kali,
Itamnyeshea mpaka ndani ya matumbo yake.
24 Atakapokimbia silaha za chuma,
Mishale kutoka katika upinde wa shaba itamchoma.
25 Huchomoa mshale mgongoni mwake,
Silaha inayong’aa kutoka kwenye nyongo yake,
Naye hushikwa na hofu.+
26 Giza zito linasubiri hazina zake;
Moto ambao haukuwashwa na yeyote utamla;
Msiba unamsubiri yeyote atakayeokoka katika hema lake.
27 Mbingu zitafunua kosa lake;
Dunia itainuka dhidi yake.
28 Mafuriko yataifagilia mbali nyumba yake;
Yatakuwa mafuriko yenye nguvu katika siku ya hasira ya Mungu.
29 Hilo ndilo fungu ambalo Mungu atampa mwovu,
Urithi ambao Mungu amemtangazia.”
21 Ayubu akajibu:
2 “Sikilizeni kwa makini ninayosema;
Na hii iwe faraja mnayonipa.
4 Je, ninamlalamikia mwanadamu?
Ikiwa ndivyo, je, nisingekosa* subira?
5 Niangalieni na kunikodolea macho kwa mshangao;
Funikeni kinywa chenu kwa mkono wenu.
6 Ninapofikiria jambo hilo, nashikwa na wasiwasi,
Na mwili wangu wote unatetemeka.
8 Huwaona watoto wao sikuzote,
Nao huendelea kuishi na kuwaona wazao wao.
10 Ng’ombe dume wao hawashindwi kuzalisha;
Ng’ombe wao huzaa na mimba haziharibiki.
11 Wavulana wao hukimbia nje kama kondoo,
Na watoto wao hurukaruka huku na huku.
14 Lakini wanamwambia Mungu wa kweli, ‘Tuache!
Hatutamani kuzijua njia zako.+
15 Mweza-Yote ni nani ili tumtumikie?+
Tutapata faida gani tukimfahamu?’+
16 Lakini ninajua kwamba hawaudhibiti ufanisi wao wenyewe.+
Mawazo ya waovu yako mbali nami.*+
17 Ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?+
Ni mara ngapi wanapopatwa na msiba?
Ni mara ngapi Mungu huwaangamiza kwa hasira yake?
18 Je, kuna wakati wowote wanapopeperushwa na upepo kama majani makavu
Na kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo wa dhoruba?
19 Mungu atawawekea watoto wa mtu mwovu adhabu ya mtu huyo.
Lakini Mungu na amlipe ili apate kujua hilo.+
21 Kwa maana, kwa nini ahangaikie kitakachoipata nyumba yake baada ya kifo chake
22 Je, kuna yeyote anayeweza kumfundisha Mungu ujuzi,*+
Wakati Yeye ndiye anayewahukumu hata walio juu zaidi?+
23 Kuna mtu anayekufa akiwa na nguvu zake zote+
Akiwa amestarehe kabisa na bila mahangaiko,+
24 Wakati mapaja yake yamenenepa kwa mafuta
Na mifupa yake ikiwa na nguvu.*
28 Kwa maana mnasema, ‘Iko wapi nyumba ya yule mtu maarufu,
Na liko wapi hema alimoishi yule mtu mwovu?’+
29 Je, hamjawauliza wasafiri?
Je, hamchunguzi kwa makini mambo waliyoona,*
30 Kwamba mtu mwovu huokolewa katika siku ya msiba
Na kuokolewa katika siku ya ghadhabu?
31 Ni nani atakayemuuliza kuhusu njia yake,
Na ni nani atakayemlipa kwa sababu ya mambo aliyotenda?
32 Anapopelekwa kaburini,
Kaburi lake litalindwa.
34 Basi kwa nini mnipe faraja isiyo na maana?+
Majibu yenu hayana lolote isipokuwa udanganyifu!”
2 “Je, mwanadamu anaweza kuwa na faida kwa Mungu?
Je, mtu yeyote mwenye ufahamu anaweza kuwa na faida kwake?+
3 Je, Mweza-Yote anajali* kwamba wewe ni mwadilifu,
Au je, anapata faida yoyote kwa sababu unafuata njia ya utimilifu?+
4 Je, atakuadhibu
Na kukushtaki kwa sababu unamheshimu?
6 Kwa maana unachukua dhamana kutoka kwa ndugu zako bila sababu,
9 Lakini uliwafukuza wajane mikono mitupu,
Nawe uliiponda mikono ya mayatima.
10 Ndiyo sababu umezungukwa na mitego,*+
Na vitisho vya ghafla vinakuogopesha;
11 Ndiyo sababu kuna giza sana hivi kwamba huwezi kuona,
Na mafuriko ya maji yamekufunika.
12 Je, Mungu hayuko katika vilele vya mbinguni?
Na tazama jinsi nyota zote zilivyo juu sana.
13 Lakini umesema: ‘Kwa kweli Mungu anajua nini?
Je, anaweza kuhukumu katika giza zito?
14 Mawingu humfunika hivi kwamba haoni
Anapotembea huku na kule kwenye duara ya mbingu.’
15 Je, utafuata kijia cha kale
Ambacho watu waovu wamefuata,
17 Walikuwa wakimwambia Mungu wa kweli: ‘Achana nasi!’
Na ‘Mweza-Yote anaweza kutufanya nini?’
18 Lakini, Yeye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vizuri.
(Sina mawazo maovu kama hayo.)
19 Waadilifu wataona hilo na kushangilia,
Na wasio na hatia watawadhihaki na kusema:
20 ‘Wapinzani wetu wameangamizwa,
Na moto utateketeza mabaki yao.’
21 Mjue Yeye, nawe utakuwa na amani;
Kisha mambo mema yatakujia.
23 Ukimrudia Mweza-Yote, utarudishiwa hali njema;+
Ukiondoa uovu katika hema lako,
24 Ukitupa dhahabu yako* mavumbini
Na dhahabu ya Ofiri+ kwenye miamba ya mabondeni,*
25 Ndipo Mweza-Yote atakapokuwa dhahabu yako,*
Naye atakuwa fedha yako iliyo bora kabisa.
26 Kwa maana ndipo utakapopendezwa na Mweza-Yote,
Nawe utauinua uso wako kumwelekea Mungu.
27 Utamsihi, naye atakusikiliza;
Nawe utatimiza nadhiri zako.
28 Jambo lolote utakaloamua kufanya litafanikiwa,
Na nuru itaangaza kwenye kijia chako.
30 Atawaokoa watu wasio na hatia;
Kwa hiyo ikiwa mikono yako ni safi, hakika utaokolewa.”
23 Ayubu akajibu:
3 Laiti ningejua mahali ninapoweza kumpata Mungu!+
Ningeenda mahali anapoishi.+
4 Ningepeleka kesi yangu mbele zake
Na kujaza hoja za kujitetea kinywani mwangu;
5 Ningefahamu jinsi ambavyo angenijibu
Na kutilia maanani anayoniambia.
6 Je, angepambana nami kwa nguvu zake nyingi?
Hapana, bila shaka angenisikiliza.+
7 Huko mtu mnyoofu angenyoosha mambo pamoja naye,
Na Mwamuzi wangu angefutilia mbali mashtaka yangu milele.
8 Lakini nikienda mashariki, hayuko huko;
Na nikirudi, simpati.
9 Anapofanya kazi upande wa kushoto, siwezi kumwona;
Kisha anageuka upande wa kulia, lakini bado simwoni.
10 Lakini anajua kijia ninachofuata.+
Baada ya kunijaribu, nitatoka nikiwa kama dhahabu safi.+
12 Sijaacha amri ya midomo yake.
Nimeyathamini maneno yake+ kama hazina hata kuliko nilivyoamriwa.*
13 Anapokusudia, ni nani anayeweza kumpinga?+
Anapotaka kufanya jambo, yeye hulifanya.+
14 Kwa maana atatenda kwa ukamili aliyokusudia* kwa ajili yangu,
Naye ana mambo mengi kama hayo akibani.
15 Ndiyo sababu nina wasiwasi kwa sababu yake;
Ninapomfikiria, hofu yangu inaongezeka.
16 Mungu amenifanya nihofu,
Na Mweza-Yote amenitia woga.
17 Lakini bado sijanyamazishwa na giza
Wala utusitusi uliofunika uso wangu.
24 “Kwa nini Mweza-Yote haweki wakati wa hukumu?+
Kwa nini wale wanaomjua hawaioni siku yake?*
4 Huwasukuma maskini waondoke barabarani;
Watu wasio na uwezo duniani hulazimika kujificha kwa sababu yao.+
8 Wanaloweshwa na mvua za milimani;
Wanashikilia miamba kwa nguvu kwa sababu hawana mahali pa kujificha.
9 Mtoto asiye na baba hunyakuliwa kutoka kwenye matiti ya mama yake;+
Na mavazi ya maskini huchukuliwa kuwa dhamana ya mkopo,+
10 Na kuwalazimisha kutembea uchi, bila nguo,
Wakiwa na njaa, huku wakibeba masuke ya nafaka.
11 Hufanya kazi ngumu kwenye matuta yaliyo milimani katika joto la mchana;*
Hukanyaga mashinikizo ya divai, lakini wanaona kiu.+
12 Wanaokufa wanaendelea kulia kwa uchungu jijini;
Waliojeruhiwa vibaya sana hulilia msaada,+
Lakini Mungu haoni jambo hilo kuwa baya.*
14 Muuaji huamka wakati wa mapambazuko;
Huwaua wasio na uwezo na maskini,+
Naye huiba wakati wa usiku.
Naye huufunika uso wake.
16 Wakati wa giza wanavunja nyumba;
Wakati wa mchana wanajifungia ndani.
Wanaepuka nuru.+
17 Kwa maana kwao, asubuhi ni kama giza zito;
Wamezoea vitisho vya giza zito.
18 Lakini wanabebwa upesi na maji.*
Fungu lao la ardhi litalaaniwa.+
Hawatarudi kwenye mashamba yao ya mizabibu.
19 Kama theluji iliyoyeyuka inavyokaushwa na ukame na joto,
20 Mama yake atamsahau;* naye ataliwa na mabuu.
Hatakumbukwa tena.+
Na uovu utakatwa kama mti.
21 Humwinda mwanamke tasa,
Na kumtesa mjane.
22 Mungu atatumia nguvu zake kuwaangamiza wenye nguvu;
Hata wakiinuka, hawana uhakika wa kuishi.
24 Wanakwezwa kwa muda mfupi, kisha wanatoweka.+
Wanashushwa chini+ na kukusanywa kama watu wengine wote;
Wanakatwa kama masuke ya nafaka.
25 Sasa ni nani anayeweza kuthibitisha kwamba mimi ni mwongo
Au kupinga neno langu?”
3 Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
5 Hata mwezi si mwangavu
Na nyota si safi machoni pake,
6 Sembuse mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni buu,
Na binadamu ambaye ni mnyoo!”
26 Ayubu akajibu:
2 “Jinsi mlivyomsaidia mtu asiye na uwezo!
Jinsi mlivyouokoa mkono usio na nguvu!+
3 Kwa kweli mmempa ushauri bora mtu asiye na hekima!+
Jinsi mlivyofunua waziwazi* hekima yenu inayotumika!*
5 Wale waliokufa ambao hawana uwezo hutetemeka;
Wako chini hata kuliko maji na viumbe wanaokaa ndani yake.
7 Hulitandaza anga la kaskazini* mahali pasipo na kitu,*+
Na kuining’iniza dunia mahali pasipo na kitu;
8 Huyafunga maji katika mawingu yake,+
Ili mawingu yasipasuke kwa sababu ya uzito wake;
9 Hufunika kiti chake cha ufalme ili kisionekane,
Na kutandaza wingu lake juu yake.+
11 Nguzo zenyewe za mbingu hutikisika;
Nazo hushtushwa na kemeo lake.
12 Huitibua bahari kwa nguvu zake,+
Na kwa uelewaji wake humvunja vipandevipande mnyama mkubwa sana wa baharini.*+
Basi ni nani anayeweza kuelewa mngurumo wake wenye nguvu?”+
27 Ayubu akaendelea kuzungumza:*
2 “Kwa hakika kama Mungu anavyoishi, ambaye ameninyima haki,+
Kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye amenitia uchungu,+
3 Maadamu pumzi imo ndani yangu
Na roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+
4 Midomo yangu haitasema uovu;
Wala ulimi wangu hautasema udanganyifu!
5 Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa waadilifu!
Mpaka nitakapokufa, sitaukana* utimilifu wangu!+
7 Adui yangu na awe kama watu waovu,
Wale wanaonishambulia na wawe kama watu wasio waadilifu.
10 Au, je, atapendezwa na Mweza-Yote?
Je, atamlilia Mungu nyakati zote?
12 Tazama! Ikiwa ninyi nyote mmeona maono,
Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?
13 Hilo ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu,+
Urithi ambao wakandamizaji hupokea kutoka kwa Mweza-Yote.
15 Pigo litawazika wazao wake watakaobaki,
Na wajane wao hawatawalilia.
16 Hata akikusanya fedha kama mavumbi
Na kuhifadhi mavazi bora kama udongo wa mfinyanzi,
17 Hata akiyakusanya,
Mwadilifu ndiye atakayeyavaa,+
Na wanyoofu watagawana fedha zake.
19 Ataenda kitandani akiwa tajiri lakini hatakusanya chochote;
Atakapofungua macho yake, hakutakuwa na chochote.
3 Mwanadamu hulishinda giza;
Huchunguza kwa kina katika utusitusi na giza,
Akitafuta mawe yenye madini.
4 Huzamisha bomba mbali na makao ya watu,
Mahali paliposahauliwa, mbali na mahali ambapo watu wanatembea;
Wanaume fulani hushuka wakining’inia kwa kamba.
6 Katika mawe hayo kuna yakuti,
Na vumbi lake lina dhahabu.
7 Hakuna ndege awindaye anayejua njia ya kufika huko;
Jicho la mwewe mweusi halijaiona.
8 Hakuna mnyama yeyote wa mwituni mwenye fahari aliyeikanyaga;
Mwanasimba hajazunguka huko.
9 Mwanadamu hugonga mwamba mgumu kwa mkono wake;
Huipindua milima kwenye misingi yake.
11 Huziba chemchemi za mito
Na kufichua vitu vilivyofichwa.
14 Vilindi vya maji vinasema, ‘Haimo ndani yangu!’
Nayo bahari inasema, ‘Haiko pamoja nami!’+
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri+
Wala kwa madini ya shohamu na yakuti yasiyopatikana kwa urahisi.
17 Dhahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo;
18 Marijani na fuwele hazistahili kutajwa,+
Kwa maana mfuko uliojaa hekima una thamani kuliko mfuko uliojaa lulu.
22 Maangamizi na kifo husema,
‘Masikio yetu yamesikia tu habari zake.’
23 Mungu anaelewa njia ya kuipata;
Yeye peke yake ndiye anayejua inakokaa,+
24 Kwa maana yeye hutazama mpaka kwenye miisho ya dunia,
Naye huona kila kitu chini ya mbingu.+
Na kuyapima maji,+
Na njia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+
27 Kisha akaiona hekima na kuifafanua;
Aliiimarisha na kuijaribu.
28 Naye akamwambia mwanadamu:
29 Ayubu akaendelea kuzungumza:*
2 “Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa miezi ya zamani,
Siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Alipoifanya taa yake iniangazie kichwani,
Nilipotembea gizani kwa nuru yake,+
4 Nilipokuwa katika kilele cha mafanikio,
Urafiki pamoja na Mungu ulipohisiwa katika hema langu,+
5 Mweza-Yote alipokuwa bado pamoja nami,
Watoto* wangu wote waliponizunguka,
6 Nyayo zangu zilipoloweshwa katika siagi,
Na miamba iliponimwagia vijito vya mafuta.+
7 Nilipokuwa nikienda kwenye lango la jiji+
Na kuketi mahali pangu kwenye uwanja wa jiji,+
8 Vijana waliponiona walinipisha,*
Na hata wazee waliinuka na kuendelea kusimama.+
9 Wakuu waliacha kuzungumza;
Walifunika kinywa chao kwa mkono wao.
10 Sauti za watu maarufu zilinyamazishwa;
Ulimi wao ulishikamana na kaakaa lao.
11 Yeyote aliyenisikia alinisifu,
Na wale walioniona walinitetea.
12 Kwa maana nilimwokoa maskini aliyelilia msaada,+
Pamoja na yatima na yeyote ambaye hakuwa na msaidizi.+
15 Nilikuwa macho kwa vipofu
Na miguu kwa walemavu.
18 Nilikuwa nikisema, ‘Nitafia nyumbani kwangu,*+
Na siku zangu zitakuwa nyingi kama chembe za mchanga.
19 Mizizi yangu itaenea ndani ya maji,
Na umande utakaa usiku kucha kwenye matawi yangu.
20 Utukufu wangu hufanywa kuwa mpya daima,
Na upinde ulio mkononi mwangu utaendelea kupiga mishale.’
23 Waliningojea kama wanavyongojea mvua;
Walifumbua vinywa vyao wazi kana kwamba wanangojea mvua ya masika.+
25 Niliwapa mwelekezo nikiwa kiongozi wao,
Nami niliishi kama mfalme anayezungukwa na majeshi yake,+
Kama mtu anayewafariji waombolezaji.+
—Wanaume wenye umri mdogo kuliko mimi,
Ambao baba zao ningekataa
Kuwaweka pamoja na mbwa waliolinda kondoo wangu.
2 Nguvu za mikono yao zilikuwa na faida gani kwangu?
Nguvu zao zimekwisha.
3 Wamedhoofika kwa sababu ya umaskini na njaa;
Wanaguguna ardhi iliyokauka
Ambayo ilikuwa tayari imeharibiwa na kuachwa ukiwa.
4 Wanakusanya mmea wenye chumvi kutoka vichakani;
Chakula chao ni mizizi ya miretemu.
7 Wanalia kwa sauti kutoka vichakani
Na kujikunyata pamoja katikati ya upupu.
12 Wanainuka upande wangu wa kulia kama umati;
Wananikimbiza
Na kuweka vizuizi vya maangamizi kwenye njia yangu.
14 Wanakuja kana kwamba wanapita kwenye ufa mpana ukutani;
Wanamiminika ndani katikati ya magofu.
15 Hofu inanilemea;
Heshima yangu inapeperushwa mbali kama upepo,
Na wokovu wangu unatoweka kama wingu.
19 Mungu ameniangusha chini kwenye matope;
Nimebaki mavumbi na majivu tu.
23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha katika kifo,
Katika nyumba ambamo watu wote walio hai watakutana.
25 Je, sijawalilia wale ambao wamekabili nyakati ngumu?*
Je, sijawahuzunikia maskini?+
26 Ingawa nilitumaini mema, mabaya yalikuja;
Nilitarajia nuru, lakini giza likaja.
27 Msukosuko uliokuwa ndani yangu haukukoma;
Siku za mateso zilinikabili.
28 Ninatembeatembea kwa huzuni;+ hakuna mwangaza wa jua.
Ninasimama na kulilia msaada katika kusanyiko.
31 Kinubi changu kinatumika kwa ajili ya maombolezo tu,
Na zumari* yangu kwa ajili ya sauti ya kilio.
31 “Nimefanya agano na macho yangu.+
Basi ninawezaje kumtazama bikira kwa njia isiyofaa?+
2 Basi, nitapata fungu gani kutoka kwa Mungu aliye juu,
Urithi gani kutoka kwa Mweza-Yote aliye juu?
5 Je, nimewahi kutembea katika njia isiyo ya kweli?*
Je, mguu wangu umekimbilia udanganyifu?+
7 Hatua zangu zikikengeuka kutoka kwenye njia+
Au ikiwa moyo wangu umefuata macho yangu+
Au ikiwa mikono yangu imechafuliwa,
8 Basi acha nipande mbegu na mtu mwingine ale,+
Na acha mimea ninayopanda ing’olewe.*
9 Ikiwa moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke+
Nami nimenyemelea+ katika mlango wa jirani yangu,
10 Basi acha mke wangu amsagie nafaka mwanamume mwingine,
Nitamjibu nini akinifanya niwajibike?+
15 Je, Yule aliyeniumba tumboni mwa mama yangu hakuwaumba wao pia?+
Je, si Ndiye aliyetuumba sisi kabla hatujazaliwa?*+
17 Ikiwa nilikula chakula changu peke yangu
Bila kuwagawia mayatima;+
18 (Kwa maana tangu nilipokuwa kijana, nimemlea yatima kana kwamba mimi ni baba yake,
Nami nimekuwa kiongozi wa mjane tangu utotoni.*)
19 Ikiwa nilimwona yeyote akiangamia kwa kukosa mavazi
Au maskini asiye na chochote cha kujifunika;+
Alipokuwa akijipasha joto kwa manyoya ya kondoo wangu;
22 Basi acha mkono* wangu ung’oke kutoka begani mwangu,
Na acha mkono wangu uvunjwe kwenye kiwiko* chake.
23 Kwa maana niliogopa sana msiba kutoka kwa Mungu,
Nami sikuweza kustahimili adhama yake.
25 Ikiwa shangwe yangu ilikuwa utajiri wangu mwingi+
Kwa sababu ya mali nyingi nilizokusanya;+
26 Ikiwa niliona jua liking’aa*
Au mwezi ukizunguka kwa fahari yake;+
27 Na moyo wangu ukashawishiwa kwa siri,
Na kinywa changu kikabusu mkono wangu nikiviabudu;+
28 Basi hilo ni kosa linalostahili adhabu kutoka kwa waamuzi,
Kwa maana nitakuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu.
31 Je, watu wa hema langu hawajauliza,
‘Ni nani anayeweza kumpata mtu ambaye hajashibishwa na chakula chake?’*+
33 Je, nimewahi kujaribu kufunika dhambi zangu, kama watu wengine,+
Kwa kuficha uovu wangu katika mfuko wa vazi langu?
34 Je, nimewahi kuogopa umati utakavyotenda,
Au kutishwa na dharau za familia nyingine,
Na hivyo kukaa kimya na kuogopa kutoka nje?
35 Laiti mtu fulani angenisikiliza!+
Ningeweka sahihi ya jina langu kwenye mambo niliyosema!*
Mweza-Yote na anijibu!+
Laiti mshtaki wangu angeandika mashtaka yangu kwenye hati!
36 Ningeibebea begani mwangu,
Nami ningeifunga kama taji kuzunguka kichwa changu.
37 Ningempa habari kuhusu kila hatua niliyopiga;
Ningemfikia kwa ujasiri, kama kiongozi.
38 Ikiwa ardhi yangu mwenyewe ingetoa kilio dhidi yangu
Na mitaro yake ingelia pamoja;
39 Ikiwa nimekula mazao yake bila kulipa,+
Au ikiwa nimewakatisha tamaa wamiliki wake;+
40 Basi miiba ichipuke kwa ajili yangu badala ya ngano
Na magugu yenye harufu mbaya badala ya shayiri.”
Maneno ya Ayubu yanaishia hapa.
32 Basi wanaume hao watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alisadiki kwamba yeye ni mwadilifu.*+ 2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi,+ wa ukoo wa Ramu, akakasirika sana. Hasira yake iliwaka dhidi ya Ayubu kwa sababu alijaribu kujithibitisha mwenyewe kuwa mwadilifu badala ya Mungu.+ 3 Pia, aliwakasirikia vikali marafiki watatu wa Ayubu kwa sababu walishindwa kujibu lakini walikuwa wamemtangaza Mungu kuwa mwovu.+ 4 Elihu alikuwa amesubiri kumjibu Ayubu, kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kuliko yeye.+ 5 Elihu alipoona kwamba wanaume hao watatu hawakuwa na jambo la kusema, aliwaka hasira. 6 Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli, kutoka Buzi, akaanza kuzungumza, akasema:
Kwa hiyo kwa heshima nilijizuia,+
Nami sikuthubutu kuwaambia ninayojua.
10 Kwa hiyo ninasema, ‘Nisikilizeni,
Nami pia nitawaambia ninayojua.’
11 Tazameni! Nimesubiri maneno yenu;
Niliendelea kusikiliza hoja zenu+
Mlipokuwa mkitafuta mambo ya kusema.+
12 Niliwasikiliza kwa makini,
Lakini hakuna yeyote miongoni mwenu aliyeweza kuthibitisha kwamba Ayubu amekosea*
Wala kujibu hoja zake.
13 Kwa hiyo msiseme, ‘Tumepata hekima;
Mungu ndiye anayempinga, si mwanadamu.’
14 Ayubu hakuelekeza maneno yake kwangu,
Kwa hiyo sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 Wamefadhaika, hawana mambo zaidi ya kusema;
Wameishiwa na maneno.
16 Nimesubiri, lakini hawaendelei kuzungumza;
Wamesimama pale tu, hawana majibu zaidi.
17 Basi, mimi pia nitajibu;
Mimi pia nitasema ninayojua,
18 Kwa maana nina mengi ya kusema;
Roho iliyo ndani yangu inanishurutisha.
19 Matumbo yangu ni kama divai isiyo na mahali pa kutokea,
Kama viriba vipya vya divai vinavyokaribia kupasuka.+
20 Acha nizungumze ili nipate kitulizo!
Nitafungua midomo yangu na kujibu.
Wala kumsifusifu* mwanadamu yeyote,
22 Kwa maana sijui kusifusifu;
Nikifanya hivyo, Muumba wangu ataniangamiza.
33 “Lakini sasa, Ayubu, tafadhali sikiliza maneno yangu;
Sikiliza kila jambo nitakalosema.
3 Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+
Na midomo yangu inasema kwa unyoofu mambo ninayojua.
5 Nijibu ikiwa unaweza;
Niambie hoja zako; jitayarishe kujitetea.
7 Kwa hiyo usiniogope,
Na uzito wa maneno yangu usikulemee.
8 Lakini nilisikia ukisema,
Naam, niliendelea kusikia maneno haya,
9 ‘Mimi ni safi, sina dhambi;+
Mimi ni safi, sina kosa.+
12 Lakini umekosea kusema hivyo, kwa hiyo nitakujibu:
Mungu ni mkuu sana kuliko mwanadamu anayeweza kufa.+
Je, ni kwa sababu hakujibu hoja zako zote?+
14 Kwa maana Mungu huzungumza mara moja na mara ya pili,
Lakini hakuna yeyote anayesikiliza,
15 Huzungumza katika ndoto, maono ya usiku,+
Watu wanaposhikwa na usingizi mzito
Wanapolala vitandani mwao.
16 Kisha hufungua masikio yao+
Na kuyakazia* maagizo yake kwao,
17 Ili kumwepusha mtu asitende dhambi+
Na kumlinda mwanadamu asiwe na kiburi.+
19 Mtu hukaripiwa pia na maumivu kitandani mwake
Na mateso yasiyo na kikomo mifupani mwake,
20 Hivi kwamba nafsi yake inachukia* mkate,
Naye anakataa hata chakula bora.+
21 Nyama ya mwili wake huisha hivi kwamba haionekani,
Na mifupa yake iliyokuwa imefichika sasa imechomoza.*
23 Ikiwa kuna mjumbe* kwa ajili yake,
Mtetezi mmoja kati ya elfu moja,
Ili amwambie mwanadamu mambo manyoofu,
24 Basi Mungu humhurumia na kusema,
Nimepata fidia!+
25 Mwili wake na uwe na afya zaidi kuliko wakati wa ujana;+
Na azirudie siku alizokuwa na nguvu za ujana.’+
26 Atamsihi Mungu,+ naye atamkubali,
Naye atauona uso wa Mungu kwa kelele za shangwe,
Na Mungu atamrudishia uadilifu Wake mwanadamu anayeweza kufa.
27 Mtu huyo atawatangazia* wanadamu,
‘Nimetenda dhambi+ na kupotosha yaliyo sawa,
Lakini sikupokea niliyostahili.*
29 Kwa kweli, Mungu hufanya mambo haya yote
Mara mbili, mara tatu, kwa ajili ya mwanadamu,
30 Ili kumrudisha kutoka shimoni,*
Ili aweze kuangaziwa nuru ya uzima.+
31 Sikiliza, Ayubu! Nisikilize!
Nyamaza, nami nitaendelea kuzungumza.
32 Ikiwa una jambo la kusema, niambie.
Sema, kwa maana nataka kuthibitisha kwamba uko sahihi.
33 Ikiwa huna la kusema, unapaswa kunisikiliza;
Nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
34 Kwa hiyo, Elihu akaendelea kusema:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi mlio na hekima;
Nisikilizeni, ninyi mnaojua mambo mengi sana.
4 Acheni tuchanganue wenyewe yaliyo sawa;
Acheni tuamue miongoni mwetu yaliyo mema.
6 Je, ninaweza kusema uwongo kuhusu hukumu ninayostahili?
Kidonda changu hakiponi, ingawa sina kosa.’+
7 Ni nani aliye kama Ayubu,
Anayekunywa dharau kama maji?
10 Kwa hiyo nisikilizeni, ninyi watu wenye uelewaji:*
16 Basi ikiwa mna uelewaji, sikilizeni mambo haya;
Sikilizeni kwa makini ninayosema.
17 Je, mtu anayechukia haki anapaswa kuongoza,
Au je, mtamhukumu mwenye nguvu ambaye ni mwadilifu?
19 Kuna Yule asiyewapendelea wakuu
Na ambaye hawapendelei matajiri na kuwapuuza maskini,*+
Kwa maana wote ni kazi ya mikono yake.+
20 Wanaweza kufa ghafla,+ katikati ya usiku;+
Wanatikisika kwa nguvu na kufa;
Hata wenye nguvu huondolewa, lakini si kwa mikono ya wanadamu.+
23 Kwa maana Mungu hajaweka wakati hususa wa mwanadamu yeyote
Kufika mbele zake ili ahukumiwe.
26 Huwapiga kwa sababu ya uovu wao,
Mahali ambapo watu wote wanaweza kuona,+
27 Kwa sababu wameacha kumfuata+
Nao hawaheshimu yoyote kati ya njia zake;+
28 Wanasababisha maskini wamlilie,
Hivi kwamba anasikia kilio cha wasio na uwezo.+
29 Mungu akikaa kimya, ni nani anayeweza kumshutumu?
Akiuficha uso wake, ni nani anayeweza kumwona?
Iwe ni kwa taifa au mtu mmoja, matokeo ni yaleyale,
30 Ili mtu anayemkataa Mungu* asitawale+
Au kuwawekea wengine mitego.
31 Je, kuna yeyote anayeweza kumwambia Mungu,
‘Nimeadhibiwa, ingawa sijafanya kosa lolote;+
32 Nifundishe jambo ambalo nimeshindwa kuona;
Ikiwa nimetenda kosa lolote, sitalirudia tena’?
33 Je, akuthawabishe kwa masharti yako wakati unakataa hukumu yake?
Amua mwenyewe, si mimi.
Basi niambie mambo unayojua vema.
34 Watu wenye uelewaji* wataniambia
—Mtu yeyote mwenye hekima anayenisikiliza—
35 ‘Ayubu anazungumza bila ujuzi,+
Na maneno yake hayana ufahamu.’
37 Anaongeza uasi kwenye dhambi yake;+
Anapiga makofi kwa dharau mbele yetu
Na kusema maneno mengi dhidi ya Mungu wa kweli!”+
35 Elihu akaendelea kusema:
3 Kwa maana unasema, ‘Hilo linakuhusuje?*
Je, hali yangu ni bora kuliko kama ningetenda dhambi?’+
6 Ukitenda dhambi, unamuumizaje?+
Dhambi zako zikiongezeka, unamwathirije?+
8 Uovu wako unamwathiri tu mwanadamu kama wewe,
Na uadilifu wako, binadamu.
9 Watu hulia kwa sauti wanapokandamizwa sana;
Wanalia wapate kitulizo kutoka chini ya mamlaka ya* wenye nguvu.+
10 Lakini hakuna anayeuliza, ‘Yuko wapi Mungu, Muumba wangu Mkuu,+
Yule anayesababisha nyimbo ziimbwe usiku?’+
11 Hutufundisha+ kuliko wanyama mwitu wa dunia,+
Naye hutufanya tuwe na hekima kuliko ndege wa angani.
14 Sembuse wewe unapolalamika kwamba humwoni!+
Kesi yako iko mbele zake, kwa hiyo unapaswa kumngojea kwa hamu.+
15 Kwa maana hajakuadhibu kwa hasira;
Wala hajakazia fikira maneno unayosema haraka-haraka bila kufikiri.+
36 Elihu akaendelea kusema:
2 “Uwe na subira zaidi ninapoendelea kueleza,
Kwa maana bado nina maneno ya kusema kwa niaba ya Mungu.
7 Yeye haondoi macho yake kwa waadilifu;+
Huwaketisha kwenye viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanakwezwa milele.
8 Lakini ikiwa wamefungwa kwa pingu
Na kunaswa na kamba za mateso,
9 Huwafunulia mambo waliyotenda,
Uovu wao uliosababishwa na kiburi chao.
13 Wanaomkataa Mungu* moyoni watakuwa na kinyongo.
Hawalilii msaada hata anapowafunga.
15 Lakini Mungu huwaokoa wanaoteseka wakati wanapoteseka;
Hufungua sikio lao wanapokandamizwa.
16 Hukuvuta mbali kutoka kwenye ukingo wa taabu+
Na kukuleta mahali penye nafasi kubwa, pasipo na vizuizi,+
Na meza yako itakuwa na chakula chenye lishe ili kukufariji.+
19 Je, kilio chako cha kuomba msaada
Au mojawapo ya jitihada zako nyingi inaweza kukuepusha na taabu?+
20 Usiutamani usiku,
Watu wanapotoweka katika makao yao.
22 Tazama! Mungu amekwezwa katika nguvu zake;
Ni nani aliye mfundishaji kama yeye?
25 Wanadamu wote wameziona,
Mwanadamu anayeweza kufa huzitazama kutoka mbali.
27 Yeye huvuta juu matone ya maji;+
Yanaganda na kuwa mvua kutokana na ukungu wake;
28 Kisha mawingu huyamwaga chini;+
Yanawanyeshea wanadamu.
37 “Kwa sababu hiyo moyo wangu hupigapiga
Na kuruka kutoka mahali pake.
2 Sikiliza kwa makini mrindimo wa sauti yake
Na mngurumo unaotoka kinywani mwake.
4 Kisha sauti ya mngurumo husikika;
Hunguruma kwa sauti yenye fahari,+
Naye haizuii radi sauti yake inaposikiwa.
5 Mungu hunguruma kwa sauti yake+ kwa njia inayostaajabisha;
Hufanya mambo makuu ambayo hatuwezi kuelewa.+
8 Wanyama wa mwituni huingia katika mapango yao
Na kubaki katika makao yao.
11 Naam, huyalemea mawingu kwa mvuke;
Hutawanya radi yake+ mawinguni;
12 Huzunguka-zunguka anakoyaelekeza;
13 Iwe ni adhabu*+ au kwa ajili ya nchi
Au kwa ajili ya upendo mshikamanifu, yeye husababisha yatendeke.+
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza* mawingu
Na jinsi anavyosababisha radi imweke kutoka katika mawingu yake?
16 Je, unajua jinsi mawingu yanavyoelea?+
Hizi ni kazi zinazostaajabisha za Yule ambaye ni mkamilifu katika ujuzi.+
19 Tuambie tunalopaswa kumwambia;
Hatuwezi kumjibu kwa sababu tuko gizani.
20 Je, anapaswa kuambiwa kwamba ninataka kuzungumza?
Au kuna yeyote ambaye amesema jambo ambalo lazima ajulishwe?+
Ingawa inang’aa angani,
Mpaka upepo unapopita na kuondoa kabisa mawingu.
24 Kwa hiyo watu wanapaswa kumwogopa.+
Kwa sababu yeye hampendi yeyote anayefikiri ana hekima.”+
38 Kisha Yehova akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo:+
4 Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?+
Niambie, ikiwa unafikiri unaelewa.
5 Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,
Au ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Nguzo zake zilizamishwa ndani ya nini,
Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,+
8 Na ni nani aliyeizuia bahari nyuma ya milango+
Ilipotoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,
9 Nilipoivalisha mawingu
Na kuifunika kwa* giza zito,
10 Nilipoiwekea mpaka wangu
Na kuweka makomeo yake na milango yake mahali pake,+
11 Nami nikaiambia, ‘Unaweza kufika hapa, lakini usipite hapa;
Hapa ndipo mawimbi yako ya kifahari yatakapokomea’?+
12 Je, umewahi kuiamuru* asubuhi
Au kuyafanya mapambazuko yajue mahali pake,+
13 Ili yaenee mpaka kwenye miisho ya dunia
Na kuwakung’uta waovu kutoka humo?+
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi utiwapo muhuri,
Na vitu vilivyomo hung’aa kama mapambo ya vazi.
15 Lakini waovu hunyimwa nuru yao,
Na mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
18 Je, umeelewa upana mkubwa sana wa dunia?+
Niambie, ikiwa unajua haya yote.
Na makao ya giza yako wapi,
20 Ili ulipeleke katika eneo lake
Na kuelewa vijia vinavyoelekea nyumbani kwake?
22 Je, umeingia kwenye maghala ya theluji,+
Au umeyaona maghala ya mvua ya mawe,+
23 Ambayo nimeyahifadhi kwa ajili ya wakati wa taabu,
Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+
25 Ni nani amechimba mtaro kwa ajili ya mafuriko
Na kutengeneza kijia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+
26 Na kuifanya mvua inyeshe mahali ambapo watu hawaishi,
Nyikani ambako hakuna wanadamu,+
27 Ili kutosheleza maeneo yaliyoharibiwa yenye ukiwa
Na kufanya majani yachipuke?+
29 Barafu ilitoka kwenye tumbo la uzazi la nani,
Na ni nani aliyeizaa theluji ya mbinguni+
30 Maji yanapofunikwa kana kwamba na jiwe,
Na sehemu ya juu ya vilindi vya maji inapoganda kabisa?+
32 Je, unaweza kuliongoza nje kundi la nyota* katika majira yake
Au kulielekeza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wanawe?
35 Je, unaweza kuutuma umeme wa radi?
Je, utakuja na kukwambia, ‘Niko hapa!’?
37 Ni nani aliye na hekima ya kutosha kuhesabu mawingu,
Au ni nani anayeweza kuinamisha mitungi ya maji ya mbinguni+
38 Mavumbi yanapomiminika na kugandamana
Na mabonge ya udongo yanaposhikamana?
39 Je, unaweza kumwindia simba mawindo
Au kutosheleza hamu ya chakula ya wanasimba+
40 Wanapojikunyata katika maficho yao
Au wanaponyemelea mapangoni mwao?
41 Ni nani anayemtayarishia chakula kunguru+
Makinda wake wanapomlilia Mungu wakiomba msaada
Na kutangatanga kwa sababu hawana chakula?
39 “Je, unajua mbuzi wa milimani huzaa wakati gani?+
Je, umewahi kuwatazama paa wakizaa watoto wao?+
2 Je, wewe huhesabu miezi ambayo wanabeba mimba?
Je, unajua wakati wanapozaa?
3 Wao huchuchumaa wanapozaa watoto wao,
Na uchungu wao wa kuzaa huisha.
4 Watoto wao hupata nguvu na kukua mbugani;
Huenda zao na hawarudi.
6 Nimelifanya jangwa tambarare kuwa makao yake
Na nchi yenye chumvi kuwa makazi yake.
7 Yeye hudharau vurugu za mji;
Hasikii kelele za mtu anayemwongoza.
8 Hutangatanga milimani, akitafuta malisho,
Akitafuta mmea wowote wa kijani.
9 Je, fahali mwitu yuko tayari kukutumikia?+
Je, atalala zizini mwako* usiku?
11 Je, utazitumaini nguvu zake nyingi
Na kumwacha afanye kazi zako ngumu?
13 Mabawa ya mbuni hupigapiga kwa shangwe,
Lakini, je, mabawa na manyoya yake yanaweza kulinganishwa na ya korongo?+
14 Kwa maana yeye huacha mayai yake ardhini,
Na kuyapasha joto mavumbini.
15 Yeye husahau kwamba mguu fulani unaweza kuyavunja
Au kwamba mnyama wa mwituni anaweza kuyakanyaga.
16 Huwatendea wanawe kwa ukatili, kana kwamba si wake;+
Haogopi kwamba huenda kazi yake ngumu ikawa ya bure.
18 Lakini anapoinuka na kupigapiga mabawa yake,
Humcheka farasi na yule aliyempanda.
19 Je, ni wewe unayempa farasi nguvu zake?+
Je, unamvika shingoni manyoya marefu yanayotikisika?
20 Je, unaweza kumfanya aruke kama nzige?
Mkoromo wake wa maringo unatisha.+
22 Huicheka hofu na haogopi chochote.+
Harudi nyuma kwa sababu ya upanga.
23 Podo la mishale hutoa sauti kando yake,
Mkuki na fumo humetameta.
25 Pembe inapolia, husema, ‘Aha!’
Hunusa vita kutoka mbali sana
Na kusikia kelele za makamanda na kelele za vita.+
26 Je, ni kwa uelewaji wako kwamba kipanga huruka,
Akiyatandaza mabawa yake kuelekea kusini?
27 Au, je, ni kwa agizo lako kwamba tai hupaa juu+
Na kujenga kiota chake juu sana,+
28 Na kulala usiku kucha juu ya jabali,
Akiishi kwenye ngome yake juu ya mwamba uliochongoka?*
40 Yehova akaendelea kumjibu Ayubu:
2 “Je, mtu anayetafuta makosa anapaswa kushindana na Mweza-Yote?+
Acha yule anayetaka kumkaripia Mungu ajibu.”+
3 Ayubu akamjibu Yehova:
Nitakujibu nini?
Ninafunika kinywa changu kwa mkono.+
5 Niliongea mara moja, lakini sitajibu tena;
Mara mbili, lakini sitaongea tena.”
6 Kisha Yehova akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo:+
8 Je, utatilia shaka* haki yangu?
Je, utanishutumu ili uwe mwadilifu?+
9 Je, una mkono wenye nguvu kama mkono wa Mungu wa kweli,+
Au je, sauti yako inaweza kunguruma kama yake?+
10 Tafadhali, jipambe kwa utukufu na ukuu;
Jivike heshima na fahari.
11 Mwaga ghadhabu ya hasira yako;
Mtazame kila mwenye kiburi, umshushe chini.
12 Mtazame kila mwenye kiburi, umnyenyekeze,
Na uwakanyage waovu mahali wanaposimama.
13 Wafiche wote mavumbini;
Wafunge* mahali palipofichika,
14 Ndipo hata mimi nitakapokiri mbele yako*
Kwamba mkono wako wa kulia unaweza kukuokoa.
15 Tazama, huyu ni Behemothi* niliyemuumba kama nilivyokuumba.
Yeye hula majani kama ng’ombe dume.
16 Tazama nguvu zilizo kiunoni mwake
Na nguvu zilizo katika misuli ya tumbo lake!
17 Huukaza mkia wake kama mwerezi;
Kano za mapaja yake zimefumwa pamoja.
18 Mifupa yake ni mabomba ya shaba;
Miguu yake ni kama fito za chuma kilichofuliwa.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu;
Ni Muumba wake tu anayeweza kumkaribia kwa upanga wake.
20 Kwa maana milima huzalisha chakula kwa ajili yake,
Ambako wanyama wote wa mwituni hucheza.
21 Hulala chini ya miti ya miyungiyungi,
Kwenye kivuli cha matete mahali penye umajimaji.
23 Mto unaposukasuka, yeye hashtuki.
Haogopi hata maji ya Yordani+ yakifurika kinywani mwake.
2 Je, unaweza kupitisha kamba* kwenye mianzi ya pua yake
Au kutoboa mataya yake kwa kulabu?*
3 Je, atakusihi sana umhurumie,
Au je, atazungumza nawe kwa upole?
4 Je, atafanya agano pamoja nawe,
Ili umfanye awe mtumwa wako milele?
5 Je, utamchezea kama ndege
Au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako?
6 Je, wafanyabiashara watamtumia kubadilishana bidhaa?
Je, watamgawanya miongoni mwao?
7 Je, utaijaza ngozi yake mikuki+
Au kichwa chake mikuki ya kuvulia samaki?
8 Mguse kwa mkono wako;
Utakumbuka vita hivyo na kamwe hutarudia kufanya hivyo!
9 Ni kazi bure kujaribu kumtiisha.
Ukimwona tu utashtuka.*
10 Hakuna anayethubutu kumchokoza.
Basi ni nani anayeweza kukabiliana nami?+
11 Ni nani aliyenipa kitu chochote kwanza ili nimlipe?+
Chochote kilicho chini ya mbingu ni changu.+
12 Sitakaa kimya kuhusu miguu yake,
Kuhusu nguvu zake na mwili wake wenye umbo zuri.
13 Ni nani aliyemvua vazi lake la nje?
Ni nani atakayeingia katikati ya mataya yake yaliyo wazi?
14 Ni nani anayeweza kuifungua kwa nguvu milango ya kinywa chake?*
Meno yake kuzunguka kinywa chote yanatisha.
16 Kila gamba limeshikamana kabisa na lingine
Hivi kwamba hewa haiwezi kupenya katikati ya magamba hayo.
17 Yamefungamana pamoja;
Yameshikamana na hayawezi kutenganishwa.
18 Mkoromo wake hufanya nuru imweke,
Na macho yake ni kama miale ya mapambazuko.
19 Mimweko ya radi hutoka kinywani mwake;
Cheche za moto huruka nje.
20 Moshi hufuka kutoka katika mianzi ya pua yake,
Kama tanuru linalowaka moto wa matete.
21 Pumzi yake huwasha makaa ya mawe,
Na mwali wa moto huruka kutoka kinywani mwake.
22 Shingo yake ina nguvu nyingi,
Wanaokutana naye hukimbia kwa hofu.
23 Mikunjo ya ngozi yake imeunganishwa kabisa pamoja;
Ni imara, kana kwamba imetengenezwa kwa chuma, nayo haiwezi kutikisika.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe,
Naam, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Anapoinuka, hata mashujaa huogopa;
Mshindo wake huwababaisha.
27 Yeye huona chuma kama nyasi,
Shaba kama ubao uliooza.
28 Mshale haumfanyi akimbie;
Mawe ya kombeo huwa kama nyasi kavu kwenye mwili wake.
29 Yeye huona rungu kuwa kama nyasi kavu,
Naye huucheka mvumo wa mkuki.
31 Hufanya vilindi vichemke kama chungu;
Huikoroga bahari kama chungu cha manukato.
32 Anapopita huacha njia ikimetameta.
Mtu anaweza kudhani kwamba vilindi vina mvi.
33 Hakuna chochote kilicho kama yeye duniani,
Kiumbe aliyeumbwa asiogope.
34 Hukodolea macho chochote chenye kiburi.
Yeye ni mfalme wa wanyama wote wa mwituni wenye fahari.”
42 Kisha Ayubu akamjibu Yehova:
2 “Sasa ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote
Na kwamba hakuna jambo lolote unalokusudia lisilowezekana kwako.+
3 Ulisema, ‘Ni nani huyu anayepotosha mashauri yangu bila ujuzi?’+
Kwa hiyo nikazungumza, lakini sikuwa na uelewaji
Kuhusu mambo yanayonistaajabisha sana, ambayo siyajui.+
4 Ulisema, ‘Tafadhali sikiliza, nami nitaongea.
Nitakuuliza maswali, nawe unijibu.’+
5 Masikio yangu yamesikia habari zako,
Lakini sasa ninakuona kwa macho yangu.
7 Baada ya Yehova kumwambia Ayubu maneno hayo, Yehova akamwambia Elifazi Mtemani:
“Hasira yangu inawaka dhidi yako na rafiki zako wawili,+ kwa sababu hamkusema ukweli kunihusu+ kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu. 8 Sasa chukueni ng’ombe dume saba na kondoo dume saba kisha mwende kwa mtumishi wangu Ayubu, na mtoe dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Na mtumishi wangu Ayubu atasali kwa ajili yenu.+ Kwa hakika nitakubali ombi lake* nami sitawatendea kulingana na upumbavu wenu, kwa sababu hamkusema ukweli kunihusu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”
9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshua, na Sofari Mnaamathi wakaenda na kufanya kama Yehova alivyowaambia. Kisha Yehova akakubali sala ya Ayubu.
10 Baada ya Ayubu kusali kwa ajili ya rafiki zake,+ Yehova akamwondolea Ayubu dhiki+ na kumrudishia ufanisi wake.* Yehova akampa maradufu ya vitu alivyokuwa navyo awali.+ 11 Ndugu na dada zake wote pamoja na rafiki zake wote wa zamani+ wakaja kwake na kula pamoja naye nyumbani mwake. Wakampa pole na kumfariji kwa sababu ya mateso yote ambayo Yehova alikuwa ameruhusu yampate. Kila mmoja wao akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 Kwa hiyo, Yehova alibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ya kwanza,+ na Ayubu akawa na kondoo 14,000, ngamia 6,000, ng’ombe 2,000,* na punda jike 1,000.+ 13 Akapata pia wana wengine saba na mabinti wengine watatu.+ 14 Akamwita binti yake wa kwanza Yemima, wa pili Kezia, na wa tatu Kereni-hapuku. 15 Katika nchi yote hapakuwa na wanawake warembo kama mabinti wa Ayubu, na baba yao aliwapa urithi pamoja na ndugu zao.
16 Baada ya hayo Ayubu aliishi miaka 140, akawaona watoto wake na wajukuu wake—vizazi vinne. 17 Mwishowe Ayubu akafa, baada ya kuishi maisha marefu na yenye kuridhisha.*
Huenda jina hili linamaanisha “Kitu Kinachochukiwa.”
Au “mtu asiye na lawama na mnyoofu.”
Tnn., “jozi 500 za ng’ombe.”
Au “katika nyumba ya kila mmoja kwa zamu yake.”
Msemo wa Kiebrania unaorejelea malaika, wana wa Mungu.
Tnn., “umeuweka moyo wako juu ya.”
Au “mtu asiye na lawama na mnyoofu.”
Au “kiko chini ya mamlaka yako.”
Tnn., “mbele za uso wa.”
Au labda, “Radi ilianguka kutoka mbinguni ikawateketeza.”
Au “hakusema kwamba Mungu ametenda jambo lolote lisilofaa.”
Msemo wa Kiebrania unaorejelea malaika, wana wa Mungu.
Tnn., “umeuweka moyo wako juu ya.”
Au “mtu asiye na lawama na mnyoofu.”
Tnn., “nimmeze.”
Au “nafsi yake.”
Au “nafsi yake.”
Tnn., “mbele za uso wa.”
Au “vidonda vibaya sana.”
Tnn., “kuilaani siku yake.”
Au “giza na kivuli cha kifo.”
Inaeleweka kwamba maneno haya yanamrejelea mamba au mnyama mwingine mkubwa mwenye nguvu anayekaa ndani ya maji.
Au labda, “Waliojijengea mahali palipo ukiwa.”
Au “wale walio na uchungu nafsini.”
Tnn., “nawe unachoka.”
Au “wanaotunga.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “wajumbe.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au “yatafanya agano (mapatano) nawe.”
Tnn., “ni amani.”
Au “nimezungumza bila kufikiri; harakaharaka.”
Au “hivi kwamba nirefushe maisha yangu (nafsi yangu)?”
Au “Msafara wa Wasabea.”
Tnn., “nikombolewe.”
Au “kubadilishana rafiki yenu kwa mali.”
Tnn., “kaakaa langu halitambui.”
Au “mpaka mapambazuko.”
Tnn., “mema.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kwa uchungu wa nafsi yangu!”
Tnn., “badala ya mifupa yangu.”
Tnn., “kuuweka moyo wako juu yake?”
Tnn., “Aliwatia mikononi mwa uasi wao.”
Tnn., “Angeinuka kwa ajili yako.”
Tnn., “Na kusema maneno yaliyo mioyoni mwao?”
Tnn., “Hivyo ndivyo zilivyo njia za.”
Au “waasi imani.”
Tnn., “nyumba ya.”
Au “Hutazama nyumba ya mawe.”
Au “anapomezwa.”
Au “hivyo ndivyo njia yake itakavyoyeyuka.”
Au “wasio na lawama.”
Tnn., “hatawashika mkono.”
Au “kumpeleka mahakamani.”
Au “huiondoa.”
Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).
Labda ni kundi la nyota la Orioni.
Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.
Tnn., “katika vyumba vya ndani vya kusini.”
Labda ni mnyama mkubwa sana wa baharini.
Au labda, “mshtaki.”
Tnn., “kunipeleka mahakamani?”
Au “Hata nikiwa bila hatia.”
Tnn., “atanitangaza kuwa mpotovu.”
Au “nikiwa bila hatia.”
Au “Siijui nafsi yangu.”
Au “Ninadharau.”
Au “watimilifu.”
Tnn., “nyuso.”
Tnn., “kuwa mwovu.”
Au “magadi.”
Au “kutupatanisha.”
Tnn., “kuweka mkono wake juu yetu wawili.”
Tnn., “angeondoa fimbo yake juu yangu.”
Au “Nafsi yangu inachukia sana.”
Au “kwa uchungu mwingi sana wa nafsi yangu!”
Au “pumzi yangu; uhai wangu.”
Tnn., “Na mambo haya umeyaficha moyoni mwako.”
Au “nichangamke kidogo.”
Au “yenye giza na kivuli cha kifo.”
Au “mwenye kujigamba atakuwa bila kosa?”
Au “mipaka ya.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Wakati tu punda mwitu atakapozaliwa akiwa mwanadamu.”
Tnn., “ninyi ndio watu.”
Tnn., “moyo.”
Au “inateleza.”
Au labda, “zungumza na.”
Au “Nafsi ya kila mtu aliye hai imo.”
Au “pumzi.”
Tnn., “kaakaa linavyoonja.”
Au “bila chochote.”
Au “wazee.”
Tnn., “hulegeza mshipi wa wenye nguvu.”
Tnn., “moyo.”
Au “mtampendelea.”
Au “inayokumbukwa.”
Tnn., “Mafundo ya ngao zenu.”
Tnn., “Kwa nini naubeba mwili wangu kwenye meno yangu?”
Au “nafsi yangu.”
Au “Nitatetea njia zangu.”
Au “mwasi imani.”
Au labda, “Ikiwa mtu anaweza kupambana nami, nitanyamaza na kufa.”
Tnn., “Mambo mawili tu, usinitendee.”
Labda “mwanadamu” anayerejelewa ni Ayubu.
Aina fulani ya mdudu mharibifu.
Au “msukosuko.”
Au labda, “hukatwa.”
Tnn., “unanileta.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Utakuwa na hamu kubwa kwa ajili ya.”
Au “Nafsi yake.”
Au “kwa ujuzi wa ubatili.”
Au “kosa lako linakizoeza kinywa chako.”
Tnn., “mkate.”
Au “kujaribu kumshinda.”
Tnn., “ngao yenye mafundo manene.”
Yaani, tumaini lolote la kupona.
Tnn., “chake.”
Au “waasi imani.”
Au “ya ubatili.”
Au “Ikiwa nafsi zenu zingechukua nafasi ya nafsi yangu.”
Au “Amewaangamiza wale wanaokusanyika nami.”
Au “nguvu zangu.” Tnn., “pembe yangu.”
Au “kivuli cha kifo.”
Au labda, “yakikosa usingizi.”
Au “kuendelea kuangalia.”
Tnn., “methali; msemo.”
Au “mwasi imani.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburi.”
Yaani, tumaini langu.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “wasio safi.”
Au “ukiirarua nafsi yako.”
Au “achechemee.”
Tnn., “Mzaliwa wa kwanza wa kifo anakula.”
Au “kifo kinachotisha.”
Tnn., “Kitu ambacho si chake kitakaa.”
Tnn., “hatakuwa na jina.”
Au “kwenye ardhi inayozaa.”
Au “makao yake ya muda.”
Au “kuikasirisha nafsi yangu.” Angalia Kamusi.
Au “Mmenitukana.”
Au “Watu wangu wa ukoo.”
Tnn., “wana wa tumbo langu la uzazi,” yaani, tumbo lililonibeba (tumbo la mama yangu).
Tnn., “Na hamtosheki na mwili wangu?”
Tnn., “juu ya (kwenye) mavumbi.”
Au “Figo zangu zimeacha kufanya kazi.”
Tnn., “roho inayotoka katika uelewaji wangu inanichochea.”
Au “mwanadamu; Adamu.”
Au “mwasi imani.”
Au “nyongo.”
Tnn., “Ulimi wa nyoka kipiri utamuua.”
Tnn., “naye hatameza.”
Tnn., “roho yangu isingekosa.”
Au “kuwa na nguvu.”
Au “filimbi.”
Au “haraka,” yaani, wanakufa upesi bila maumivu.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Mashauri; Njama za waovu ziko mbali nami.”
Au “imegawanywa mara mbili.”
Au “kumfundisha Mungu jambo lolote.”
Tnn., “umajimaji ulio mifupani haujakauka.”
Au “akiwa na uchungu nafsini.”
Au labda, “ili kunitendea kikatili.”
Tnn., “ishara zao.”
Au “korongoni.”
Tnn., “Naye atawakokota wanadamu wote wamfuate.”
Au “anafurahi.”
Tnn., “unawavua walio uchi mavazi yao.”
Tnn., “mitego ya ndege.”
Au “ambao maisha yao yalifupishwa.”
Tnn., “mto.”
Au “Ukivitupa vipande vyako vya dhahabu.”
Au “makorongoni.”
Au “vipande vyako vya dhahabu.”
Au “walio na macho yanayotazama chini.”
Au “lalamiko langu ni uasi.”
Au “nilivyoagizwa.”
Au “aliyoagiza.”
Yaani, siku yake ya hukumu.
Au “rehani.”
Au labda, “kuvuna chakula cha mifugo shambani.”
Au labda, “Hukamua mafuta katikati ya kuta za matuta.”
Au labda, “Mungu hamhukumu yeyote kwa kutenda mabaya.”
Tnn., “Yeye ni mwepesi juu ya maji.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “Tumbo la uzazi litamsahau.”
Tnn., “njia zao.”
Tnn., “katika vilele vyake.”
Au “safi.”
Au “kwa wingi.”
Au “akili yenu.”
Tnn., “Ni pumzi (roho) ya nani iliyotoka kwenu?”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Abadoni.”
Tnn., “Hutandaza kaskazini.”
Au “kwenye eneo tupu.”
Tnn., “duara.”
Tnn., “Rahabu.”
Tnn., “upepo wake.”
Au “anayenyiririka.”
Tnn., “kutoa methali.”
Au “sitajiondolea; nitadumisha.”
Au “hautanidhihaki.”
Au “siku yoyote maishani mwangu.”
Au “mwasi imani.”
Au “nafsi yake.”
Au labda, “kwa mkono wa.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au labda, “Wanampigia makofi na kumpigia mluzi kutoka mahali pao.”
Tnn., “humwagwa.”
Inaonekana kwamba maneno haya yanahusu uchimbaji wa madini.
Au “iliyosafishwa.”
Tnn., “uzito.”
Tnn., “kutoa methali.”
Au “Watumishi.”
Tnn., “walijificha.”
Yaani, joho lisilo na mikono.
Tnn., “kwenye kiota changu.”
Tnn., “yalitonatona.”
Au labda, “Hawakuitia giza nuru ya uso wangu.”
Au “makorongo.”
Tnn., “Wamepigwa mijeledi na kufukuzwa.”
Tnn., “methali; msemo kwao.”
Tnn., “amelegeza kamba ya upinde wangu.”
Tnn., “Wanatupilia mbali lijamu.”
Au labda, “Na hakuna yeyote anayewasaidia.”
Tnn., “Mifupa yangu inatobolewa.”
Au labda, “Mateso yangu makali yanauharibu mwili wangu.”
Au labda, “unaniyeyusha kwa kishindo.”
Tnn., “kushambulia rundo la magofu.”
Au “walio na siku ngumu?”
Au labda, “homa.”
Au “filimbi.”
Au labda, “na watu wasiopenda kweli?”
Au “acha wazao wangu wang’olewe.”
Tnn., “acha wanaume wengine wapige magoti juu yake.”
Tnn., “unaokula (unaonyafua) na kuangamiza.”
Au “Unaong’oa.”
Au “kesi.”
Tnn., “akiinuka?”
Tnn., “katika tumbo la uzazi.”
Tnn., “niliyadhoofisha macho ya mjane.”
Tnn., “tangu tumboni mwa mama yangu.”
Tnn., “Ikiwa kiuno chake hakikunibariki.”
Au labda, “Nilipoona kwamba nina watu wanaonisaidia katika lango la jiji.”
Au “mtulinga.”
Au “kwenye kiungio chake; kutoka kwenye mfupa wake wa juu.”
Tnn., “nuru iking’aa.”
Tnn., “nyama yake.”
Au “mkaaji mgeni.”
Au “Hii ndiyo sahihi yangu.”
Au “alijiona kuwa mwadilifu.”
Tnn., “Mimi ni mdogo wa siku.”
Tnn., “siku ziseme.”
Au “Siku nyingi peke yake hazimfanyi.”
Au “aliyeweza kumkaripia Ayubu.”
Au “kumpa jina la cheo.”
Tnn., “Ni lazima ulimi wangu na kaakaa langu vizungumze.”
Tnn., “kuyatia muhuri.”
Au “huulinda uhai wake usiingie.”
Au “kaburini.”
Au “kwa silaha.”
Tnn., “uhai wake unachukia.”
Au “inaonekana waziwazi.”
Au “Uhai wake unakaribia.”
Au “kaburini.”
Au “malaika.”
Au “kaburini.”
Tnn., “atawaimbia.”
Au labda, “Nami sikupata faida.”
Au “Ameukomboa uhai wangu usiingie.”
Au “kaburini.”
Au “kaburini.”
Tnn., “kaakaa linavyoonja.”
Tnn., “moyo.”
Au “dunia inayokaliwa.”
Tnn., “moyo wake.”
Tnn., “Miili yote itaangamia.”
Au “watu maarufu na kuwapuuza watu wa hali ya chini.”
Au “mwasi imani.”
Tnn., “moyo.”
Au labda, “Baba yangu, acha Ayubu ajaribiwe.”
Inaelekea anamwambia Mungu.
Tnn., “kutoka mkononi mwa.”
Au “hasikilizi uwongo.”
Tnn., “moyo.”
Au labda, “Huwaketisha wafalme kwenye viti vya ufalme.”
Au “kwa silaha.”
Au “Waasi imani.”
Au labda, “Wakimaliza.”
Au “upige makofi kwa chuki.”
Au labda, “amechambua; amemfanya awajibike kuhusu.”
Au “haichunguziki.”
Tnn., “kibanda chake.”
Tnn., “nuru.”
Tnn., “mizizi ya.”
Au labda, “huwatetea.”
Au labda, “husema ni nini kinachokuja.”
Tnn., “huweka muhuri juu ya mkono wa kila mwanadamu.”
Au “ardhi inayozaa.”
Tnn., “fimbo.”
Au “anavyoyaamuru.”
Au “kuzikunjua.”
Yaani, ya jua.
Tnn., “jifunge.”
Msemo wa Kiebrania unaorejelea malaika, wana wa Mungu.
Au “kuifungafunga katika.”
Tnn., “Je, katika siku zako umeiamuru.”
Au “kivuli cha kifo.”
Tnn., “Na idadi ya siku zako ni nyingi?”
Au labda, “Radi.”
Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.
Labda ni kundi la nyota la Orioni.
Tnn., “Mazarothi.” Kwenye 2Fa 23:5, neno linalohusiana na hilo ambalo liko katika wingi linarejelea makundi ya nyota za unajimu.
Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).
Au labda, “mamlaka Yake.”
Au labda, “ndani ya mwanadamu.”
Au labda, “kuweka uelewaji akilini.”
Au “katika hori lako.”
Au “alime matuta.”
Tnn., “mbegu zako.”
Tnn., “amemfanya asahau.”
Tnn., “Huenda kukutana na silaha.”
Tnn., “Humeza ardhi (dunia).”
Au labda, “Haamini.”
Tnn., “kwenye jino la jabali.”
Tnn., “jifunge.”
Au “utabatilisha.”
Tnn., “Zifunge nyuso zao.”
Au “nitakapokupongeza.”
Labda ni kiboko.
Au “korongoni.”
Tnn., “mtego.”
Labda ni mamba.
Tnn., “unyasi.”
Tnn., “mwiba.”
Au “utaanguka chini.”
Tnn., “uso wake.”
Au labda, “Anajivunia safu zake za magamba.”
Au “ninafuta.”
Tnn., “Kwa hakika nitauinua uso wake.”
Tnn., “Yehova akaondoa utekwa wa Ayubu.”
Yaani, jozi 1,000 za ng’ombe.
Tnn., “akiwa amezeeka na akiwa amejaa siku.”