16 Mwishowe Yehova akamwambia Samweli: “Ni mpaka wakati gani utamwombolezea Sauli,+ huku mimi, kwa upande mwingine, nimemkataa asitawale akiwa mfalme juu ya Israeli?+ Jaza pembe yako mafuta,+ nawe uende. Nitakutuma kwa Yese+ Mbethlehemu, kwa maana nimejipatia mfalme kati ya wanawe.”+