-
Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’Mnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 1
-
-
Kisa kimoja kinachokazia uadui kati ya Raheli na Lea kilihusu matunda fulani ya dudai ambayo Rubeni mwana wa Lea alipata. Watu waliamini kwamba tunda hilo lilimsaidia mwanamke kupata mimba. Raheli alipoomba baadhi ya matunda hayo, Lea alimjibu kwa uchungu: “Je, hili ni jambo dogo, kwamba wewe umemchukua mume wangu, na sasa wewe uzichukue pia dudai za mwanangu?” Watu wengine wanaelewa maneno ya Lea kuwa yanamaanisha kwamba mara nyingi Yakobo alikuwa pamoja na Raheli kuliko Lea. Labda Raheli aliona kwamba Lea alikuwa na sababu nzuri ya kulalamika, kwa kuwa alimjibu hivi: “Kwa sababu hiyo yeye atalala nawe usiku wa leo kwa kubadilishana na dudai za mwana wako.” Hivyo, Yakobo aliporudi nyumbani jioni hiyo, Lea alimwambia hivi: “Utalala nami, kwa sababu nimekukodi moja kwa moja kwa dudai za mwanangu.”—Mwanzo 30:15, 16.
-
-
Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’Mnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 1
-
-
Matunda ya dudai hayakusaidia kupata mimba. Mwishowe, Raheli alipopata mimba na kumzaa Yosefu baada ya miaka sita ya ndoa, ilikuwa kwa sababu Yehova ‘alimkumbuka’ naye akajibu sala yake. Huo ndio wakati tu Raheli angeweza kusema: “Mungu ameondolea mbali shutuma yangu!”—Mwanzo 30:22-24.
-