-
“Kusitawi Wakati wa Kuwa na Kichwa Chenye Mvi”Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
“Kusitawi Wakati wa Kuwa na Kichwa Chenye Mvi”
WATU wengi katika nchi za Mediterania wanapanda mitende katika nyua zao. Miti hiyo inajulikana kwa sababu ya umaridadi wake na matunda yake matamu. Zaidi ya hayo, mitende inaendelea kusitawi kwa miaka zaidi ya mia moja.
-
-
“Kusitawi Wakati wa Kuwa na Kichwa Chenye Mvi”Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Si wanawake warembo peke yao wanaofananishwa na mtende. Mtunga-zaburi aliimba hivi: “Mwadilifu atachanua kama mtende; kama mwerezi katika Lebanoni, atakuwa mkubwa. Wale ambao wamepandwa katika nyumba ya Yehova, katika nyua za Mungu wetu, watachanuka. Bado wataendelea kusitawi wakati wa kuwa na kichwa chenye mvi, wataendelea kuwa wanono na wabichi.”—Zaburi 92:12-14.
Kwa njia ya mfano, wale wanaomtumikia Mungu kwa uaminifu katika maisha yao ya uzee wanalingana sana na mtende maridadi. “Kichwa chenye mvi ni taji la uzuri kinapopatikana katika njia ya uadilifu,” Biblia inasema. (Methali 16:31) Ingawa huenda nguvu zao za kimwili zikapungua kadiri wanavyozeeka, wazee wanaweza kudumisha nguvu zao za kiroho kwa kujilisha kupitia funzo la kawaida la Neno la Mungu, Biblia. (Zaburi 1:1-3; Yeremia 17:7, 8) Maneno yanayovutia ya waaminifu hao walio na umri mkubwa na mfano wao mzuri, unawatia moyo wengine na wanaendelea kuzaa matunda mwaka baada ya mwaka. (Tito 2:2-5; Waebrania 13:15, 16) Kama mtende, wale waliozeeka wanaweza pia kusitawi katika umri wao wa uzee.
-