-
Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”Mkaribie Yehova
-
-
4. Yehova anakumbuka nini kuhusu hali yetu, na hilo linamfanya ashughulike nasi kwa njia gani?
4 Yehova anajua udhaifu wetu. “Yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi,” yasema Zaburi 103:14. Hasahau kwamba sisi ni viumbe wa udongo, wenye kasoro, au udhaifu kwa sababu ya kutokamilika. Usemi kwamba anajua “umbo letu” unatukumbusha kuwa Biblia inamlinganisha Yehova na mfinyanzi na inatulinganisha na vyombo vya udongo anavyofinyanga.a (Yeremia 18:2-6) Mfinyanzi huyo Mkuu anashughulika nasi kupatana na hali yetu dhaifu yenye dhambi ikitegemea jinsi tunavyofuata au kutofuata mwongozo wake.
-
-
Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”Mkaribie Yehova
-
-
a Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “umbo letu” linatumiwa pia kuhusiana na vyombo vya udongo vinavyofinyangwa na mfinyanzi.—Isaya 29:16.
-