-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
Hataogopa hata habari mbaya. Moyo wake ni imara, umefanywa umtegemee Yehova.
-
-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
Katika historia yote, hakujawahi kamwe kuwa na habari nyingi mbaya kama leo, kutia ndani habari za vita, ugaidi, magonjwa mapya na magonjwa ya zamani ambayo yameanza tena kutokea, uhalifu, umaskini, na uharibifu wa mazingira. Wale ambao Mungu anawaona kuwa waadilifu hawawezi kuepuka matokeo mabaya ya habari hizo mbaya, lakini hawafi moyo kwa sababu ya woga. Badala yake, mioyo yao iko “imara” na ‘haitikiswi’ kwa kuwa wanatazamia wakati ujao wakiwa na uhakika, huku wakijua kwamba ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu unakaribia. Wanaweza kuvumilia misiba inayotokea kwa sababu wanategemea msaada wa Yehova.
-
-
Waadilifu Watamsifu Mungu MileleMnara wa Mlinzi—2009 | Machi 15
-
-
16 Waadilifu wa Mungu wanapaswa pia kuvumilia chuki na uwongo unaoenezwa na wapinzani, lakini mbinu hizo zimeshindwa na zitaendelea kushindwa kuwanyamazisha Wakristo wa kweli. Badala yake, watumishi wa Mungu wanaendelea kubaki imara na wasiotikiswa katika kazi ambayo wamepewa na Yehova ya kuhubiri habari njema ya Ufalme na kujifunza na wote wanaokubali.
-