-
‘Tumeumbwa Kwa Njia ya Ajabu’Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 15
-
-
Akili Yetu ya Pekee
12. Ni nini kinachofanya wanadamu wawe tofauti kabisa na wanyama?
12 “Kwa hiyo, jinsi mawazo yako yalivyo yenye thamani kwangu! Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kuu! Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za mchanga.” (Zaburi 139:17, 18a) Wanyama pia wameumbwa kwa njia ya ajabu, na wanyama fulani wana uwezo na hisi fulani ambazo zinapita zile za wanadamu. Lakini Mungu aliwapa wanadamu akili inayopita akili ya mnyama yeyote yule. Kitabu kimoja cha sayansi kinasema hivi: “Ni kweli kwamba sisi wanadamu tunalingana na viumbe wengine kwa njia nyingi, lakini uwezo wetu wa kuzungumza lugha na kufikiri ni wa pekee sana miongoni mwa viumbe walio duniani. Pia, tuna hamu ya pekee sana ya kujua jinsi tulivyo: Mwili wetu umefanywa jinsi gani? Tuliumbwa jinsi gani?” Hayo ni maswali ambayo Daudi pia alifikiria.
13. (a) Daudi angeweza jinsi gani kutafakari kuhusu mawazo ya Mungu? (b) Tunaweza kufuata mfano wa Daudi jinsi gani?
13 Jambo la maana zaidi ni kwamba tofauti na wanyama, tuna uwezo wa pekee sana wa kutafakari kuhusu mawazo ya Mungu.c Zawadi hiyo ya pekee ni moja ya mambo yanayoonyesha tumeumbwa “kwa mfano wa Mungu.” (Mwanzo 1:27) Daudi alitumia zawadi hiyo vizuri. Alitafakari kuhusu mambo yanayothibitisha kwamba kuna Mungu na akatafakari pia kuhusu sifa nzuri zinazoonekana katika dunia. Daudi alikuwa pia na vitabu vya zamani vya Maandiko Matakatifu ambamo Mungu anafunua habari na kazi zake. Maandiko hayo yaliyoongozwa na roho yalimsaidia Daudi kuelewa mawazo, utu, na kusudi la Mungu. Kutafakari kuhusu Maandiko, uumbaji, na jinsi Mungu alivyoshughulika naye kulimchochea Daudi amsifu Mtengenezaji wake.
-
-
‘Tumeumbwa Kwa Njia ya Ajabu’Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 15
-
-
c Inaonekana maneno ya Daudi katika Zaburi 139:18b yanamaanisha kwamba ikiwa angehesabu mawazo ya Yehova siku nzima mpaka alipolala usiku, bado angekuwa na mawazo mengi ya kuhesabu wakati angeamka asubuhi.
-