-
Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Kisha Koreshi akajitayarisha kukabiliana na Babiloni lenye nguvu. Tangu hapo na kuendelea, akaanza kutimiza unabii wa Biblia. Kupitia nabii Isaya, karibu karne mbili mapema, Yehova alikuwa amemtaja Koreshi kuwa mtawala ambaye angeshinda Babiloni na kuwaweka Wayahudi huru kutoka kifungoni. Maandiko humwita Koreshi “masihi” wa Yehova kwa kuwa alichaguliwa mapema.—Isaya 44:26-28.
-
-
Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Kwa Wayahudi waliokuwa Babiloni, ushindi wa Koreshi ulimaanisha kuachiliwa kutoka utekwa kulikongojewa sana na mwisho wa ule ukiwa wa miaka 70 wa nchi ya kwao. Lazima wawe walisisimuka kama nini Koreshi alipotoa tangazo lenye kuwaidhinisha warudi Yerusalemu na kujenga upya hekalu! Koreshi aliwarudishia pia vyombo vitakatifu ambavyo Nebukadreza alikuwa amepeleka Babiloni, akawapa idhini ya kuagiza mbao kutoka Lebanoni, na kuidhinisha fedha kutoka kwa nyumba ya mfalme zilipie gharama za ujenzi.—Ezra 1:1-11; 6:3-5.
-