-
Uwe Mshikamanifu kwa Kristo na kwa Mtumwa Wake MwaminifuMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
Kwa kweli ninawaambia ninyi, Atamweka juu ya mali zake zote.” (Mathayo 24:3, 45-47)
-
-
Uwe Mshikamanifu kwa Kristo na kwa Mtumwa Wake MwaminifuMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
Aliwakubali kwa ujumla kuwa chombo chake, au “mtumwa,” na mnamo 1919 akawaweka wasimamie mali zake zote za kidunia.
Kusimamia Mali za Kidunia za Kristo
6, 7. (a) Yesu alizungumza kuhusu “mtumwa” mwaminifu kwa maneno gani mengine? (b) Yesu anamaanisha nini anapotumia neno “msimamizi-nyumba”?
6 Miezi michache kabla ya Yesu kutoa unabii kuhusu ishara ya kuwapo kwake, kutia ndani kuwapo kwa “mtumwa” ambaye angemwakilisha hapa duniani, alizungumza kuhusu “mtumwa” huyo kwa maneno tofauti kidogo ambayo yanafunua wajibu wa mtumwa huyo. Yesu alisema hivi: “Ni nani kwa kweli aliye msimamizi-nyumba mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka rasmi juu ya watumishi wake kuendelea kuwapa kipimo chao cha chakula katika wakati unaofaa? Ninawaambia ninyi kwa kweli, Yeye atamweka rasmi juu ya mali zake zote.”—Luka 12:42, 44.
7 Katika andiko hilo mtumwa huyo anaitwa msimamizi-nyumba. Neno hilo linatafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki linalomaanisha “msimamizi wa shamba au nyumba.” Jamii hiyo ya msimamizi-nyumba haingekuwa tu kikundi cha wasomi wanaoeleza mambo yenye kupendeza kutoka katika Biblia. Mbali na kuandaa chakula kizuri cha kiroho “kwa wakati unaofaa,” “msimamizi-nyumba mwaminifu” angewekwa rasmi juu ya kikundi kizima cha watumishi wa Kristo, naye angepewa mgawo wa kusimamia kutaniko la Kristo na shughuli zake zote duniani, yaani, “mali zake zote.” Mgawo huo ungetia ndani nini?
8, 9. Mtumwa amewekwa rasmi asimamie “mali” gani?
8 Wajibu wa mtumwa huyo unatia ndani kusimamia majengo na vifaa halisi vinavyotumiwa na wafuasi wa Kristo kuendesha shughuli zao za Kikristo, kama vile makao makuu ya ulimwenguni pote na ofisi za tawi za Mashahidi wa Yehova, na pia mahali pao pa kufanyia ibada, yaani, Majumba ya Ufalme na Majumba ya Makusanyiko ulimwenguni pote. Jambo muhimu zaidi ni kwamba mtumwa huyo anasimamia pia programu za kiroho zenye kujenga za kujifunza Biblia katika mikutano ya kila juma na makusanyiko yanayofanywa mara kwa mara. Katika mikutano na makusanyiko hayo, habari kuhusu kutimizwa kwa unabii wa Biblia inazungumziwa, na mwelekezo unatolewa kwa wakati unaofaa ambao unaonyesha jinsi ya kutumia kanuni za Biblia katika maisha ya kila siku.
9 Wajibu wa msimamizi-nyumba huyo unatia ndani pia kusimamia kazi muhimu zaidi ya kuhubiri “habari njema ya ufalme” na ya kufanya “wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.” Kazi hiyo inatia ndani kuwafundisha watu kufanya mambo yote ambayo Kristo, aliye Kichwa cha kutaniko, aliamuru yafanywe katika wakati huu wa mwisho. (Mathayo 24:14; 28:19, 20; Ufunuo 12:17) Kazi hiyo ya kuhubiri na kufundisha imetokeza “umati mkubwa” wa waandamani washikamanifu wa mabaki watiwa-mafuta. Bila shaka, ‘vitu hivyo vyenye kutamanika vya mataifa yote’ ni sehemu ya “mali” za Kristo zenye thamani ambazo mtumwa mwaminifu anasimamia.—Ufunuo 7:9; Hagai 2:7.
-