-
“Zaidi Ya Mambo Yote, Iweni Na Upendo Mkubwa”Endeleeni Kukesha!
-
-
“Zaidi Ya Mambo Yote, Iweni Na Upendo Mkubwa”
“Mwisho wa mambo yote umekaribia. . . . Zaidi ya mambo yote, iweni na upendo mkubwa ninyi kwa ninyi.”—1 PETRO 4:7, 8.
YESU alijua kwamba saa chache za mwisho pamoja na mitume wake zilikuwa muhimu. Alijua mambo ambayo wangekabili. Walikuwa na kazi nyingi ya kufanya, lakini wangechukiwa na kuteswa kama yeye. (Yohana 15:18-20) Alipokuwa nao usiku wa mwisho, aliwakumbusha tena na tena kwamba wanapaswa ‘kupendana.’—Yohana 13:34, 35; 15:12, 13, 17.
2 Mtume Petro ambaye alikuwapo usiku huo alielewa umuhimu wa kikumbusho cha Yesu. Miaka mingi baadaye, muda mfupi tu kabla ya Yerusalemu kuharibiwa, Petro aliandika na kukazia umuhimu wa upendo. Aliwashauri Wakristo hivi: “Mwisho wa mambo yote umekaribia. . . . Zaidi ya mambo yote, iweni na upendo mkubwa ninyi kwa ninyi.” (1 Petro 4:7, 8) Maneno ya Petro ni yenye maana sana kwa wale wanaoishi “siku za mwisho” za mfumo huu wa mambo. (2 Timotheo 3:1) “Upendo mkubwa” ni nini? Kwa nini ni muhimu tuwaonyeshe wengine upendo huo? Na tunawezaje kuonyesha upendo huo?
“Upendo Mkubwa” Ni Nini?
3 Watu wengi hufikiri upendo ni hisia inayojitokeza yenyewe. Lakini Petro hakuwa akizungumzia upendo wa aina yoyote tu; alikuwa akizungumzia upendo wa hali ya juu sana. Neno “upendo” kwenye 1 Petro 4:8 ni tafsiri ya neno la Kigiriki a·gaʹpe. Neno hilo linamaanisha upendo usio na ubinafsi ambao unaongozwa na kanuni. Kitabu kimoja kinasema: “Mtu anaweza kuamriwa kuonyesha upendo wa agape kwa sababu upendo huo si hisia tu bali ni azimio linalomwongoza kutenda.” Kwa kuwa tumerithi mwelekeo wa kuwa na ubinafsi, tunahitaji kukumbushwa mara kwa mara tupendane kulingana na kanuni za Mungu.—Mwanzo 8:21; Waroma 5:12.
4 Lakini hiyo haimaanishi kwamba tupendane kwa sababu tu tumeamriwa kufanya hivyo. A·gaʹpe si upendo usio na hisia. Petro alisema ni lazima tuwe na ‘upendo mkubwa [kihalisi, “unaopanuka”] sisi kwa sisi.’a (Kingdom Interlinear) Hata hivyo, upendo huo unahitaji jitihada. Msomi mmoja alisema hivi kuhusu neno la Kigiriki linalotafsiriwa “mkubwa”: “Linatoa wazo la mwanariadha anayekaza misuli yake na kujikakamua kwa nguvu zake zote kumaliza mbio.”
5 Basi hatupaswi kuonyesha upendo wetu kwa watu wachache tu au inapokuwa rahisi kufanya hivyo. Tunahitaji ‘kuupanua’ moyo wetu na kuonyesha upendo wa Kikristo hata katika hali ngumu. (2 Wakorintho 6:11-13) Ni wazi kwamba tunahitaji kusitawisha upendo huo na kujitahidi kuukuza kama vile mwanariadha anavyohitaji kufanya mazoezi na kujitahidi kuboresha stadi zake. Ni muhimu kuwa na upendo huo sisi kwa sisi.
-
-
“Zaidi Ya Mambo Yote, Iweni Na Upendo Mkubwa”Endeleeni Kukesha!
-
-
a Kwenye 1 Petro 4:8, tafsiri nyingine za Biblia husema ni lazima tupendane “kutoka moyoni,” “kindani,” au “kwa bidii.”
-
-
“Zaidi Ya Mambo Yote, Iweni Na Upendo Mkubwa”Endeleeni Kukesha!
-
-
7 Pili, ni muhimu sana tupendane zaidi wakati huu ili tuweze kuwasaidia ndugu zetu wenye uhitaji kwa sababu “mwisho wa mambo yote umekaribia.” (1 Petro 4:7) Tunaishi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1) Hali za ulimwengu, misiba ya asili, na upinzani hutuletea magumu. Tunahitaji kuwa na uhusiano wa karibu hata zaidi na wenzetu hali zinapokuwa ngumu. Upendo mkubwa utatuunganisha kabisa na kutuchochea ‘tutunzane.’—1 Wakorintho 12:25, 26.
8 Tatu, tunahitaji kupendana kwa sababu hatutaki ‘kumpa Ibilisi nafasi’ ya kututumia vibaya. (Waefeso 4:27) Shetani yuko macho kutumia kutokamilika kwa waamini wenzetu, iwe ni udhaifu wao, kasoro zao, na makosa yao ili kutukwaza. Je, tutaacha kutaniko kwa sababu mwamini mwenzetu alisema bila kufikiri au alitutendea vibaya? (Methali 12:18) Hatutafanya hivyo ikiwa tuna upendo mkubwa sisi kwa sisi! Upendo huo hutusaidia kudumisha amani na kumtumikia Mungu kwa umoja na “bega kwa bega.”—Sefania 3:9.
-
-
“Zaidi Ya Mambo Yote, Iweni Na Upendo Mkubwa”Endeleeni Kukesha!
-
-
13 Upendo hutusukuma kutokazia fikira kasoro za wengine. Kumbuka kwamba Petro alipowashauri wasomaji wake ‘wawe na upendo mkubwa wao kwa wao,’ alisema ni muhimu sana kufanya hivyo, “kwa sababu upendo hufunika dhambi nyingi.” (1 Petro 4:8) ‘Kufunika’ dhambi hakumaanishi kuficha dhambi nzito. Wale walio na madaraka kutanikoni wanapaswa kujulishwa dhambi hizo ili wazishughulikie. (Mambo ya Walawi 5:1; Methali 29:24) Si jambo la upendo hata kidogo na ni kinyume cha Maandiko kuwaruhusu wale wanaotenda dhambi nzito waendelee kuwaumiza au kuwadhulumu watu wasio na hatia.—1 Wakorintho 5:9-13.
14 Mara nyingi, makosa na kasoro za waamini wenzetu huwa ndogo sana. Nyakati nyingine sote hujikwaa kwa maneno au matendo na kuwavunja moyo au hata kuwaumiza wenzetu. (Yakobo 3:2) Je, tunapaswa kutangaza kasoro za wengine? Kufanya hivyo kutasababisha tu migogoro kutanikoni. (Waefeso 4:1-3) Ikiwa tunaongozwa na upendo, ‘hatutafichua kosa’ la mwabudu mwenzetu. (Zaburi 50:20) Kama vile simiti na rangi zinavyofunika mianya iliyo ukutani, ndivyo upendo unavyofunika kasoro za wengine.—Methali 17:9.
-