Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 1
    • Je, Raheli Apewe Watoto?

      Wakati huo, kutozaa kulionwa kuwa mateso. Mungu alikuwa amewaahidi Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba familia zao zingetokeza “uzao” ambao kupitia huo familia zote zingejibariki. (Mwanzo 26:4; 28:14) Hata hivyo, Raheli hakuwa na mtoto. Yakobo alijua kwamba Mungu tu ndiye angeweza kumpa Raheli watoto, na hivyo kumwezesha kuchangia baraka hizo. Lakini, Raheli hakuwa na subira. Alisema hivi: “Kijakazi wangu Bilha huyu. Lala naye, apate kuzaa magotini pangu ili kwamba mimi, naam mimi, nipate watoto kwake.”—Mwanzo 30:2, 3.

      Huenda ikawa vigumu kwetu kuelewa mtazamo wa Raheli. Hata hivyo, hati za zamani za ndoa zilizopatikana kotekote katika Mashariki ya Karibu zinaonyesha kwamba ilikuwa desturi iliyokubaliwa kwa mke asiyezaa kumpa mume wake msichana mjakazi ili kuzaa mrithi.a (Mwanzo 16:1-3) Katika hali fulani, watoto wa msichana mtumwa walionwa kuwa watoto wa mke huyo.

      Bilha alipozaa mtoto wa kiume, Raheli alifurahi na kutangaza hivi: “Mungu ametenda kama mwamuzi wangu na pia ameisikiliza sauti yangu, akanipa mwana.” Akamwita Dani, jina linalomaanisha “Mwamuzi.” Raheli alisali pia kuhusu hali yake. Bilha alipozaa mwana wake wa pili, Naftali, jina linalomaanisha “Miereka Yangu,” Raheli alisema: “Nimepigana miereka yenye nguvu na dada yangu. Nami nimekuwa mshindi!” Majina hayo yanaonyesha ugomvi mkali uliokuwa kati ya wapinzani hao.—Mwanzo 30:5-8.

      Labda Raheli alifikiri kwamba alikuwa akitenda kupatana na sala zake alipompa Yakobo kijakazi wake Bilha, lakini hiyo haikuwa njia ya Mungu ya kumpa watoto. Kuna somo katika kisa hicho. Hatupaswi kukosa subira tunapomwomba Yehova. Anaweza kujibu sala kwa njia tusizotazamia na wakati tusiotazamia.

  • Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 1
    • a Hati moja kama hiyo kutoka Nuzi, Iraki inasema hivi: “Kelim-ninu ameolewa na Shennima. . . . Ikiwa Kelim-ninu hazai [watoto], Kelim-ninu atatafuta mwanamke [msichana mtumwa] wa nchi ya Lullu ili awe mke wa Shennima.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki