Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baraka za Kimungu kwa “Walio na Akili”
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 1
    • 1. Baada ya kueleza wakati wa taabu juu ya wachochezi wa vita, ndipo yule malaika anaelekeza fikira zake kwenye nini?

      UNABII wa yule malaika aliompa Danieli umetuleta kutoka muda wote wa tangu karne ya nne K.W.K. mpaka kwenye Har–Magedoni. Umeonyesha kwamba Mikaeli ataleta amani duniani katika ile njia pekee inayowezekana: kwa kuharibu wachochezi wa vita. Sasa, baada ya kuchunguza kimbele unabii kwa njia hiyo yenye kutokeza, yule malaika anatabiri baadhi ya baraka nyingi zinazofurahiwa na watu wa Mungu “katika ile sehemu ya mwisho kabisa ya zile siku.”—Danieli 10:14, NW.

      Wakati wa Mafufuo

      2. Baadhi ya waliokufa ‘waliamkaje’ katika wakati wa “ile sehemu ya mwisho kabisa ya zile siku”?

      2 Yule malaika alimwambia Danieli hivi: “Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, na wengine aibu na kudharauliwa [“kukirihiwa,” NW] milele.” (Danieli 12:2) Kwa wazi, “ile sehemu ya mwisho kabisa ya zile siku” ni wakati wa mafufuo, wa kuinua wale “walalao katika mavumbi ya nchi.” Kumojapo kwa kuamshwa huku kulianza upesi baada ya Yesu kuwa Mfalme katika 1914. (Mathayo 24:3) Akitazamia wakati huo, mtume Paulo aliandika: “Sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa [kuwapo, NW] kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala [katika] mauti. . . Waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. (1 Wathesalonike 4:15, 16; Ufunuo 6:9-11) Ni wazi, basi, upesi baada ya 1914 Yesu aliinua kwenye uzima wa kiroho katika mbingu wale wa “Israeli wa Mungu” ambao tayari walikuwa wamekufa wakiwa waaminifu. (Wagalatia 6:16) Kwa wao, kuamshwa kulikuwa kwenye “uzima wa milele.”

      3, 4. Kikundi cha watumishi waaminifu wa Mungu walipataje kuwa ‘wafu’ katika 1918?

      3 Lakini maneno ya yule malaika bila shaka yanatia ndani ufufuo mwingine. Kwa muda wa karibu miaka 40 kutangulia 1914, kikundi kidogo cha Wakristo kilikuwa kimekuwa kikiona kwamba mwaka huo ungetia alama mwisho wa Majira ya Mataifa kama yalivyotabiriwa na Yesu. (Luka 21:24) Wakristo hao waliandikisha kisheria katika 1884 shirika Zion’s Watch Tower Tract Society, na walitangaza matokeo ya uchunguzi wao wa Biblia katika jarida lililoitwa Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence.

      4 Katika 1914 ukweli wa ujumbe wao ulithibitishwa katika njia yenye kutazamisha sana wakati vita ya ulimwengu ya kwanza ilipofyatuka, nayo “maumivu makali ya ghafula ya taabu” yaliyotabiriwa na Yesu yakaanza. (Mathayo 24:7, 8, NW) Hata hivyo, maadui wao wa kidini walitumia kichaa cha vita kuwatesa mpaka mwishowe, katika 1918, kazi yao ya kuhubiri ikawa karibu imesimamishwa na watumishi mashuhuri wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi wakatiwa gerezani isivyo haki. Jambo hilo liliwafanya wengine washangilie sana. Pia lilitimiza ule unabii ulioandikwa katika kitabu cha Ufunuo: “Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika [shimo refu, NW] atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua.”—Ufunuo 11:7.

      5, 6. Mambo yaliyokipata kikundi hiki katika 1919 yalitoaje utimizo wa unabii kwamba “wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka”?

      5 Hata hivyo, kulingana na unabii huo, hawangeendelea kuwa ‘wafu.’ “Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. . . . Wakapanda mbinguni katika wingu, adui zao wakiwatazama.” (Ufunuo 11:11, 12; Ezekieli 37:1-14) Ufufuo wao kwa wazi ulikuwa mfano, kwa kuwa ufufuo halisi kwenye uzima wa roho katika mbingu ungalikuwa usioonekana kwa adui zao. Kwa kweli, wao walifufuliwa kutoka hali kama ya kifo ya kutotenda wakaingizwa kwenye hali yenye kusisimua yenye utendaji wa bidii wakionekana wazi kabisa na wale waliofanya mipango ya hila ya kuwakomesha. Katika 1919 wale wawakilishi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi waliachiliwa kutoka gerezani, kazi ya kuhubiri ilipangwa tena kitengenezo, nao ulimwengu ukaona mwanzo wa kampeni iliyo kubwa zaidi katika historia ya kushuhudia Ufalme.—Mathayo 24:14.

      6 Katika maana hii ya kifano, ‘wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya ardhi waliamka.’ Ndipo, kuanzia 1919, kundi hilo ndogo, lililoamshwa la Wanafunzi wa Biblia lilianza kutafuta na kukusanya mabaki ndugu za Yesu ili ile hesabu kamili ya 144,000 waweze kutiwa muhuri. (Mathayo 24:31; Ufunuo 7:1-3) watu mmoja mmoja walipoitikia, walijiweka wakfu kupitia Kristo wakawa washiriki wa tengenezo lionekanalo la Yehova duniani. Wakipokea kipawa cha bure cha roho takatifu, walitangazwa kuwa waadilifu kwa msingi wa imani yao katika dhabihu ya ukombozi ya Yesu na wakalelewa kuwa wana wa Mungu katika njia ya kiroho.—Warumi 8:16; Wagalatia 2:17; 3:8.

      7. Kwa wengi wa hawa, hili litathibitikaje kuwa kuamka “wapate uzima wa milele”?

      7 Wale kati yao wanaobaki waaminifu mpaka mwisho wa maisha zao za kidunia wana taraja thabiti la kuchukua mahali pao katika mbingu wakiwa pamoja na Yesu Kristo. (1 Wakorintho 15:50-53) Hivyo, kuamshwa kwao kiroho kunakuwa ni kwenye uzima wa milele. Wakati wangali hai duniani, wanapata amani miongoni mwao wenyewe hata ingawa wanaishi katika ulimwengu wenye kupiga vita. (Warumi 14:19) Lakini la maana zaidi, wao wanafurahia amani pamoja na Yehova Mungu mwenyewe, “amani ya Mungu inayoyashinda mawazo yote.” —Wafilipi 4:7, NW.

      Kuamka “Wapate . . . Aibu”

      8, 9. Ni katika njia gani kuamka huku kwa kiroho kungeweza kuwa kwenye “aibu na kudharauliwa milele”?

      8 Ni kwa sababu gani, basi, wengine “wataamka .. . wapate . . . aibu na kudharauliwa milele”? Uhakika ni kwamba, si wote wale wanaokubali mwaliko wa kuwa sehemu ya jamii ya Ufalme huo wanabaki wakiwa waaminifu. Wengine wanaacha imani yao idhoofike na kushindwa kuvumilia. (Waebrania 2:1) Wachache hata wanakuwa waasi-imani na inakuwa lazima waondolewe kutoka kundi la Kikristo. (Mathayo 13:41, 42) Hao wanafanana na yule mwanamume katika mfano wa Yesu aliyeenda kwenye karamu ya arusi lakini akashindwa kuvaa vazi la arusi linalofaa. Yeye alirudishwa katika giza la nje. Ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno” kwake.—Mathayo 22:13; Waefeso 4:18; 5:6-8.

      9 Lo! ni sikitiko kama nini, kukubali pendeleo la juu zaidi sana lililopata kutolewa kwa wanadamu wasiokamilika kisha kugeuka na kulipinga! Kwa habari ya wale wanaotenda katika njia hii, mtume Paulo alisema hivi: “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa [roho takatifu, NW] na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za [mfumo wa mambo ujao, NW] wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa [wamtundika mtini, NW] Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.” (Waebrania 6:4-6) Katika njia hii, kuamka kwao kunakuwa ni kwenye “aibu na kudharauliwa milele.” Wao hawana taraja tena la uzima wa milele.

  • Baraka za Kimungu kwa “Walio na Akili”
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 1
    • Ufufuo Mwingine

      14. Ule unabii wa kwamba “wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka” ukakuja kutia ndani nani wengine?

      14 Hivyo, maneno ya yule malaika yametupeleka mbali kupita wakati wa ‘kusimama’ kwa Mikaeli na “wakati wa taabu” usio na kifani mpaka kuingia mfumo mpya wa mambo. Isitoshe, baraka zinazopitia kwa hao wanaong’aa “kama nyota” hazitakuwa za wale tu wanaookoka huo “wakati wa taabu.” Yesu, alipokuwa angali mwanadamu duniani, alisema: “Saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.” (Yohana 5:28, 29) Maneno haya yanaelekeza kwenye ufufuo halisi wa wanadamu wafu, na bila shaka ufufuo huu, pia, ni utimizo uliopanuliwa wa maneno haya ya yule malaika: “Wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka.”—Danieli 12:2.

      15. Kwa wale wafufuliwao wakati huo, kunaweza kuthibitikaje kuwa kuamka “wapate uzima wa milele”?

      15 Miongoni mwa hao wanaotiwa katika kuamka huku hasa atakuwa Danieli mwenyewe. Aliambiwa hivi na yule malaika: “Lakini enenda zako hata utakapokuwa mwisho ule; maana wewe utastarehe [utalala katika kifo], nawe utasimama katika kura yako mwisho wa siku hizo.” (Danieli 12:13) Wale kama Danieli wanaofufuliwa wakati huu na wanaoitikia huduma ya Yesu na ndugu zake kutoka mbingu watainuliwa kufikia ukamilifu wa kibinadamu. Wapitapo jaribu la mwisho, wataandikisha majina yao kwa kudumu katika kile kitabu cha uzima. (Ufunuo 20:5) Kwao, pia, kuamka kutakuwa kwenye “uzima wa milele.”

      16. Ni kwa akina nani kuamka katika ule mfumo mpya wa mambo kutathibitika kuwa kwenye “aibu na kudharauliwa milele”?

      16 Si wote wataitikia hivyo, hata hivyo. Wengine bila shaka watajaribu kurudisha mazoea ambayo yamenyang’anya wanadamu amani kwa muda mrefu sana. Hao wana onyo linalofaa katika Biblia: “Bali woga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Ufunuo 21:8) Hii “mauti ya pili” ni hukumu ya moja kwa moja kutoka Yehova ambayo katika hiyo hakuna ufufuo. Ni ya milele, kufutiliwa mbali kusiko na mwisho. Wale waliofufuliwa wanaojithibitisha kuwa wasiothamini watapatwa na hiki kifo cha pili; kwa sababu hiyo, kwa kuamshwa kwao, kutakuwa ni kwenye “aibu na kudharauliwa milele.”—Danieli 12:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki