-
Tayari Kuhubiri Licha ya MatesoYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu anawapa mitume wake maagizo bora kuhusu jinsi ya kufanya kazi ya kuhubiri, nao wanaenda wawili wawili. Hata hivyo, anawaambia mambo mengine pia. Kwa fadhili anawaonya kuhusu wapinzani: “Tazama! Ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwamwitu . . . Jihadharini na watu, kwa maana watawapeleka mahakamani na kuwapiga mijeledi katika masinagogi yao. Nanyi mtapelekwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu.”—Mathayo 10:16-18.
-
-
Tayari Kuhubiri Licha ya MatesoYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu anawatia moyo mitume wake 12 na kuwapa maagizo na maonyo hayo yaliyo bora sana! Hata hivyo, inaeleweka kwamba, maneno hayo yanawahusu pia wale ambao watafanya kazi ya kuhubiri baada ya Yesu kufa na kufufuliwa. Hilo linathibitishwa na maneno ambayo Yesu alisema, kwamba wanafunzi wake ‘watachukiwa na watu wote,’ bali si wale tu ambao mitume walitumwa kuwahubiria. Isitoshe, haijaandikwa kwamba mitume walipelekwa mbele ya magavana na wafalme katika kampeni hii fupi ya kuhubiri huko Galilaya, wala kwamba watu wa familia zao waliwatoa ili wauawe.
Ni wazi kwamba Yesu anafikiria wakati ujao anapowaambia mitume mambo hayo. Fikiria maneno aliyosema, kwamba wanafunzi wake hawatamaliza “kuzunguka majiji ya Israeli kabla ya Mwana wa binadamu kufika.” Yesu anaonyesha kuwa mitume wake hawatamaliza kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu kabla ya Mfalme aliyetukuzwa, Yesu Kristo kufika akiwa hakimu wa Mungu.
-