Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Alitupenda Kwanza”
    Mkaribie Yehova
    • Tendo Kubwa Zaidi la Upendo

      4. Ofisa wa jeshi Mroma alipataje kujua kwamba Yesu hakuwa mtu wa kawaida, naye alifikia mkataa gani?

      4 Ofisa wa jeshi Mroma aliyesimamia mauaji ya Yesu, alishangaa alipoona giza lililotokea kabla ya Yesu kufa na tetemeko kubwa la ardhi lililotokea baadaye. Alisema hivi: “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.” (Mathayo 27:54) Ni wazi kwamba Yesu hakuwa mtu wa kawaida. Ofisa huyo aliunga mkono mauaji ya Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu Aliye Juu Zaidi! Mwana huyo alipendwa na Baba yake kwa kadiri gani?

      5. Ni nini kinachothibitisha kwamba Yehova na Mwana wake wamekuwa mbinguni kwa muda mrefu?

      5 Biblia inamwita Yesu “mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” (Wakolosai 1:15) Hilo linamaanisha kwamba Mwana wa Mungu alikuwepo kabla ya ulimwengu kuumbwa. Basi, Mwana huyo alikaa na Baba yake kwa muda gani? Wanasayansi fulani wanakadiria kwamba ulimwengu umekuwapo kwa muda wa miaka bilioni 13. Ni vigumu kwetu hata kuwazia muda huo mrefu sana, sivyo? Hata hivyo, ikiwa wanachosema ni sahihi, hilo linamaanisha kwamba Mwana wa Mungu ameishi kwa muda wa zaidi ya miaka bilioni 13! Alikuwa akifanya kazi gani wakati huo wote?

      6. (a) Mwana wa Mungu alikuwa akifanya nini kabla ya kuwa mwanadamu? (b) Yehova na Mwana wake wanaunganishwa na kifungo cha aina gani?

      6 Mwana huyo alifurahia kutumiwa na Baba yake akiwa “mfanyakazi stadi.” (Methali 8:30) Biblia inasema hivi: “Na bila yeye [Mwana] hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako.” (Yohana 1:3) Kwa hiyo, Yehova na Mwana wake walishirikiana kuumba vitu vingine vyote. Bila shaka, walifurahia sana kufanya kazi pamoja. Watu wengi hukubali kwamba mzazi na mtoto hupendana sana. Na upendo “ni kifungo kikamilifu cha muungano.” (Wakolosai 3:14) Basi, ni nani kati yetu anayeweza kuelewa kikamili nguvu za kifungo ambacho kimekuwapo kwa muda mrefu hivyo? Ni wazi kwamba Yehova Mungu na Mwana wake wameunganishwa na kifungo cha upendo chenye nguvu kuliko kifungo chochote kile.

      7. Yesu alipobatizwa, Yehova alionyeshaje hisia zake kumwelekea?

      7 Ingawa Yehova alimpenda sana Mwana wake, alimtuma aje duniani na kuzaliwa akiwa mwanadamu. Kufanya hivyo kulimaanisha kwamba Yehova hakuweza kushirikiana na Mwana wake mpendwa huko mbinguni kwa miaka kadhaa. Akiwa mbinguni, Yehova alimtazama Yesu akikua hadi kufikia kuwa mwanamume mkamilifu. Yesu alibatizwa alipokuwa na umri wa miaka 30 hivi. Yehova alihisije kumhusu Mwana wake? Yehova mwenyewe alizungumza kutoka mbinguni akisema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” (Mathayo 3:17) Yesu alifanya mambo yote yaliyotabiriwa na ambayo Yehova alimwagiza kufanya. Bila shaka, hilo lilimfurahisha sana Baba yake.​—Yohana 5:36; 17:4.

      8, 9. (a) Yesu alitendewa jinsi gani Nisani 14, mwaka wa 33 W.K., na Baba yake wa mbinguni alihisije? (b) Kwa nini Yehova aliruhusu Mwana wake ateseke na kufa?

      8 Yehova alihisije Nisani 14, mwaka wa 33 W.K.? Alihisije Yesu aliposalitiwa na kukamatwa na umati wa watu usiku huo? Alihisije Yesu alipoachwa na rafiki zake na kushtakiwa isivyo haki? Alihisije Yesu alipodhihakiwa, kutemewa mate, na kupigwa ngumi? Alihisije alipopigwa mijeledi iliyochanachana mgongo wake? Alihisije mikono na miguu yake ilipopigiliwa misumari kwenye mti, kisha akaachwa akiwa amening’inia huku watu wakimtukana? Baba alihisije Mwana wake mpendwa alipokuwa akimlilia akiwa na maumivu makali? Yehova alihisije Yesu alipokata pumzi, na kwa mara ya kwanza kabisa tangu mwanzo wa uumbaji wote, Mwana wake mpendwa akafa?​—Mathayo 26:14-16, 46, 47, 56, 59, 67; 27:38-44, 46; Yohana 19:1.

      9 Kwa kuwa Yehova ana hisia, hatuwezi kamwe kueleza uchungu ambao alihisi kwa sababu ya kifo cha Mwana wake. Lakini tunaweza kuelewa kusudi la Yehova la kuruhusu jambo hilo litokee. Kwa nini Baba ya Yesu aliruhusu maumivu hayo makali yampate? Yehova anatueleza jambo lenye kupendeza katika Yohana 3:16—mstari huu wa Biblia ni muhimu sana hivi kwamba umeitwa Injili ndogo. Andiko hilo linasema: “Kwa maana, Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” Kwa hiyo, Yehova alifanya hivyo kwa sababu ya upendo. Zawadi ambayo Yehova alitoa—kumtuma Mwana wake ateseke na kufa kwa ajili yetu—ndilo tendo kubwa zaidi la upendo ambalo limewahi kufanywa.

      ‘Mungu alimtoa Mwana wake mzaliwa pekee’

  • “Alitupenda Kwanza”
    Mkaribie Yehova
    • 12 Neno A·gaʹpe kama linavyotumiwa mara nyingi katika Biblia, linaleta wazo la upendo unaoongozwa na kanuni. Hiyo ni aina ya upendo ambao hautegemei tu hisia zetu kumwelekea mtu. Upendo huo unatia ndani mambo mengi, unahusisha fikira na una kusudi fulani. Zaidi ya yote, upendo wa Kikristo hauna ubinafsi. Kwa mfano, soma tena Yohana 3:16. Ni “ulimwengu” upi ambao Mungu aliupenda sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee? Ulimwengu huo ni wanadamu wanaoweza kukombolewa. Unatia ndani watu wengi ambao wanaendelea kutenda dhambi maishani. Je, Yehova anampenda kila mtu kama alivyompenda mwanamume mwaminifu Abrahamu, aliyekuwa rafiki yake? (Yakobo 2:23) Hapana, lakini kwa upendo, Yehova anawatendea watu wote mema hata wakati ambapo kufanya hivyo kunamgharimu. Anataka watu wote watubu na kubadili njia zao. (2 Petro 3:9) Wengi hufanya hivyo. Naye hufurahia kuwa rafiki yao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki