-
Je, Ndoa Iwe Muungano wa Maisha?Amkeni!—2001 | Februari 8
-
-
Waefeso 4:26: “Msiache jua litue mkiwa katika hali ya kuchokozeka.”a Mwanamume mmoja mwenye ndoa yenye furaha anaamini kwamba andiko hili humsaidia yeye na mke wake watatue kutoelewana bila kukawia. “Ikiwa huwezi kulala baada ya kutoelewana, mambo hayako sawa. Huwezi kuruhusu tatizo liendelee,” yeye anasema. Nyakati nyingine yeye na mke wake wamezungumzia matatizo yao hadi usiku. Lakini hufanikiwa. Aongeza kusema: “Kutumia kanuni za Biblia kumeleta matokeo mazuri ajabu.” Kwa kufanya hivyo, mwanamume huyo na mke wake wamefurahia maisha ya ndoa yenye furaha kwa miaka 42.
-
-
Je, Ndoa Iwe Muungano wa Maisha?Amkeni!—2001 | Februari 8
-
-
a Kulingana na saa za Mashariki ya Kati ya karne ya kwanza, siku huisha jua linaposhuka. Kwa hiyo Paulo alikuwa akiwatia moyo wasomaji wafanye amani na wengine kabla kila siku kwisha.
-