-
Wachukiwa kwa Sababu ya Imani YaoMnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
-
-
17. Ni nini kionyeshacho kwamba kazi ya kuhubiri ya Wakristo wa karne ya kwanza ilikuwa na matokeo?
17 Wakristo wa karne ya kwanza walihubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu kwa bidii isiyoridhiana. (Mathayo 24:14) Kufikia mwaka wa 60 W.K., Paulo angeweza kusema kwamba habari njema ilikuwa ‘imehubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu.’ (Wakolosai 1:23) Kufikia mwisho wa karne ya kwanza, wafuasi wa Yesu walikuwa wamefanya wanafunzi kotekote katika Milki ya Waroma—katika Asia, Ulaya, na Afrika! Hata washiriki fulani wa “nyumbani mwa Kaisari” wakawa Wakristo.a (Wafilipi 4:22) Kuhubiri huko kwa bidii kulichochea chuki. Neander asema: “Ukristo ulienea hatua kwa hatua miongoni mwa watu wa kila tabaka, ukatisha kuangamiza dini ya taifa.”
-
-
Wachukiwa kwa Sababu ya Imani YaoMnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
-
-
a Si lazima usemi “nyumbani mwa Kaisari” uwe warejezea washiriki wa karibu wa familia ya Nero, aliyekuwa akitawala wakati huo. Badala yake, huenda ukarejezea watumishi wa nyumbani na maofisa wa vyeo vya chini, ambao yawezekana walitoa utumishi wa nyumbani kama vile kupika na kusafisha kwa niaba ya familia ya kifalme na wafanyakazi wao.
-