-
1 Wafalme 1:38-40Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
38 Kisha Sadoki kuhani, Natani nabii, Benaya+ mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti+ wakashuka na wakamupandisha Sulemani juu ya nyumbu wa Mufalme Daudi,+ na wakamupeleka mupaka Gihoni.+ 39 Kisha Sadoki kuhani akakamata pembe ya mafuta+ kutoka katika hema+ na akamutia Sulemani mafuta,+ na wakaanza kupiga baragumu, na watu wote wakaanza kusema kwa sauti kubwa: “Mufalme Sulemani aishi siku nyingi!” 40 Kisha watu wote wakamufuata na kupanda, wakipiga filimbi na kufurahi sana, na hivyo dunia ikapasuka na kufunguka kwa sababu ya makelele yao.+
-