Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 9
Yehova aliendelea kuonya Israeli na Yuda kupitia manabii wake wote.—2 Fa. 17:13.
Mara kwa mara Yehova alitumia manabii wake juu waonye na kurekebisha batu yake. Kwa mufano, Mungu alisema hivi kupitia nabii Yeremia: “Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi . . . Sitakuangalia kwa kasirani, kwa maana mimi ni mushikamanifu . . . Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova.” (Yer. 3:12, 13) Kupitia Yoeli Yehova alisema hivi: “Murudie kwangu kwa mioyo yenu yote.” (Yoe. 2:12, 13) Alimuomba Isaya aseme hivi: “Mujinawishe, mujisafishe; muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu; muache kutenda mabaya.” (Isa. 1:16-19) Kupitia Ezekieli Yehova aliuliza hivi: “Je, ninafurahia kabisa kifo cha mutu muovu? . . . Je, mimi sifurahie kwamba aache njia zake naye aendelee kuishi? Sifurahie hata kidogo kifo cha mutu yeyote, . . . kwa hiyo mugeuke na kuishi.” (Eze. 18:23, 32) Yehova anafurahia kuona batu banatubu juu anapenda baishi milele. w24.08 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 9
Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.—2 Ti. 3:16.
Watu wote wa Yehova wanapata chakula ya kiroho, muongozo, na ulinzi wenye wako nao lazima. Jambo yenye inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi ni hii: Anahakikisha kama watu wote mu dunia wanaweza kupata Biblia. Maandiko Matakatifu iliandikwa mu luga tatu za kwanza-kwanza: Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Je, wale wenye wanajua kusoma zile luga wako na urafiki wa karibu pamoya na Yehova kuliko watu wengine? Hapana. (Mt. 11:25) Haiko masomo yenye tulisoma ao uwezo wetu wa kujua luga fulani njo unafanya Yehova atukubali. Haiko wale wenye walisoma sana njo tu Yehova anapatiaka hekima yake. Watu wote wenye kuwa ku dunia wanaweza kupata hekima yake, ikuwe walisoma sana ao hapana. Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake takatifu, imetafsiriwa mu maelfu ya luga. Kwa hiyo, watu mu dunia yote wanaweza kupata mafundisho yake na kujifunza mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake.—2 Ti. 3:16, 17. w24.06 6-7 fu. 13-15
Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 9
Uharibifu wa Yerusalemu] umekaribia.—Lu. 21:20.
Sawa vile Yesu alitabiri, mupangilio wa mambo wa Wayahudi ulikuwa karibu kuharibiwa. Wakristo walipaswa kutumia wakati yenye ilibakia juu ya kujitayarisha kwa kukomalisha sifa sawa vile imani na uvumilivu. (Ebr. 10:25; 12:1, 2) Hivi karibuni tutapambana na taabu kubwa kupita yenye Wakristo Waebrania walipambana nayo. (Mt. 24:21; Ufu. 16:14, 16) Tuone mashauri fulani yenye Yehova alitolea wale Wakristo juu inaweza pia kutusaidia. Mutume Paulo alitia moyo waamini wenzake wajifunze Neno ya Mungu kwa undani kabisa. (Ebr. 5:14–6:1) Paulo alitumia Maandiko ya Kiebrania ili kufikiri na ndugu zake juu ya kuwasaidia waelewe kama namna ya kuabudu ya Wakristo ni ya hali ya juu sana kupita namna ya kuabudu ya Wayahudi. Paulo alijua kama, ikiwa wale Wakristo wanakuwa na ujuzi ya mingi na ikiwa wanaelewa muzuri zaidi kweli, wataweza kutambua na kuepuka mafundisho ya bongo juu wasidanganywe. w24.09 8-9 fu. 2-3; 10 fu. 6