Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 9
Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.—2 Ti. 3:16.
Watu wote wa Yehova wanapata chakula ya kiroho, muongozo, na ulinzi wenye wako nao lazima. Jambo yenye inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi ni hii: Anahakikisha kama watu wote mu dunia wanaweza kupata Biblia. Maandiko Matakatifu iliandikwa mu luga tatu za kwanza-kwanza: Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Je, wale wenye wanajua kusoma zile luga wako na urafiki wa karibu pamoya na Yehova kuliko watu wengine? Hapana. (Mt. 11:25) Haiko masomo yenye tulisoma ao uwezo wetu wa kujua luga fulani njo unafanya Yehova atukubali. Haiko wale wenye walisoma sana njo tu Yehova anapatiaka hekima yake. Watu wote wenye kuwa ku dunia wanaweza kupata hekima yake, ikuwe walisoma sana ao hapana. Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake takatifu, imetafsiriwa mu maelfu ya luga. Kwa hiyo, watu mu dunia yote wanaweza kupata mafundisho yake na kujifunza mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake.—2 Ti. 3:16, 17. w24.06 6-7 fu. 13-15
Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 9
Uharibifu wa Yerusalemu] umekaribia.—Lu. 21:20.
Sawa vile Yesu alitabiri, mupangilio wa mambo wa Wayahudi ulikuwa karibu kuharibiwa. Wakristo walipaswa kutumia wakati yenye ilibakia juu ya kujitayarisha kwa kukomalisha sifa sawa vile imani na uvumilivu. (Ebr. 10:25; 12:1, 2) Hivi karibuni tutapambana na taabu kubwa kupita yenye Wakristo Waebrania walipambana nayo. (Mt. 24:21; Ufu. 16:14, 16) Tuone mashauri fulani yenye Yehova alitolea wale Wakristo juu inaweza pia kutusaidia. Mutume Paulo alitia moyo waamini wenzake wajifunze Neno ya Mungu kwa undani kabisa. (Ebr. 5:14–6:1) Paulo alitumia Maandiko ya Kiebrania ili kufikiri na ndugu zake juu ya kuwasaidia waelewe kama namna ya kuabudu ya Wakristo ni ya hali ya juu sana kupita namna ya kuabudu ya Wayahudi. Paulo alijua kama, ikiwa wale Wakristo wanakuwa na ujuzi ya mingi na ikiwa wanaelewa muzuri zaidi kweli, wataweza kutambua na kuepuka mafundisho ya bongo juu wasidanganywe. w24.09 8-9 fu. 2-3; 10 fu. 6
Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 9
Kwa kweli Bwana alifufuliwa.—Lu. 24:34.
Banafunzi ya Yesu balikuwa na lazima ya kutiwa moyo. Juu ya nini? Bamoya baliacha nyumba, familia, na kazi juu ya kumufuata Yesu wakati wote. (Mt. 19:27) Bengine balitendewa mubaya juu balikuwa banafunzi ya Yesu. (Yoh. 9:22) Balijitoa sana juu balijua kama Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Mt. 16:16) Lakini wakati Yesu aliuawa, tumaini yabo ilipotea na balivunjika moyo. Yesu hakuona huzuni ya banafunzi yake kuwa alama ya kuonyesha kama habakukuwa nguvu kiroho. Lakini alielewa kama balitenda vile juu balimupoteza. Kwa hiyo, siku ya kwanza tu kisha kufufuka, Yesu alianza kutia moyo barafiki yake. Kwa mufano, alimutokea Maria Magdalene wakati alikuwa nalia ku kaburi. (Yoh. 20:11, 16) Alitokea pia banafunzi bawili benye balikuwa naenda mu kijiji ya Emau. Na alitokea pia mutume Petro. w24.10 13 fu. 5-6