Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 9
Anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.—Ebr. 11:6.
Yehova anapatia zawabu ao anabariki wale wenye kumuabudu. (Ebr. 11:6) Anatupatia amani na anatusaidia tutosheke sasa, na wakati wenye kuya atatupatia uzima wa milele. Tunaweza kumutumainia na kuwa hakika kama anapenda kutupatia zawabu na iko na nguvu ya kufanya vile. Kuwa hakika na ile jambo kunatuchochea tuendelee kumutumikia kwa bidii, sawa vile watumishi wake waaminifu wa zamani walifanya. Ni vile Timoteo alifanya mu karne ya kwanza (Ebr. 6:10-12) Timoteo alimutumainia Mungu mwenye kuishi. (1 Ti. 4:10) Ile ilimuchochea atumike kwa bidii na ajitoe kabisa. Alifanya vile namna gani? Paulo alimutia moyo akuwe mufundishaji muzuri zaidi mu kutaniko na mu mahubiri. Timoteo alipaswa pia kuwekea waabudu wenzake, vijana na wazee, mufano muzuri. Na wakati fulani aliombwa kufanya mambo yenye haikukuwa mwepesi, sawa vile kutolea Wakristo mashauri mazito lakini yenye upendo. (1 Ti. 4:11-16; 2 Ti. 4:1-5) Timoteo angekuwa hakika kuwa Yehova angemupatia zawabu.—Ro. 2: 6, 7. w24.06 22-23 fu. 10-11
Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 9
Yehova aliendelea kuonya Israeli na Yuda kupitia manabii wake wote.—2 Fa. 17:13.
Mara kwa mara Yehova alitumia manabii wake juu waonye na kurekebisha batu yake. Kwa mufano, Mungu alisema hivi kupitia nabii Yeremia: “Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi . . . Sitakuangalia kwa kasirani, kwa maana mimi ni mushikamanifu . . . Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova.” (Yer. 3:12, 13) Kupitia Yoeli Yehova alisema hivi: “Murudie kwangu kwa mioyo yenu yote.” (Yoe. 2:12, 13) Alimuomba Isaya aseme hivi: “Mujinawishe, mujisafishe; muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu; muache kutenda mabaya.” (Isa. 1:16-19) Kupitia Ezekieli Yehova aliuliza hivi: “Je, ninafurahia kabisa kifo cha mutu muovu? . . . Je, mimi sifurahie kwamba aache njia zake naye aendelee kuishi? Sifurahie hata kidogo kifo cha mutu yeyote, . . . kwa hiyo mugeuke na kuishi.” (Eze. 18:23, 32) Yehova anafurahia kuona batu banatubu juu anapenda baishi milele. w24.08 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 9
Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.—2 Ti. 3:16.
Watu wote wa Yehova wanapata chakula ya kiroho, muongozo, na ulinzi wenye wako nao lazima. Jambo yenye inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi ni hii: Anahakikisha kama watu wote mu dunia wanaweza kupata Biblia. Maandiko Matakatifu iliandikwa mu luga tatu za kwanza-kwanza: Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Je, wale wenye wanajua kusoma zile luga wako na urafiki wa karibu pamoya na Yehova kuliko watu wengine? Hapana. (Mt. 11:25) Haiko masomo yenye tulisoma ao uwezo wetu wa kujua luga fulani njo unafanya Yehova atukubali. Haiko wale wenye walisoma sana njo tu Yehova anapatiaka hekima yake. Watu wote wenye kuwa ku dunia wanaweza kupata hekima yake, ikuwe walisoma sana ao hapana. Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake takatifu, imetafsiriwa mu maelfu ya luga. Kwa hiyo, watu mu dunia yote wanaweza kupata mafundisho yake na kujifunza mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake.—2 Ti. 3:16, 17. w24.06 6-7 fu. 13-15