Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 9

Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.—Ufu. 4:11.

Sababu ya maana zaidi yenye inatuchochea kuhubiri habari njema ni juu tunamupenda Mungu na jina yake takatifu. Tunaona kuwa, kazi yetu ya kuhubiri ni nafasi ya kumusifu Mungu mwenye tunapenda. Tunakubaliana kama Yehova Mungu anastahili kupokea utukufu, heshima, na nguvu, kutoka kwa waabudu wake washikamanifu. Tunamutolea Yehova utukufu na heshima wakati tunaonyesha wengine ushuhuda wenye kuonyesha kama ‘aliumba vitu vyote’ na kama ni yeye njo alitupatia uzima. Tunamutolea nguvu yetu wakati tunatumia uwezo wetu, wakati wetu, na vitu vyetu ili kutegemeza kazi ya kuhubiri kadiri hali yetu inaruhusu. (Mt. 6:33; Lu. 13:24; Kol. 3:23) Mu maneno ingine, tunapenda kuzungumuza juu ya Mungu mwenye tunapenda. Tunachochewa pia kuambia wengine kuhusu jina yake na maana ya jina yake. w24.05 17 fu. 11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 9

Anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.—Ebr. 11:6.

Yehova anapatia zawabu ao anabariki wale wenye kumuabudu. (Ebr. 11:6) Anatupatia amani na anatusaidia tutosheke sasa, na wakati wenye kuya atatupatia uzima wa milele. Tunaweza kumutumainia na kuwa hakika kama anapenda kutupatia zawabu na iko na nguvu ya kufanya vile. Kuwa hakika na ile jambo kunatuchochea tuendelee kumutumikia kwa bidii, sawa vile watumishi wake waaminifu wa zamani walifanya. Ni vile Timoteo alifanya mu karne ya kwanza (Ebr. 6:​10-12) Timoteo alimutumainia Mungu mwenye kuishi. (1 Ti. 4:10) Ile ilimuchochea atumike kwa bidii na ajitoe kabisa. Alifanya vile namna gani? Paulo alimutia moyo akuwe mufundishaji muzuri zaidi mu kutaniko na mu mahubiri. Timoteo alipaswa pia kuwekea waabudu wenzake, vijana na wazee, mufano muzuri. Na wakati fulani aliombwa kufanya mambo yenye haikukuwa mwepesi, sawa vile kutolea Wakristo mashauri mazito lakini yenye upendo. (1 Ti. 4:​11-16; 2 Ti. 4:​1-5) Timoteo angekuwa hakika kuwa Yehova angemupatia zawabu.—Ro. 2: 6, 7. w24.06 22-23 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 9

Yehova aliendelea kuonya Israeli na Yuda kupitia manabii wake wote.—2 Fa. 17:13.

Mara kwa mara Yehova alitumia manabii wake juu waonye na kurekebisha batu yake. Kwa mufano, Mungu alisema hivi kupitia nabii Yeremia: “Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi . . . Sitakuangalia kwa kasirani, kwa maana mimi ni mushikamanifu . . . Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova.” (Yer. 3:​12, 13) Kupitia Yoeli Yehova alisema hivi: “Murudie kwangu kwa mioyo yenu yote.” (Yoe. 2:​12, 13) Alimuomba Isaya aseme hivi: “Mujinawishe, mujisafishe; muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu; muache kutenda mabaya.” (Isa. 1:​16-19) Kupitia Ezekieli Yehova aliuliza hivi: “Je, ninafurahia kabisa kifo cha mutu muovu? . . . Je, mimi sifurahie kwamba aache njia zake naye aendelee kuishi? Sifurahie hata kidogo kifo cha mutu yeyote, . . . kwa hiyo mugeuke na kuishi.” (Eze. 18:​23, 32) Yehova anafurahia kuona batu banatubu juu anapenda baishi milele. w24.08 9 fu. 5-6

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine