Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
Matangazo
Luga mupya yenye kupatikana: Sakalava
  • Leo

Siku ya Tano, 28 Mwezi wa 8

Unafungua mukono wako na kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.—Zb. 145:16.

Sawa vile Yehova, na siye tunaweza kupatia watu vitu juu tunawapenda. Kwa mufano, unajua ndugu ao dada fulani mwenye iko na lazima ya chakula ao manguo? Yehova anaweza kukutumikisha juu amupatie ule mutu vitu vyenye iko navyo lazima. Watu wa Yehova wanajulikana kuwa watu wakarimu, zaidi sana wakati wa misiba. Kwa mufano mu kipindi ya Korona ndugu na dada walitolea wengine chakula, manguo, na vitu vingine vya lazima. Pia wengi walitoa michango juu ya kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Ile michango ilifanya iwezekane kusaidia ndugu na dada wa mu dunia yote mu ile kipindi ya nguvu. Wale ndugu na dada wakarimu walifuata shauri yenye kuwa mu Waebrania 13:16 yenye inasema: “Musisahau kutenda mema na kushiriki pamoja na wengine vile vyenye muko navyo, kwa maana Mungu anapendezwa na zabihu za namna hiyo.” w24.09 27 fu. 6-7

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Posho, 29 Mwezi wa 8

Muhakikishe mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.

Fikiria hii hali. Uko natafuta kazi ya kukusaidia kutimiza mahitaji ya familia yako. Unapata kazi mbili. Unatafuta kujua habari zote; kwa mufano ni kazi ya namna gani, programu ya kazi itakuwa namna gani, itakuwa nakamata wakati ngapi juu ya kufika ku kazi, na mambo ingine. Zile kazi zote mbili hazipingane na kanuni za Biblia. Pengine unafurahia zaidi kazi moya kati ya zile kazi mbili juu ni kazi yenye unapendaka ao juu watakuwa nakulipa makuta mingi. Lakini kuko mambo ingine ya kufikiria mbele ya kukamata uamuzi. Kwa mufano, mu zile kazi mbili kuko yenye itakuzuia kukusanyika? Kuko yenye itakukula wakati mingi mupaka ukose wakati wa kupitisha pamoya na familia yako na kuitimizia mahitaji ya kiroho? Kujiuliza maulizo ya vile kutakusaidia utie “mambo ya maana zaidi,” ni kusema ibada na mahitaji ya familia yako, pa nafasi ya kwanza kuliko vitu vya kimwili. Kisha unaweza sasa kukamata uamuzi wenye Yehova atabariki. w25.01 17-18 fu. 11-13

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Yenga, 30 Mwezi wa 8

Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo.—Zb. 34:18.

Hata kama batu fulani balikutendea mubaya, ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anakuona kuwa wa maana. Kama unajisikia kuwa mwenye “kupondwa roho,” kumbuka kama Yehova aliona mambo ya muzuri mu moyo wako na alikualika kwake. (Yoh. 6:44) Kila siku, Yehova iko tayari kukusaidia juu uko wa maana kwake. Wakati tunachunguza mufano wa Yesu, tunaelewa namna Yehova anatuona. Mu utumishi wake ku dunia, Yesu alihangaikia bale benye balikuwa naonewa, na alibatendea muzuri. (Mt. 9:​9-12) Wakati mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa mubaya sana aligusa nguo yake juu apone, Yesu alimufariji na alimupongeza juu ya imani yake. (Mk. 5:​25-34) Yesu anaiga kwa ukamili sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana na anaona sifa zako za muzuri, anaona imani yako, na namna unamupenda. w24.10 7 fu. 4-5

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine