Siku ya Posho, 29 Mwezi wa 8
Muhakikishe mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.
Fikiria hii hali. Uko natafuta kazi ya kukusaidia kutimiza mahitaji ya familia yako. Unapata kazi mbili. Unatafuta kujua habari zote; kwa mufano ni kazi ya namna gani, programu ya kazi itakuwa namna gani, itakuwa nakamata wakati ngapi juu ya kufika ku kazi, na mambo ingine. Zile kazi zote mbili hazipingane na kanuni za Biblia. Pengine unafurahia zaidi kazi moya kati ya zile kazi mbili juu ni kazi yenye unapendaka ao juu watakuwa nakulipa makuta mingi. Lakini kuko mambo ingine ya kufikiria mbele ya kukamata uamuzi. Kwa mufano, mu zile kazi mbili kuko yenye itakuzuia kukusanyika? Kuko yenye itakukula wakati mingi mupaka ukose wakati wa kupitisha pamoya na familia yako na kuitimizia mahitaji ya kiroho? Kujiuliza maulizo ya vile kutakusaidia utie “mambo ya maana zaidi,” ni kusema ibada na mahitaji ya familia yako, pa nafasi ya kwanza kuliko vitu vya kimwili. Kisha unaweza sasa kukamata uamuzi wenye Yehova atabariki. w25.01 17-18 fu. 11-13
Siku ya Yenga, 30 Mwezi wa 8
Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo.—Zb. 34:18.
Hata kama batu fulani balikutendea mubaya, ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anakuona kuwa wa maana. Kama unajisikia kuwa mwenye “kupondwa roho,” kumbuka kama Yehova aliona mambo ya muzuri mu moyo wako na alikualika kwake. (Yoh. 6:44) Kila siku, Yehova iko tayari kukusaidia juu uko wa maana kwake. Wakati tunachunguza mufano wa Yesu, tunaelewa namna Yehova anatuona. Mu utumishi wake ku dunia, Yesu alihangaikia bale benye balikuwa naonewa, na alibatendea muzuri. (Mt. 9:9-12) Wakati mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa mubaya sana aligusa nguo yake juu apone, Yesu alimufariji na alimupongeza juu ya imani yake. (Mk. 5:25-34) Yesu anaiga kwa ukamili sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana na anaona sifa zako za muzuri, anaona imani yako, na namna unamupenda. w24.10 7 fu. 4-5
Siku ya Kwanza, 31 Mwezi wa 8
Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.—Zb. 56:8.
Daudi alipata magumu mingi sana mu maisha yake yenye ilifanya alie. Batu balimuchukia na hata batu benye alitumainia balimusaliti. (1 Sa. 19:10, 11; 2 Sa. 15:10-14, 30) Wakati fulani, aliandika hivi: “Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu; usiku wote ninalowanisha kitanda changu kwa machozi.” (Zb. 6:6) Hata kama Daudi alipata magumu mingi, alikuwa hakika kama Yehova alimupenda. Aliandika hivi: “Yehova atasikia sauti ya kilio changu.” (Zb. 6:8) Maneno ya andiko ya leo inaonyesha wazi namna Yehova anatupenda na kutuhangaikia sana. Daudi alisikia sawa vile Yehova iko anakusanya machozi yake mu chupa ao kuiandika mu kitabu. Daudi alikuwa hakika kama Yehova aliona na alikumbuka maumivu yake. Alikuwa hakika kama Baba yake wa mbinguni mwenye upendo alijua magumu yenye alipita ndani, lakini pia alijua maumivu yenye ile magumu ilimuletea. w24.12 22 fu. 11-12