Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2022)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kufanya utafiti mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
Matangazo
Luga mupya zenye kupatikana: Diola, Mauritian Sign Language
  • Leo

Siku ya Tatu, 10 Mwezi wa 8

Mitume na wazee wakakusanyika pamoja ili kuchunguza jambo hilo.​—Mdo. 15:6.

Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 1988 ulisema hivi: “Wazee wanapaswa kujua kama Kristo, kupitia roho takatifu, anaweza kuongoza muzee yeyote mu baraza ili asaidie wazee wenzake wajue kanuni ya Biblia ya kutumia mu hali fulani ao wakati wanapenda kukamata uamuzi fulani wa maana. (Mdo. 15:7-15) Mu baraza la wazee, hakuna muzee mwenye anapaswa kuwaza kama yeye tu njo iko na roho takatifu.” Muzee mwenye kuheshimia wazee wenzake, anaepukaka kuwa wa kwanza kila mara kutoa mawazo yake ku mikutano ya wazee. Hatawalake mazungumuzo, na hawazake kama maoni yake tu njo ya muzuri. Lakini analetaka mawazo yake kwa unyenyekevu. Anasikilizaka kwa uangalifu wakati wazee wengine wako wanasema. Na jambo la maana zaidi, mawazo yake inategemeaka kanuni za Biblia na muongozo wa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45-47) Wakati wazee wanazungumuza kwa upendo na kwa heshima, roho ya Mungu itakuwa pale, na itawasaidia wakamate maamuzi ya muzuri.​—Yak. 3:17, 18. w20.08 27 fu. 5-6

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2022

Siku ya Ine, 11 Mwezi wa 8

Endelea kushinda uovu kwa wema.​—Ro. 12:21.

Maadui wa Paulo walikuwa wenye nguvu sana kuliko yeye. Mara mingi walimupiga na walimutia mu gereza. Pia, Paulo alitendewa mubaya na watu wenye walipaswa kuwa marafiki wake. Hata wamoja katika kutaniko la Kikristo walimupinga. (2 Ko. 12:11; Flp. 3:18) Lakini, Paulo alipata ushindi juu ya wale wote wenye walimupinga. Juu ya nini tunasema vile? Juu aliendelea kuhubiri hata kama kulikuwa upinzani. Aliendelea kubakia mushikamanifu kwa ndugu na dada zake hata wakati walimuvunja moyo. Na zaidi ya yote, alikuwa muaminifu kwa Mungu mupaka mwisho wa maisha yake. (2 Ti. 4:8) Alipata ushindi juu ya ile matatizo yote, haiko kwa sababu ya nguvu yake ya kimwili, lakini kwa sababu alimutegemea Yehova. Je, kuko watu wenye wako wanakutesa ao kukutukana? Kusudi letu ni kuingiza Neno la Mungu katika akili na mioyo ya watu wenye wako tayari kusikiliza. Tunaweza kufanya vile kwa kutumia Biblia ili kujibia maulizo ya watu, kwa kuheshimia na kutendea muzuri watu wenye kututendea mubaya, na kwa kutendea watu wote mema, hata maadui wetu.​—Mt. 5:44; 1 Pe. 3:15-17. w20.07 17-18 fu. 14-15

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2022

Siku ya Tano, 12 Mwezi wa 8

Unyenyekevu wako unanifanya nikuwe mukubwa.​—2 Sa. 22:36.

Tunaweza kusema kama Yehova ni munyenyekevu? Ndiyo, kama vile ile maneno ya Daudi inaonyesha. (Zb. 18:35) Wakati Daudi alisema vile, pengine alikuwa anakumbuka siku nabii Samweli alikuja kwao ili kutia mafuta mwenye angekuwa mufalme wa Israeli. Baba ya Daudi alikuwa na watoto wanaume munane, na Daudi njo alikuwa mudogo zaidi kati yao. Lakini, yeye njo Yehova alichagua ili akamate nafasi ya Mufalme Sauli. (1 Sa. 16:1, 10-13) Bila shaka Daudi alikubaliana na mawazo ya muandikaji wa zaburi ya 113, mwenye alisema: “Anainama ili aangalie mbingu na dunia, anainua mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi. Anainua maskini . . . ili kumufanya akae pamoja na watu wenye vyeo.” (Zb. 113:6-8) Namna Yehova anatendea watumishi wake wenye hawakamilike inaonyesha kama iko munyenyekevu. Anakubali ibada yetu na anatuona kuwa marafiki wake. (Zb. 25:14) Ili tuweze kuwa marafiki wake, Yehova alimutoa Mwana wake akufe kwa ajili ya zambi zetu. Ile inaonyesha kama Yehova iko na huruma sana. w20.08 8 fu. 1-3

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2022
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kufanya utafiti mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Mapendezi
  • Copyright © 2022 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine