Siku ya Yenga, 8 Mwezi wa 9
Chagua uzima ili uendelee kuishi, wewe na wazao wako.—Kum. 30:19.
Haitoshe tu kuambia watoto wako mambo yenye kuwa mazuri na yale yenye kuwa mabaya. Ni muzuri pia uwasaidie wafikirie maulizo kama vile: ‘Sababu gani Biblia inakataza mambo yenye yanaweza kuonekana kuwa yenye kufurahisha? Ni nini inanihakikishia kuwa kanuni za Biblia ni zenye kuniletea faida sikuzote?’ (Isa. 48:17, 18) Ikiwa mutoto wako anaonyesha kuwa anapenda kubatizwa, unapaswa kumusaidia kufikiri juu ya jambo lingine; iko na mawazo gani juu ya madaraka yenye mutu anakuwa nayo wakati anakuwa Mukristo. Atapata baraka gani? Atapata magumu gani? Namna gani baraka zenye atapata ni nyingi kuliko magumu? (Mk. 10:29, 30) Hayo ni maulizo yenye yanaweza kutokea kisha kubatizwa. Kwa hiyo, ni jambo la maana kufikiria mambo hayo mbele ya kuchukua uamuzi huo muzito. Ikiwa unasaidia watoto wako wafikiri sana juu mambo hayo, hilo linaweza kuwasaidia wakuwe hakika kuwa kanuni za Biblia zitawaletea faida sikuzote. w17.12 21 fu. 14-15
Siku ya Kwanza, 9 Mwezi wa 9
Anaviita vyote kwa jina.—Isa. 40:26.
Wengi kati yenu ndugu na dada wapendwa munapambana na magonjwa hatari. Na wengine, hata kama wamekwisha kukomaa sana, wanahangaikia watu wa jamaa zao wenye kuzeeka. Tena, wengine wanajikaza sana ili kutimizia watu wa familia yao mahitaji ya lazima. Na tunajua kama wengi hawapambane na tatizo moja tu, lakini wanapambana na matatizo mengi kama hayo kwa wakati mumoja! Ikiwa Yehova anahangaikia viumbe vyake vyenye havina uzima, wazia namna gani anakuona wewe mwenye kumutumikia kwa sababu unamupenda, lakini haiko kwa sababu umepangwa kufanya hivyo! (Zb. 19:1, 3, 14) Baba yetu mupendwa anakujua muzuri sana. Biblia inasema hivi: “Nywele zote za vichwa vyenu zimehesabiwa” naye. (Mt. 10:30) Na muandikaji mumoja wa zaburi anatuhakikishia jambo hili: “Yehova anajua mambo yenye watu wenye hawana lawama wanapambana nayo.” (Zb. 37:18) Ndiyo, anajua magumu yenye unapambana nayo, na anaweza kukupatia nguvu ya kuvumilia magumu hayo yote. w18.01 7 fu. 1; 8 fu. 4
Siku ya Pili, 10 Mwezi wa 9
Tabita, simama!—Mdo. 9:40.
Wakati Petro alimufufua Tabita, tukio hilo lilikuwa lenye kusadikisha sana na likafanya ‘wengi wakuwe waamini katika Bwana.’ Wangeweza kutoa ushahidi juu ya Bwana, na zaidi sana juu ya uwezo wa Yehova wa kufufua wafu. (Mdo. 9:36-42) Wengine walijionea ufufuo mwengine. Wakati mumoja Paulo alikuwa katika mukutano fulani katika chumba cha juu katika Troa; sasa ni sehemu ya kaskazini-mangaribi mwa Uturuki. Paulo alizungumuza mupaka katikati ya usiku. Kijana mwanaume mwenye aliitwa Eutiko alikuwa anasikiliza, na alikuwa anakaa kwenye dirisha. Lakini alianza kusinzia na akaanguka chini kutoka kwenye gorofa ya tatu. Pengine munganga Luka ndiye alikuwa wa kwanza kufika mahali penye Eutiko alikuwa na akachunguza hali yake: Eutiko hakuumia tu ao kupoteza akili, lakini alikuwa amekufa! Paulo alishuka chini na akakumbatia mwili huo, na kisha akasema maneno haya yenye kushangaza: “Yeye ni muzima.” Hilo lilipaswa kugusa sana mioyo ya watu wenye walijionea jambo hilo! Kwa sababu walijionea namna Paulo anafufua mutu, “wakafarijika sana.”—Mdo. 20:7-12. w17.12 5 fu. 10-11