Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 7
Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, unikumbuke, tafazali, na kunitia nguvu.—Amu. 16:28.
Nini inakuyaka mu akili yako ukisikia jina Samsoni? Pengine unakumbukaka mwanaume mwenye alikuwa na nguvu ya ajabu. Ni kweli. Lakini Samsoni alikamata uamuzi wa mubaya wenye ulikuwa na matokeo ya kuumiza. Hata vile, Yehova alikazia uangalifu maisha ya uaminifu ya Samsoni na aliiandikisha mu Biblia ili ituletee faida. Yehova alimutumia Samsoni ili kufanya mambo ya ajabu juu ya kusaidia watu wake wenye alikuwa amechagua, ni kusema Waisraeli. Miaka mingi kisha kifo ya Samsoni, Yehova alimuongoza mutume Paulo atie jina ya Samsoni mu liste ya watu wenye walikuwa na imani ya ajabu. (Ebr. 11:32-34) Mufano wa Samsoni unaweza kututia moyo. Alimutegemea Yehova hata wakati hali ilikuwa nguvu. Mufano wake unaweza kututia moyo na mambo ingine yenye unaweza kutufundisha. w23.09 2 fu. 1-2
Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 7
Maombi yenu yajulishwe Mungu.—Flp. 4:6.
Tunaweza kukomalisha sifa ya uvumilivu kwa kumuambia Yehova kwa ukawaida mambo yenye iko natuhangaisha. (1 Te. 5:17) Pengine kwa sasa hauna magumu ya nguvu sana. Hata vile, Je, unamuombaka Yehova akuongoze kila mara wakati unapata magumu, unahangaika, na haujue ufanye nini? Kama unamuombaka Yehova akusaidie saa unapata magumu ya kidogo-kidogo leo, itakuwa mwepesi kwako kufanya vile wakati utapata magumu ya nguvu wakati wenye kuya. Kisha, utakuwa hakika kama anajua kabisa wakati na namna ya kukusaidia. (Zb. 27:1, 3) Itakuwa mwepesi sana kwetu kuvumilia taabu kubwa kama tuko navumilia magumu leo. (Ro. 5:3) Juu ya nini tunasema vile? Ndugu na dada wengi wanasemaka kama kila wakati wenye wanavumilia hali ya nguvu, ile inawasaidiaka wakuwe tayari kuvumilia magumu ingine yenye wanaweza kupata. Wakati wanavumilia magumu kwa musaada wa Yehova, ile inafanya wakuwe na imani kama anapenda kuwasaidia. Na ile imani ya nguvu itawasaidia wavumilie magumu ingine yenye wanaweza kupata.—Yak. 1:2-4. w23.07 3 fu. 7-8
Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 7
Nitakuonyesha ufikirio.—Mwa. 19:21.
Unyenyekevu na huruma inafanyaka Yehova akuwe na usawaziko. Kwa mufano, Yehova alionyesha kama ni munyenyekevu wakati alikuwa karibu kuharibu watu waovu wenye waliishi mu Sodoma. Alituma malaika wamuambie Loti mwenye haki akimbilie mu maeneo ya milima. Loti aliogopa kuenda kule. Njo maana alimuomba sana Yehova aruhusu yeye na familia yake wakimbilie Soari, muji mudogo wenye Yehova alipangaka pia kuharibu. Yehova angemuambia tu Loti aende kule kwenye alikuwa namuambia aende. Lakini, alimuruhusu aende Soari, na hakuharibu tena ule muji. (Mwa. 19:18-22) Karne mingi kisha, Yehova aliwasikilia huruma wakaaji wa Ninawi. Alituma nabii Yona aambie watu waovu wa mu Ninawi kama atawaharibu na kama ataharibu pia muji wao. Lakini wakati watu wa Ninawi walitubu, Yehova aliwasikilia huruma na hakuharibu tena ule muji.—Yon. 3:1, 10; 4:10, 11. w23.07 21 fu. 5