-
1 Wakorinto 16:1Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
16 Sasa kuhusu muchango kwa ajili ya watakatifu,+ munaweza kufuata miongozo yenye nilitoa kwa makutaniko ya Galatia.
-
-
2 Wakorinto 8:1-4Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
8 Basi ndugu, tunataka mujue juu ya fazili zenye hazistahiliwe za Mungu zenye makutaniko ya Makedonia+ yamepewa. 2 Wakati wa jaribu kali chini ya taabu, furaha yao nyingi na umaskini mukubwa vilifanya utajiri wa ukarimu wao ukuwe mwingi.* 3 Kwa maana ilikuwa kulingana na uwezo wao,+ ndiyo, ninatoa ushahidi, hata ilikuwa kupita uwezo wao,+ 4 wakati kwa kupenda kwao wenyewe waliendelea kutuomba sana ili wapate pendeleo la kutoa kwa fazili, ili washiriki katika utumishi wa kutoa musaada kwa ajili ya watakatifu.+
-
-
2 Wakorinto 9:2Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
2 kwa maana ninajua utayari wenu wenye ninajisifia kwa Wamakedonia, kwamba Akaya imekwisha kuwa tayari tangu mwaka mumoja sasa, na bidii yenu imechochea wengi kati yao.
-