Cha Kwanza cha Samweli
15 Kisha Samweli akamuambia Sauli: “Yehova alinituma nikutie mafuta ili ukuwe mufalme juu ya watu wake Israeli;+ sasa sikiliza mambo yenye Yehova anataka kusema.+ 2 Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Nitaomba Waamaleki watoe hesabu kwa sababu ya mambo yenye walifanyia Israeli wakati waliwapinga katika njia yao ya kupanda kutoka Misri.+ 3 Sasa uende, na upige na kuua Waamaleki+ na kuwaharibu+ wao pamoja na vitu vyote vyenye wako navyo. Usikose kuwaharibu;* unapaswa kuwaua wote,+ wanaume na wanamuke, mutoto na mutoto mwenye kunyonya, ngombe-dume na kondoo, ngamia na punda.’”+ 4 Sauli akaita watu na kuwahesabia kule Telaimu: Kulikuwa maaskari elfu mia mbili (200 000) wenye kutembea kwa miguu na watu elfu kumi (10 000) wa Yuda.+
5 Sauli akaenda mupaka kwenye muji wa Amaleki na akavizia karibu na bonde.* 6 Kisha Sauli akaambia Wakeni:+ “Muende, mutoke kati ya Waamaleki ili nisiwafagilie mbali pamoja nao.+ Kwa maana mulionyesha watu wote wa Israeli+ upendo mushikamanifu wakati walipanda kutoka Misri.” Kwa hiyo Wakeni wakatoka katikati ya Amaleki. 7 Kisha Sauli akapiga na kuua Waamaleki+ kuanzia Havila+ mupaka Shuri,+ muji wenye kuwa karibu na Misri. 8 Akamukamata Agagi+ mufalme wa Amaleki akiwa muzima, lakini watu wengine wote akawaharibu kwa upanga.+ 9 Lakini, Sauli na watu wake hawakumuharibu* Agagi na wanyama wazuri sana wa kundi, mifugo, wanyama wenye kunenepa, kondoo-dume, na vitu vyote vyenye vilikuwa vya muzuri.+ Hawakutaka kuviharibu. Lakini vitu vyote vyenye vilikuwa havina mafaa yoyote na vyenye kuzarauliwa, hivyo waliviharibu.
10 Basi neno la Yehova likakuja kwa Samweli: 11 “Ninasikitika* kwamba nimemufanya Sauli kuwa mufalme, kwa sababu ameacha kunifuata na hakutimiza maneno yangu.”+ Samweli akakasirika sana, na akaendelea kumulilia Yehova usiku wote.+ 12 Wakati Samweli aliamuka asubui sana ili akutane na Sauli, Samweli akaambiwa: “Sauli alienda Karmeli,+ na kule alijisimamishia munara.+ Kisha akageuka na kushuka mupaka Gilgali.” 13 Wakati mwishowe Samweli alifika mbele ya Sauli, Sauli akamuambia: “Yehova akubariki. Nimetimiza neno la Yehova.” 14 Lakini Samweli akamuambia: “Basi ni nini sauti hii ya kundi katika masikio yangu na sauti hii ya ngombe yenye ninasikia?”+ 15 Basi Sauli akasema: “Waliletwa kutoka kwa Waamaleki, kwa sababu watu hawakuharibu* wanyama wazuri sana wa kundi na mifugo ili wawatoe zabihu kwa Yehova Mungu wako; lakini vitu vyenye vilibakia tuliviharibu.” 16 Halafu Samweli akamuambia Sauli: “Nyamaza! Acha nikuambie jambo lenye Yehova aliniambia jana usiku.”+ Kwa hiyo akamuambia: “Sema!”
17 Samweli akaendelea kusema: “Je, haukujiona kuwa mutu wa hali ya chini+ wakati ulifanywa kuwa kichwa cha makabila ya Israeli na wakati Yehova alikutia mafuta ili ukuwe mufalme juu ya Israeli?+ 18 Kisha wakati fulani Yehova alikutuma ufanye kazi fulani na kusema, ‘Uende, na uharibu Waamaleki watenda-zambi.+ Pigana nao mupaka wakati utakuwa umewamaliza kabisa.’+ 19 Basi sababu gani haukutii sauti ya Yehova? Lakini, ulikimbilia kwa pupa vitu vyenye vinachukuliwa katika vita+ na ulifanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova!”
20 Hata hivyo, Sauli akamuambia Samweli: “Lakini nimetii sauti ya Yehova! Nilienda kufanya kazi yenye Yehova alinituma nifanye, na nilimuleta Agagi mufalme wa Amaleki, na niliharibu Waamaleki.+ 21 Lakini watu walikamata kondoo na ngombe kati ya vitu vyenye vinachukuliwa katika vita, vitu vya muzuri sana kati ya vitu vyenye vilipaswa kuharibiwa, ili wavitoe zabihu kwa Yehova Mungu wako kule Gilgali.”+
22 Basi Samweli akasema: “Je, Yehova anapendezwa na matoleo ya kuteketezwa na zabihu+ sawasawa na kutii sauti ya Yehova? Angalia! Kutii ni muzuri kuliko zabihu,+ na kusikiliza kwa uangalifu kuliko mafuta+ ya kondoo-dume; 23 kwa maana uasi+ ni sawa na zambi ya uaguzi,+ na kuenda mbele kwa kimbelembele ni sawa na kutumia nguvu za uchawi na ibada ya sanamu.* Kwa sababu umekataa neno la Yehova,+ yeye pia amekukataa usikuwe mufalme.”+
24 Basi Sauli akamuambia Samweli: “Nimetenda zambi, kwa maana nimeasi agizo la Yehova na maneno yako, kwa sababu niliogopa watu na nilisikiliza mambo yenye walisema. 25 Na sasa, tafazali, unisamehe zambi yangu, na urudie pamoja na mimi ili nimuinamie Yehova.”+ 26 Lakini Samweli akamuambia Sauli: “Sitarudia pamoja na wewe, kwa maana umekataa neno la Yehova, na Yehova amekukataa usiendelee kuwa mufalme juu ya Israeli.”+ 27 Wakati Samweli alikuwa anageuka ili aende, Sauli akashika upindo wa koti yake yenye haina mikono, lakini ikapasuka. 28 Basi Samweli akamuambia: “Yehova ameondoa ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, na atamupatia mwenzako mwenye kuwa muzuri kuliko wewe.+ 29 Tena, Mutukufu wa Israeli+ hatasema uongo+ wala kubadilisha nia yake,* kwa maana Yeye haiko mwanadamu bure ili abadilishe nia yake.”*+
30 Basi Sauli akasema: “Nimetenda zambi. Lakini uniheshimishe, tafazali, mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli. Rudia pamoja na mimi, na mimi nitamuinamia Yehova Mungu wako.”+ 31 Kwa hiyo Samweli akarudia nyuma ya Sauli, na Sauli akamuinamia Yehova. 32 Na Samweli akasema: “Mumulete Agagi mufalme wa Waamaleki karibu yangu.” Basi Agagi akaenda karibu naye akisita-sita,* kwa sababu Agagi alikuwa anasema katika moyo wake: “Hakika hatari ya kifo imepita.”* 33 Lakini, Samweli akasema: “Kama vile upanga wako ulifanya wanamuke wakose watoto, ni vile mama yako atakosa watoto kuliko wanamuke wote.” Basi Samweli akamukata-kata Agagi vipande-vipande mbele ya Yehova kule Gilgali.+
34 Kisha Samweli akaenda Rama, na Sauli akapanda kuenda kwenye nyumba yake katika muji wa Gibea wa Sauli. 35 Samweli hakumuona tena Sauli mupaka siku alikufa, kwa maana Samweli alikuwa anamuombolezea Sauli.+ Na Yehova akasikitika kwamba alikuwa amemufanya Sauli kuwa mufalme juu ya Israeli.+