Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Sakalava
  • Leo

Jumapili, Agosti 30

Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo.—Zab. 34:18.

Hata ikiwa wengine wamekutendea kwa njia isiyofaa, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova anakupenda na anakuthamini. Ikiwa unahisi ‘umepondeka roho,’ kumbuka kwamba Yehova aliona mambo mazuri moyoni mwako na alikuvuta kibinafsi kwake. (Yoh. 6:44) Sikuzote yuko tayari kukusaidia kwa sababu wewe ni mwenye thamani kwake. Tunaweza kujifunza kuhusu hisia za Yehova kwa kuchunguza mfano wa Yesu. Wakati wa huduma yake duniani, Yesu aliwaonyesha fadhili wale ambao walidharauliwa na wengine, naye aliwatendea kwa huruma. (Mt. 9:​9-12) Wakati mwanamke aliyetamani kuponywa ugonjwa wake mbaya alipogusa vazi lake, Yesu alimfariji na kumpongeza kwa sababu ya imani yake. (Marko 5:​25-34) Yesu anaiga kikamilifu utu wa Baba yake. (Yoh. 14:9) Hivyo, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova anakuthamini na anaona sifa zako nzuri, kutia ndani imani yako na upendo wako kwake. w24.10 40:4-5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumatatu, Agosti 31

Yakusanye machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi.—Zab. 56:8.

Katika maisha yake, Daudi alikabili hali ngumu kadhaa zilizomfanya atokwe na machozi. Alichukiwa na watu wengine na hata kusalitiwa na wale ambao aliwatumaini. (1 Sam. 19:​10, 11; 2 Sam. 15:​10-14, 30) Pindi moja aliandika hivi: “Nimechoka kwa sababu ya kulia kwa uchungu; usiku kucha ninakilowesha kitanda changu kwa machozi; kochi langu nalifanya lifurike kwa machozi.” (Zab. 6:6) Licha ya hali ngumu ambazo Daudi alikabili, alikuwa na uhakika kwamba Yehova alimpenda. Aliandika hivi: “Yehova atasikia sauti ya kilio changu.” (Zab. 6:8) Maneno ya andiko letu yanaonyesha jinsi Yehova anavyotujali kwa wororo. Daudi alihisi kana kwamba Yehova alikuwa akikusanya machozi yake kwenye kiriba au kuyaandika kwenye kitabu. Daudi alikuwa na uhakika kwamba Yehova aliona na kukumbuka maumivu yake. Daudi alikuwa na uhakika kwamba Baba yake wa mbinguni mwenye upendo alijua mambo ambayo alikuwa amepitia na pia jinsi yalivyomwathiri. w24.12 51:11-12

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumanne, Septemba 1

Endeleeni kujijaribu kama mko katika imani.—2 Kor. 13:5.

Ni lazima tujitahidi sana ili kufikia ukomavu wa kiroho na pia kuudumisha. Ili tufanikiwe tunahitaji kuepuka kujiamini kupita kiasi. (1 Kor. 10:12) Tunapaswa ‘kuendelea kujijaribu’ ili kuhakikisha kwamba tunaendelea kufanya maendeleo. Katika barua yake kwa Wakolosai, mtume Paulo anaonyesha tena kwamba tunahitaji kuendelea kuwa wakomavu. Ingawa Wakristo hao walikuwa wakomavu, Paulo aliwaonya wawe makini ili wasinaswe na njia ya kufikiri ya ulimwengu. (Kol. 2:​6-10) Na Epafra, ambaye inawezekana aliwajua vizuri ndugu na dada kutanikoni, alisali bila kuacha kwamba ‘mwishowe wasimame wakiwa kamili,’ au wakomavu. (Kol. 4:12) Tunaweza kujifunza somo gani? Paulo na Epafra walijua kwamba ili tuendelee kuwa wakomavu tunahitaji kufanya jitihada nyingi na kupata msaada wa Mungu. Walitaka Wakristo Wakolosai waendelee kuwa wakomavu licha ya changamoto walizokuwa wakikabili. w24.04 14:16-17

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki