Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Septemba 3

Je, Mwamuzi wa dunia yote hatatenda jambo la haki?—Mwa. 18:25.

Je, tuna sababu nzuri za kuwa na uhakika kwamba Yehova anapowahukumu watu, sikuzote hukumu zake zote ni za haki? Ndiyo! Abrahamu alielewa vizuri kwamba Yehova ni “Mwamuzi wa dunia yote” ambaye ni mkamilifu, mwenye hekima yote, na mwenye rehema. Amemzoeza Mwana wake na kumkabidhi kazi yote ya kuhukumu. (Yoh. 5:22) Yehova na Mwana wake wanaweza kusoma mambo yaliyo moyoni mwa kila mwanadamu. (Mt. 9:4) Katika kila kisa, watafanya “jambo la haki”! Acheni tuendelee kuazimia kumtumaini Yehova na maamuzi yake yote. Tunatambua kwamba sisi hatustahili kutoa hukumu—lakini yeye anastahili! (Isa. 55:​8, 9) Kwa hiyo, tukiwa na uhakika, tunamwachia kazi yote ya kuhukumu yeye na Mwana wake, Mfalme ambaye anaiga kikamilifu haki na rehema ya Baba yake.—Isa. 11:​3, 4. w24.05 18:18-19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Ijumaa, Septemba 4

Yehova humchukia mtu mwenye hila, lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.—Met. 3:32.

Tunaweza kujifunza kuhusu umuhimu wa kuwa na moyo mnyoofu kwa kuchunguza pindi Yesu na Nathanaeli walipokutana kwa mara ya kwanza. Filipo alipomleta Nathanaeli, rafiki yake, akutane na Yesu, jambo la pekee lilitukia. Ingawa Yesu hakuwa amewahi kukutana na Nathanaeli, alisema hivi: “Ona, Mwisraeli kwa hakika ambaye hamna udanganyifu ndani yake.” (Yoh. 1:47) Yesu aliona unyoofu wa pekee wa Nathanaeli. Kama tu sisi, Nathanaeli alikuwa mtu ambaye si mkamilifu. Lakini hakuwa na unafiki wowote, badala yake alikuwa mnyoofu katika mambo yote. Yesu alivutiwa na jambo hilo na akampongeza Nathanaeli. Matakwa mengi ya kumpendeza Yehova yaliyoorodheshwa kwenye Zaburi ya 15 yanahusu jinsi tunavyowatendea wengine. Zaburi 15:3 inasema kwamba mgeni katika hema la Yehova “hachongei kwa ulimi wake, hamtendei jirani yake jambo lolote ovu, naye hawaharibii sifa rafiki zake.” Kutumia usemi wetu vibaya katika njia hizo kunaweza kuwadhuru sana wengine.—Yak. 1:26. w24.06 24:7, 9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumamosi, Septemba 5

Bwana, hata tunawatiisha roho waovu kwa kutumia jina lako.—Luka 10:17.

Ukijitayarisha vizuri kwa ajili ya huduma, inaelekea kwamba utajihisi huru zaidi unapozungumza na wengine. Yesu aliwasaidia wanafunzi wake wajitayarishe kabla ya kuwatuma kwenda kuhubiri. (Luka 10:​1-11) Kwa kuwa wanafunzi hao walitumia mambo ambayo Yesu aliwafundisha, waliweza kutimiza mambo mengi na hilo lilifanya wawe na shangwe sana. Tunawezaje kujitayarisha kwa ajili ya huduma? Tunahitaji kufikiria jinsi tunavyoweza kuelezea kweli kwa njia yenye matokeo kwa maneno yetu wenyewe. Pia, ingefaa ikiwa utafikiria mapema njia mbili au tatu ambazo watu huitikia katika eneo tunalohubiri na kufikiria jinsi utakavyowajibu. Kisha, tunapozungumza na watu, tutajitahidi kutulia, kutabasamu, na kuwa wenye urafiki. w24.04 16:6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki