Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya inayopatikana: Burkina Faso Sign Language
  • Leo

Jumamosi, Juni 13

Yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.—Ebr. 3:4.

Kadiri mtoto wako anavyojifunza mengi zaidi katika somo la sayansi akiwa shuleni, ndivyo atakavyogundua kwamba kuna sheria zinazoongoza maumbo ya vitu vingi. Kwa mfano, miti mingi ina maumbo yanayojirudia-rudia (fractal patterns). Shina linajigawanya katika matawi na matawi yanajigawanya katika vitawi. Maumbo hayo yanapatikana pia katika vitu vingine. Lakini ni nani aliyeweka sheria zinazotokeza maumbo hayo? Ni nani aliyebuni maumbo hayo yenye mpangilio maridadi? Kadiri mtoto wako anavyotafakari kuhusu maswali hayo, inaelekea ndivyo atakavyoweza kusitawisha imani yenye nguvu kwamba Mungu aliumba vitu vyote. Mtoto wako anapoendelea kukua, unaweza kumuuliza swali hili, “Ikiwa Mungu alituumba, je, inapatana na akili kufikia mkataa kwamba ametupatia pia mwongozo wa maadili ili tuwe na furaha?” Kisha, unaweza kumweleza kwamba mwongozo huo wenye thamani unapatikana katika Biblia. w24.12 50:8

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumapili, Juni 14

Kuna habari kwamba kuna uasherati miongoni mwenu, tena uasherati ambao haujatokea hata miongoni mwa mataifa—mwanamume kuishi na mke wa baba yake.—1 Kor. 5:1.

Chini ya mwongozo wa roho takatifu, mtume Paulo aliandika barua akiagiza kwamba mtenda dhambi asiyetubu alipaswa kuondolewa kutanikoni. (1 Kor. 5:13) Wakristo waaminifu walipaswa kumtendeaje? Paulo aliwaambia ‘waache kushirikiana’ naye. Hilo lilimaanisha nini? Paulo alifafanua kwamba amri hiyo ilitia ndani “hata [kutokula] chakula pamoja na mtu wa namna hiyo.” (1 Kor. 5:11) Unapokula chakula pamoja na mtu, unatumia muda pamoja naye na kuzungumza naye na hilo linaweza kufanya iwe rahisi kuanza kutumia muda zaidi pamoja na mtu huyo. Ni wazi Paulo alimaanisha kwamba kutaniko halipaswi kutumia muda isivyo lazima pamoja na mtu huyo. Jambo hilo lingelilinda kutaniko kutokana na mwenendo wake mbaya. (1 Kor. 5:​5-7) Zaidi ya hilo, kuacha kushirikiana kwa ukaribu na mtu huyo huenda kungemsaidia atambue jinsi alivyo mbali sana na njia za Yehova, na huenda angehisi aibu na kuchochewa kutubu. w24.08 33:4-5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumatatu, Juni 15

Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee.—Yoh. 3:16.

Katika taifa la Israeli, Siku ya Kufunika Dhambi iliadhimishwa mara moja kwa mwaka. Siku hiyo, kuhani mkuu alitoa dhabihu za wanyama kwa niaba ya watu. Bila shaka, dhabihu za wanyama hazingeweza kufunika kabisa dhambi za mtu yeyote kwa sababu wanyama ni duni kwa kulinganishwa na wanadamu. Lakini Yehova alikuwa tayari kusamehe dhambi zao, maadamu Waisraeli waliotubu walitoa dhabihu ambazo aliagiza. (Ebr. 10:​1-4) Mpango huo uliwakumbusha Waisraeli kwamba wao ni watenda. Hata hivyo, Yehova alikuwa na mpango wa kudumu wa kuwasamehe wanadamu dhambi. Alipanga Mwana wake mpendwa “[atolewe] mara moja kwa wakati wote ili kubeba dhambi za wengi.” (Ebr. 9:28) Yesu alitoa “uhai wake uwe fidia badala ya wengi.”—Mt. 20:28. w25.02 6:9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki