Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
Matangazo
Luga mupya yenye kupatikana: Sakalava
  • Leo

Siku ya Pili, 1 Mwezi wa 9

Muendelee kujijaribu ili kuona kama muko katika imani.—2 Ko. 13:5.

Tunapaswa kujikaza kufikia kuwa watu wakomavu kiroho, lakini pia tunapaswa kuendelea kuwa wakomavu. Ili kufanya vile hatupaswe kujitumainia kupita kiasi. (1 Ko. 10:12) Tunapaswa ‘kuendelea kujijaribu’ ili kuhakikisha kama tunaendelea kufanya maendeleo. Mu barua yake kwa Wakolosai, mutume Paulo anakazia tena kama ni jambo ya maana kuendelea kuwa wakomavu kiroho. Hata kama Wakolosai walikuwa watu wazima kiroho, Paulo aliwaambia wakuwe waangalifu ili wasidanganywe na mawazo ya ulimwengu. (Kol. 2:​6-10) Epafra pia, mwenye inaonekana alijua muzuri Wakristo wa ile kutaniko, alisali siku zote ili ‘mwishowe wasimame wakiwa kamili,’ ni kusema wenye kukomaa kiroho. (Kol. 4:12) Ile inatufundisha nini? Paulo na Epafra walielewa kama ili tuendelee kuwa wakomavu kiroho, tuko na lazima ya musaada wa Mungu na tunapaswa kujikaza sana. Walipenda Wakolosai waendelee kuwa wakomavu ao watu wazima kiroho, hata wapambane na magumu gani. w24.04 6-7 fu. 16-17

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Tatu, 2 Mwezi wa 9

Yehova iko pamoja na sisi. Musiwaogope.—Hes. 14:9.

Wakati tunamuogopa Yehova mu njia yenye kufaa, tunamupenda sana na hatupendi hata siku moya kufanya jambo fulani yenye inaweza kumuhuzunisha. Ili Yehova atukubali, tunapaswa kujifunza tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa, kati ya mambo ya kweli na mambo ya uongo. (Mez. 2:​3-6; Ebr. 5:14) Kama tunaanza kuogopa wanadamu kuliko Mungu, pole kwa pole tutaanza kuacha kweli. Fikiria mufano wa wakubwa 12 wenye walienda kupeleleza inchi yenye Yehova alikuwa ameahidi kama atapatia Waisraeli. Woga wenye wale wapelelezi kumi walikuwa nao kwa Wakanaani, ulikuwa nguvu sana kupita upendo wao kwa Yehova. Waliambia hivi Waisraeli wenzao: “Hatuwezi kupanda ili kupigana na watu hao, kwa sababu wako na nguvu kutupita.” (Hes. 13:​27-31) Ku macho ya wanadamu, ni kweli kama Wakanaani walikuwa nguvu zaidi. Lakini kusema kama Waisraeli hawangeweza kushinda maadui wao, ilikuwa kumutia Yehova pembeni. w24.07 9 fu. 5-6

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 9

Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?—Mwa. 18:25.

Unawaza tuko na sababu ya muzuri ya kutumainia hukumu zote za Yehova, hata zikuwe za namna gani? Ndiyo! Sawa vile Abrahamu alielewa, Yehova “Muamuzi wa dunia yote” ni mukamilifu, ni mwenye hekima mingi sana, na ni mwenye rehema. Amezoeza Mwana wake na amemupatia daraka ya kuhukumu wengine. (Yoh. 5:22) Yehova na Mwana wake wanaweza kusoma mambo yenye kuwa mu moyo wa kila mwanadamu. (Mt. 9:4) Sikuzote, wanafanya “jambo lenye kuwa sawa”! Tuazimie basi kumutumainia Yehova na kuwa hakika kama maamuzi yake inakuwaka ya muzuri sikuzote. Tunajua kama hakuna hata mumoja kati yetu mwenye anastahili kuhukumu wengine, lakini Yehova yeye anastahili! (Isa. 55:​8, 9) Kwa hiyo tunaachia Yehova na Mwana wake kazi ya kuhukumu watu. Tuko hakika kama Yesu anaiga rehema na haki ya Baba yake kwa ukamilifu.—Isa. 11:​3, 4. w24.05 7 fu. 18-19

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine