Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 9
Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?—Mwa. 18:25.
Unawaza tuko na sababu ya muzuri ya kutumainia hukumu zote za Yehova, hata zikuwe za namna gani? Ndiyo! Sawa vile Abrahamu alielewa, Yehova “Muamuzi wa dunia yote” ni mukamilifu, ni mwenye hekima mingi sana, na ni mwenye rehema. Amezoeza Mwana wake na amemupatia daraka ya kuhukumu wengine. (Yoh. 5:22) Yehova na Mwana wake wanaweza kusoma mambo yenye kuwa mu moyo wa kila mwanadamu. (Mt. 9:4) Sikuzote, wanafanya “jambo lenye kuwa sawa”! Tuazimie basi kumutumainia Yehova na kuwa hakika kama maamuzi yake inakuwaka ya muzuri sikuzote. Tunajua kama hakuna hata mumoja kati yetu mwenye anastahili kuhukumu wengine, lakini Yehova yeye anastahili! (Isa. 55:8, 9) Kwa hiyo tunaachia Yehova na Mwana wake kazi ya kuhukumu watu. Tuko hakika kama Yesu anaiga rehema na haki ya Baba yake kwa ukamilifu.—Isa. 11:3, 4. w24.05 7 fu. 18-19
Siku ya Tano, 4 Mwezi wa 9
Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.—Mez. 3:32.
Mambo yenye Yesu alisema wakati alikutana na Natanaeli kwa mara ya kwanza inaweza kutufundisha jambo ya maana kuhusu kuwa na moyo wenye hauna udanganyifu. Wakati Filipo alileta rafiki yake Natanaeli ili akutane na Yesu, jambo fulani ya pekee ilitokea. Hata kama ilikuwa mara ya kwanza Yesu aonane na Natanaeli, alisema hivi: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.” (Yoh. 1:47) Yesu aliona unyoofu wa pekee katika Natanaeli. Kama siye wote, Natanaeli pia hakukuwa mukamilifu. Lakini hakukuwa na udanganyifu ndani yake. Yesu alifurahia ile jambo na alimupongeza. Mambo mingi yenye Yehova anatuomba tufanye mu Zaburi 15 ili kumufurahisha inahusu namna tunatendea wengine. Zaburi 15:3 inasema kama mugeni mu hema ya Yehova “hasingizie kwa ulimi wake, hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya, naye hawaharibishie marafiki wake sifa.” Kutumia mubaya ulimi wetu mu ile njia kunaweza kuumiza sana wengine.—Yak. 1:26. w24.06 10 fu. 7, 9; 11 fu. 10
Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 9
Bwana, hata pepo wachafu wanatutii wakati tunatumia jina lako.—Lu. 10:17.
Kama unajitayarisha muzuri kwa ajili ya mahubiri, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuzungumuza na wengine. Mbele ya kuwatuma mu mahubiri, Yesu alisaidia wanafunzi wake wajitayarishe. (Lu. 10:1-11) Juu walitumikisha mambo yenye Yesu aliwafundisha, walifurahi sana kwa sababu ya mambo yenye waliweza kutimiza. Tunaweza kujitayarisha namna gani kwa ajili ya mahubiri? Tufikirie namna tunaweza kufasiria kweli muzuri zaidi mu maneno yetu wenyewe. Pia ni jambo ya maana tufikirie mawazo ao maulizo mbili ao tatu yenye watu wa mu eneo yetu wanazoea kuwa nayo, kisha tufikirie mbele ya wakati namna tunaweza kuwajibu. Na wakati tunakaribia watu, tunaweza kujikaza kutulia, kucheka kidogo, na kuzungumuza nao kwa njia ya urafiki. w24.04 16 fu. 6-7