Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 9
Uharibifu wa Yerusalemu] umekaribia.—Lu. 21:20.
Sawa vile Yesu alitabiri, mupangilio wa mambo wa Wayahudi ulikuwa karibu kuharibiwa. Wakristo walipaswa kutumia wakati yenye ilibakia juu ya kujitayarisha kwa kukomalisha sifa sawa vile imani na uvumilivu. (Ebr. 10:25; 12:1, 2) Hivi karibuni tutapambana na taabu kubwa kupita yenye Wakristo Waebrania walipambana nayo. (Mt. 24:21; Ufu. 16:14, 16) Tuone mashauri fulani yenye Yehova alitolea wale Wakristo juu inaweza pia kutusaidia. Mutume Paulo alitia moyo waamini wenzake wajifunze Neno ya Mungu kwa undani kabisa. (Ebr. 5:14–6:1) Paulo alitumia Maandiko ya Kiebrania ili kufikiri na ndugu zake juu ya kuwasaidia waelewe kama namna ya kuabudu ya Wakristo ni ya hali ya juu sana kupita namna ya kuabudu ya Wayahudi. Paulo alijua kama, ikiwa wale Wakristo wanakuwa na ujuzi ya mingi na ikiwa wanaelewa muzuri zaidi kweli, wataweza kutambua na kuepuka mafundisho ya bongo juu wasidanganywe. w24.09 8-9 fu. 2-3; 10 fu. 6
Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 9
Kwa kweli Bwana alifufuliwa.—Lu. 24:34.
Banafunzi ya Yesu balikuwa na lazima ya kutiwa moyo. Juu ya nini? Bamoya baliacha nyumba, familia, na kazi juu ya kumufuata Yesu wakati wote. (Mt. 19:27) Bengine balitendewa mubaya juu balikuwa banafunzi ya Yesu. (Yoh. 9:22) Balijitoa sana juu balijua kama Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Mt. 16:16) Lakini wakati Yesu aliuawa, tumaini yabo ilipotea na balivunjika moyo. Yesu hakuona huzuni ya banafunzi yake kuwa alama ya kuonyesha kama habakukuwa nguvu kiroho. Lakini alielewa kama balitenda vile juu balimupoteza. Kwa hiyo, siku ya kwanza tu kisha kufufuka, Yesu alianza kutia moyo barafiki yake. Kwa mufano, alimutokea Maria Magdalene wakati alikuwa nalia ku kaburi. (Yoh. 20:11, 16) Alitokea pia banafunzi bawili benye balikuwa naenda mu kijiji ya Emau. Na alitokea pia mutume Petro. w24.10 13 fu. 5-6
Siku ya Posho, 12 Mwezi wa 9
Sikuzote mukuwe tayari kujitetea mbele ya kila mutu mwenye anawauliza ninyi sababu ya tumaini lenye muko nalo.—1 Pe. 3:15.
Muzazi, tayarisha mutoto wako aweze kufasiria juu ya nini anaamini kama kuko Muumbaji. Kati ya mambo yenye inaweza kusaidia sana ni kuchunguza pamoya na mutoto wako habari zenye kuwa ku jw.org chini ya kichwa “Vijana Huuliza— Uumbaji au Mageuzi?” Muchague mafasirio yenye mutoto wako anaona inaweza kusaidia wengine waamini kama kuko Muumbaji. Umutie moyo atumikishe mafasirio yenye kuwa mwepesi kuelewa na yenye kuwa wazi ikiwa kuko mutu mwenye iko tayari kumusikiliza. Kwa mufano, mwanafunzi fulani anaweza kusema hivi: “Miye ninaaminiaka tu mambo yenye ninaona, lakini siyamuonaka Mungu.” Kijana Mukristo anaweza kujibia hivi: “Wazia uko natembea mu pori mbali sana na batu kisha unakuta kisima yenye inajengewa muzuri. Utawaza nini? Kunapaswa kuwa mutu wa akili mwenye alijenga ile kisima. Sasa, tuseme nini juu ya ulimwengu?” w24.12 18 fu. 16