Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 9

Bwana, hata pepo wachafu wanatutii wakati tunatumia jina lako.—Lu. 10:17.

Kama unajitayarisha muzuri kwa ajili ya mahubiri, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuzungumuza na wengine. Mbele ya kuwatuma mu mahubiri, Yesu alisaidia wanafunzi wake wajitayarishe. (Lu. 10:​1-11) Juu walitumikisha mambo yenye Yesu aliwafundisha, walifurahi sana kwa sababu ya mambo yenye waliweza kutimiza. Tunaweza kujitayarisha namna gani kwa ajili ya mahubiri? Tufikirie namna tunaweza kufasiria kweli muzuri zaidi mu maneno yetu wenyewe. Pia ni jambo ya maana tufikirie mawazo ao maulizo mbili ao tatu yenye watu wa mu eneo yetu wanazoea kuwa nayo, kisha tufikirie mbele ya wakati namna tunaweza kuwajibu. Na wakati tunakaribia watu, tunaweza kujikaza kutulia, kucheka kidogo, na kuzungumuza nao kwa njia ya urafiki. w24.04 16 fu. 6-7

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 9

Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.—Ufu. 4:11.

Sababu ya maana zaidi yenye inatuchochea kuhubiri habari njema ni juu tunamupenda Mungu na jina yake takatifu. Tunaona kuwa, kazi yetu ya kuhubiri ni nafasi ya kumusifu Mungu mwenye tunapenda. Tunakubaliana kama Yehova Mungu anastahili kupokea utukufu, heshima, na nguvu, kutoka kwa waabudu wake washikamanifu. Tunamutolea Yehova utukufu na heshima wakati tunaonyesha wengine ushuhuda wenye kuonyesha kama ‘aliumba vitu vyote’ na kama ni yeye njo alitupatia uzima. Tunamutolea nguvu yetu wakati tunatumia uwezo wetu, wakati wetu, na vitu vyetu ili kutegemeza kazi ya kuhubiri kadiri hali yetu inaruhusu. (Mt. 6:33; Lu. 13:24; Kol. 3:23) Mu maneno ingine, tunapenda kuzungumuza juu ya Mungu mwenye tunapenda. Tunachochewa pia kuambia wengine kuhusu jina yake na maana ya jina yake. w24.05 17 fu. 11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026

Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 9

Anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.—Ebr. 11:6.

Yehova anapatia zawabu ao anabariki wale wenye kumuabudu. (Ebr. 11:6) Anatupatia amani na anatusaidia tutosheke sasa, na wakati wenye kuya atatupatia uzima wa milele. Tunaweza kumutumainia na kuwa hakika kama anapenda kutupatia zawabu na iko na nguvu ya kufanya vile. Kuwa hakika na ile jambo kunatuchochea tuendelee kumutumikia kwa bidii, sawa vile watumishi wake waaminifu wa zamani walifanya. Ni vile Timoteo alifanya mu karne ya kwanza (Ebr. 6:​10-12) Timoteo alimutumainia Mungu mwenye kuishi. (1 Ti. 4:10) Ile ilimuchochea atumike kwa bidii na ajitoe kabisa. Alifanya vile namna gani? Paulo alimutia moyo akuwe mufundishaji muzuri zaidi mu kutaniko na mu mahubiri. Timoteo alipaswa pia kuwekea waabudu wenzake, vijana na wazee, mufano muzuri. Na wakati fulani aliombwa kufanya mambo yenye haikukuwa mwepesi, sawa vile kutolea Wakristo mashauri mazito lakini yenye upendo. (1 Ti. 4:​11-16; 2 Ti. 4:​1-5) Timoteo angekuwa hakika kuwa Yehova angemupatia zawabu.—Ro. 2: 6, 7. w24.06 22-23 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine