Ezekieli
2 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu,+ simama kwa miguu yako ili niseme nawe.”+ 2 Na roho ikaanza kuingia ndani yangu mara tu aliposema nami,+ nayo mwishowe ikanifanya nisimame kwa miguu yangu ili nimsikie Yule anayesema nami.+
3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa wana wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Hao wenyewe na mababu zao wamenitendea makosa mpaka siku hii ya leo.+ 4 Na wana wenye uso wa dharau+ na wenye moyo mgumu+—ninakutuma wewe kwao, nawe lazima utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’ 5 Nao, ikiwa watasikia+ au watakataa+—kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi+—hakika watajua pia kwamba nabii alikuwako katikati yao.+
6 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, usiwaogope;+ wala maneno yao usiyaogope, kwa sababu kuna wakaidi+ na vitu vinavyokuwasha+ nawe unakaa katikati ya nge.+ Maneno yao usiyaogope,+ nawe usiingiwe na hofu+ kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.+ 7 Nawe utawaambia maneno yangu, bila kujali ikiwa watasikia au watakataa, kwa maana wao ni waasi.+
8 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, sikia ninalokuambia. Usiwe mwasi kama ile nyumba yenye kuasi.+ Fungua kinywa chako ule ninachokupa.”+
9 Nami nikaanza kuona, na, tazama! kulikuwa na mkono ulionyooshwa kunielekea,+ na, tazama! kitabu cha kukunjwa kilikuwa ndani yake.+ 10 Naye akakikunjua mbele yangu hatua kwa hatua, nacho kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma;+ nacho kilikuwa kimeandikwa nyimbo za huzuni na maombolezo na vilio.+