Ezekieli
3 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, kula unachoona. Kula kitabu hiki cha kukunjwa,+ uende, ukaseme na nyumba ya Israeli.”
2 Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye hatua kwa hatua akanilisha kile kitabu.+ 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, unapaswa kulisha tumbo lako, ili ujaze matumbo yako kwa kitabu hiki ninachokupa wewe.” Nami nikaanza kukila, nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu.+
4 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, nenda, uingie katikati ya nyumba+ ya Israeli, nawe lazima uwaambie maneno yangu. 5 Kwa maana hutumwi kwenda kwa watu wa lugha isiyoeleweka+ wala walio wazito wa ulimi+—kwa nyumba ya Israeli, 6 si kwa vikundi vya watu wengi sana wa lugha isiyoeleweka wala walio wazito wa ulimi, ambao maneno yao huwezi kuyasikia ukayafahamu.+ Ikiwa ningekutuma kwao, watu hao wangekusikiliza wewe.+ 7 Lakini nyumba ya Israeli, hawatataka kukusikiliza wewe, kwa maana hawataki kunisikiliza mimi;+ kwa sababu wote hao wa nyumba ya Israeli wana vichwa vigumu na mioyo migumu.+ 8 Tazama! Nimeufanya uso wako uwe mgumu+ kama nyuso zao na paji la uso wako liwe gumu kama mapaji ya nyuso zao.+ 9 Nimelifanya paji la uso wako kuwa kama almasi, gumu kuliko jiwe gumu.+ Usiwaogope,+ wala usiingiwe na hofu kwa sababu ya nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.”+
10 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, maneno yangu yote nitakayokuambia, yatie moyoni+ mwako na usikie kwa masikio yako mwenyewe. 11 Nawe uende, uingie katikati ya watu waliohamishwa,+ katikati ya wana wa watu wako, nawe utasema nao na kuwaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema,’ bila kujali ikiwa watasikia au watakataa.”+
12 Nayo roho ikaniinua+ nami nikaanza kusikia nyuma yangu kishindo cha mvumo mkubwa:+ “Na ubarikiwe utukufu wa Yehova kutoka katika mahali pake.”+ 13 Na kulikuwa na kishindo cha mabawa ya wale viumbe hai yaliyokuwa yakigusana karibu karibu,+ na kishindo cha magurudumu karibu nao kando yao,+ na kishindo cha mvumo mkubwa. 14 Nayo roho ikaniinua+ na kunichukua, hivi kwamba nikaenda kwa uchungu katika ghadhabu ya roho yangu, na mkono wa Yehova juu yangu ulikuwa wenye nguvu.+ 15 Kwa hiyo nikaingia katikati ya watu waliohamishwa huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa+ kando ya mto Kebari,+ nami nikaanza kukaa mahali walipokuwa wakikaa; nami nikaendelea kukaa hapo kwa siku saba, nikiwa nimepigwa na bumbuazi katikati yao.+
16 Na ikawa kwamba mwishoni mwa siku saba neno la Yehova likanijia, na kusema:
17 “Mwana wa binadamu, nimekufanya kuwa mlinzi katika nyumba ya Israeli,+ nawe utasikia maneno kutoka katika kinywa changu nawe lazima utawapa maonyo kutoka kwangu.+ 18 Mimi ninapomwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’+ na wewe usimwonye na kusema ili kumwonya mwovu aiache njia yake ya uovu ili kumhifadhi hai,+ yeye akiwa ni mwovu, katika kosa lake atakufa,+ lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.+ 19 Lakini wewe, ikiwa umemwonya mwovu+ naye asigeuke na kuuacha uovu wake na njia yake ya uovu, yeye mwenyewe atakufa kwa sababu ya kosa lake;+ lakini wewe, utakuwa umeiokoa nafsi yako mwenyewe.+ 20 Na mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu+ wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki nami nilazimike kuweka kikwazo mbele yake,+ yeye mwenyewe atakufa kwa sababu hukumwonya. Kwa sababu ya dhambi yake atakufa,+ na matendo yake ya uadilifu aliyoyatenda hayatakumbukwa,+ lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.+ 21 Na wewe, ikiwa umemwonya mtu mwadilifu kwamba mwadilifu huyo asitende dhambi, naye mwenyewe aepuke kutenda dhambi,+ hakika ataendelea kuishi kwa sababu alikuwa ameonywa,+ na wewe mwenyewe utakuwa umeiokoa nafsi yako mwenyewe.”+
22 Nao mkono wa Yehova ukawa juu yangu huko, naye akaniambia: “Ondoka, nenda kwenye nchi tambarare ya bondeni,+ na huko nitasema nawe.” 23 Basi nikaondoka na kwenda kwenye nchi tambarare ya bondeni, na, tazama! utukufu wa Yehova ulikuwa umesimama huko,+ kama utukufu niliouona kando ya mto Kebari,+ nami nikaanguka kifudifudi.+ 24 Ndipo roho ikaingia+ ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu,+ naye akaanza kusema nami na kuniambia:
“Nenda, jifungie ndani ya nyumba yako. 25 Na wewe, Ee mwana wa binadamu, tazama! hakika wataweka kamba juu yako nao watatumia kamba hizo kukufunga ili usiweze kwenda katikati yao.+ 26 Nami nitaufanya ulimi wako ushikamane na kaakaa la kinywa chako,+ nawe hakika utakuwa bubu,+ na kwao wewe hutakuwa mtu mwenye kutoa karipio,+ kwa sababu wao ni nyumba yenye kuasi.+ 27 Nami ninaposema nawe, nitakifungua kinywa chako, nawe utawaambia,+ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’ Anayesikia na asikie,+ na anayekataa na akatae, kwa sababu wao ni nyumba yenye kuasi.+