-
Ezekieli 18:24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 “ ‘Sasa, mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki;+ kulingana na machukizo yote ambayo mwovu ametenda yeye anaendelea kutenda+ naye anaishi, hakuna lolote la matendo yake ya uadilifu ambayo ametenda litakalokumbukwa.+ Atakufa kwa sababu ya ukosefu wake wa uaminifu ambao ametenda na kwa sababu ya dhambi ambayo ametenda.+
-
-
Ezekieli 33:12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, waambie wana wa watu wako, ‘Uadilifu wenyewe wa mwadilifu hautamkomboa katika siku ya maasi yake.+ Lakini kwa habari ya uovu wa mwovu, hautamtikisa katika siku atakapogeuka na kuuacha uovu wake.+ Wala hata mtu yeyote mwenye uadilifu hataweza kuendelea kuishi kwa sababu ya huo siku ile atakapotenda dhambi.+
-