Ezekieli
18 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Inamaanisha nini kwenu kwamba mnataja neno hili la kimethali kwenye udongo wa Israeli, na kusema, ‘Akina baba ndio wanaokula zabibu mbichi, lakini meno ya wana ndiyo yanayotiwa ukakasi’?+
3 “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hamtaendelea kuwa na sababu ya kulitaja neno hili la kimethali katika Israeli. 4 Tazama! Nafsi zote—ni zangu.+ Kama ilivyo nafsi+ ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu.+ Nafsi inayotenda dhambi+—hiyo yenyewe itakufa.+
5 “ ‘Na mtu, ikiwa ni mwadilifu naye ametenda haki na uadilifu;+ 6 naye hakula+ juu ya milima+ wala hakuyainua macho yake kuelekea sanamu za mavi za nyumba ya Israeli,+ wala hakumnajisi mke wa mwenzake+ wala hakumkaribia mwanamke aliye katika uchafu wake;+ 7 wala hakumtendea vibaya mtu yeyote;+ rehani aliyotwaa kwa ajili ya deni, alikuwa akiirudisha;+ hakuwa akinyakua chochote kwa unyang’anyi;+ mkate wake mwenyewe alikuwa akimpa mwenye njaa+ na alikuwa akimvika vazi aliye uchi;+ 8 naye hakuwa akitoa chochote apate faida+ wala hakuwa akichukua riba yoyote;+ naye alikuwa akiuepusha mkono wake na ukosefu wa haki;+ naye alikuwa akiitenda haki ya kweli kati ya mtu na mwenzake;+ 9 naye aliendelea kutembea katika amri zangu+ na aliyashika maamuzi yangu ya hukumu ili kutenda kweli,+ yeye ni mwadilifu.+ Hakika yeye ataendelea kuishi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
10 “ ‘Na ikiwa mtu amemzaa mwana ambaye ni mnyang’anyi,+ mmwagaji wa damu,+ ambaye amefanya jambo linalofanana na moja kati ya mambo hayo 11 (lakini yeye mwenyewe hajafanya lolote la mambo hayo); ikiwa yeye pia amekula juu ya milima,+ naye amemnajisi mke wa mwenzake;+ 12 naye amemtendea vibaya mtu mwenye kuteseka na aliye maskini;+ naye amenyakua vitu kwa unyang’anyi,+ naye hakuwa akirudisha kitu kilichowekwa rehani;+ naye aliyainua macho yake kuelekea sanamu za mavi,+ yeye amefanya chukizo.+ 13 Ametoa kwa riba,+ na amechukua faida,+ naye hakika hataendelea kuishi. Ameyafanya machukizo hayo yote.+ Hakika atauawa. Damu yake mwenyewe itakuwa juu yake.+
14 “ ‘Na, tazama! mtu amemzaa mwana, ambaye anaendelea kuona dhambi zote za baba yake ambazo amefanya, naye anaona lakini hafanyi mambo kama hayo.+ 15 Hajakula juu ya milima, naye hajayainua macho yake kuelekea sanamu za mavi za nyumba ya Israeli;+ hajamnajisi mke wa mwenzake;+ 16 wala hajamtendea vibaya+ mtu yeyote, hajachukua rehani+ yoyote, wala hajachukua chochote kwa unyang’anyi;+ yeye amempa mwenye njaa mkate wake mwenyewe,+ na amemvika vazi aliye uchi;+ 17 ameuepusha mkono wake na mwenye kuteseka; hajachukua riba+ wala faida+ yoyote; ameyafanya maamuzi yangu ya hukumu;+ ametembea katika amri zangu;+ yeye mwenyewe hatakufa kwa sababu ya kosa la baba yake.+ Hakika ataendelea kuishi.+ 18 Naye baba yake, kwa sababu alifanya unyang’anyi+ wa moja kwa moja, alinyakua kitu kwa kumnyang’anya ndugu,+ na lolote ambalo si zuri amelifanya katikati ya watu wake,+ tazama! basi lazima afe kwa ajili ya kosa lake.+
19 “ ‘Nanyi hakika mtasema: “Kwa nini mwana hawezi kuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la baba?”+ Sasa kwa habari ya mwana huyo, yeye ametenda haki na uadilifu,+ amezishika amri zangu zote naye anaendelea kuzitenda.+ Hakika ataendelea kuishi.+ 20 Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.+ Mwana hatakuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la baba, na baba hatakuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la mwana.+ Uadilifu wa mwadilifu utakuwa juu yake mwenyewe,+ nao uovu wa mwovu utakuwa juu yake mwenyewe.+
21 “ ‘Sasa kwa habari ya mwovu, ikiwa atageuka na kuziacha dhambi zake zote ambazo ametenda+ naye hakika ashike sheria zangu zote na kutenda haki na uadilifu,+ hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.+ 22 Makosa yake yote ambayo ametenda—hayo hayatakumbukwa juu yake.+ Ataendelea kuishi kwa uadilifu ambao ametenda.’+
23 “ ‘Je, ninapendezwa hata kidogo na kifo cha mtu mwovu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘bali kwamba ageuke na kuziacha njia zake, naye kwa kweli aendelee kuishi?’+
24 “ ‘Sasa, mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki;+ kulingana na machukizo yote ambayo mwovu ametenda yeye anaendelea kutenda+ naye anaishi, hakuna lolote la matendo yake ya uadilifu ambayo ametenda litakalokumbukwa.+ Atakufa kwa sababu ya ukosefu wake wa uaminifu ambao ametenda na kwa sababu ya dhambi ambayo ametenda.+
25 “ ‘Nanyi hakika mtasema: “Njia ya Yehova si sawa.”+ Sikia, tafadhali, Ee nyumba ya Israeli. Je, njia yangu mwenyewe si sawa?+ Je, njia zenu ninyi sizo ambazo si sawa?+
26 “ ‘Mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki+ na afe kutokana nao, atakufa kwa sababu ya kutenda kwa njia isiyo ya haki.+
27 “ ‘Na mwovu anapogeuka na kuuacha uovu wake ambao ameutenda naye atende haki na uadilifu,+ yeye ndiye atakayeihifadhi hai nafsi yake mwenyewe.+ 28 Anapoona+ na kugeuka na kuyaacha makosa yake yote ambayo ametenda,+ hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.+
29 “ ‘Nayo nyumba ya Israeli hakika itasema: “Njia ya Yehova si sawa.”+ Nazo njia zangu, je, si sawa, Ee nyumba ya Israeli?+ Je, njia zenu sizo ambazo si sawa?’+
30 “ ‘Kwa hiyo nitawahukumu ninyi kila mmoja kulingana na njia yake,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ ‘Geukeni, naam, geukeni na kuyaacha makosa yenu yote,+ na chochote kisiwe kwenu kikwazo kinachosababisha kosa.+ 31 Tupilieni mbali kutoka juu yenu makosa yenu yote mliyokosa+ na kujifanyia wenyewe moyo mpya+ na roho mpya,+ kwa maana kwa nini mfe,+ Ee nyumba ya Israeli?’
32 “ ‘Kwa maana sipendezwi na kifo cha mtu anayekufa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Kwa hiyo geukeni, mwendelee kuishi.’ ”+