SEHEMU YA 3
“Upendo Alio Nao Kristo Hutuchochea”
Ni nini kinachotuchochea kuendelea kumfuata Yesu? Mtume Paulo anajibu: “Upendo alio nao Kristo hutuchochea.” (2 Wakorintho 5:14) Katika sehemu hii, tutajifunza kuhusu upendo alio nao Yesu—kumwelekea Yehova, kuwaelekea wanadamu, na jinsi anavyompenda kila mmoja wetu. Kujifunza kuhusu upendo huo kutatuchochea sana. Mioyo yetu itachochewa, nasi tutaona kwamba ni lazima tuchukue hatua, tufanye maendeleo, na kufuata mfano wa Bwana wetu.