HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATENDO 1-3
Roho Takatifu Yamiminwa Juu ya Kutaniko la Kikristo
Wayahudi wengi waliokuwa Yerusalemu katika Pentekoste 33 W.K. walitoka kwenye nchi nyingine. (Mdo 2:9-11) Ingawa walitii Sheria ya Musa, huenda walikuwa wameishi katika nchi ya kigeni maisha yao yote. (Yer 44:1) Hivyo, ingawa walikuwa Wayahudi huenda baadhi yao walionekana na kuongea kama watu wa mataifa waliyotoka. Watu 3,000 kati ya umati huo uliotoka mataifa mbalimbali walipobatizwa, ghafula kutaniko la Kikristo likawa na watu kutoka maeneo mengi tofauti-tofauti. Lakini licha ya malezi yao mbalimbali, “walihudhuria daima kwenye hekalu kwa kusudi moja.”—Mdo 2:46.
Unaweza kuonyeshaje kwamba unapendezwa kibinafsi na . . .
watu katika eneo lenu wanaotoka nchi nyingine?
ndugu na dada katika kutaniko lenu wanaotoka nchi nyingine?