Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Leo
Aprili
Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumanne, Aprili 14

Je, Mwamuzi wa dunia yote hatatenda jambo la haki?—Mwa. 18:25.

Wakati ujao wa milele wa mtu hautegemei anakufa wakati gani. Yehova ni Mwamuzi mkamilifu—anafanya maamuzi kwa uadilifu na haki. (Zab. 33:​4, 5) Tunaweza kuwa na uhakika kwamba “Mwamuzi wa dunia yote” atatenda jambo la haki. Pia, inafaa kufikia mkataa kwamba wakati ujao wa milele wa mtu hautegemei mahali anapoishi. Yehova hawezi kamwe kuwahukumu mamilioni ya watu kuwa “mbuzi” kwa sababu tu wanaishi katika nchi ambazo hawakuwa na fursa ya kusikia ujumbe wa Ufalme. (Mt. 25:46) Mwamuzi wa dunia yote ambaye ni mwadilifu anawajali watu hao kuliko hata sisi tunavyowajali. Hatujui jinsi Yehova atakavyoongoza mambo wakati wa dhiki kuu. Huenda baadhi ya watu hao watapata nafasi ya kujifunza kumhusu Yehova, kuonyesha imani kwake, na kuchukua msimamo upande wa Yehova atakapojitakasa mwenyewe mbele ya mataifa yote.—Eze. 38:16. w24.05 12 ¶14-15

Aprili 13-19
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2026 | Machi

APRILI 13-19

ISAYA 52-53

Wimbo 18 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

[Picha kwenye jalada]

Yesu akienda kuuawa

1. Yesu Alionyesha Upendo Mkubwa!

(Dak. 10)

Yesu angedharauliwa (Isa 53:3; Mt 26:​67, 68; w10 11/15 7 ¶2)

Yesu angekubali kuteswa (Isa 53:7; ip-2 205 ¶25)

Upendo ulimchochea Yesu kuwa tayari kuteseka ili kufanya mapenzi ya Yehova na kuondoa dhambi zetu (Isa 53:​10-12; Yoh 14:31; 15:13)

Yesu amezungukwa na viongozi wa kidini huku uso wake ukiwa umefunikwa. Mmoja wa viongozi hao anampiga ngumi huku wengine wakimdhihaki.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Isa 52:11—Eleza jinsi amri hii ya kinabii ilivyotumika. (it “Vyombo” ¶2)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Isa 53:​3-12 (th somo la 10)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mwenye nyumba ajifunze Biblia. (lmd somo la 4 jambo kuu la 4)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Shiriki kweli kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 3 jambo kuu la 3)

6. Kufuatia Upendezi

(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mtu aliyehudhuria Ukumbusho ajifunze Biblia. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 20

7. Uwe Rafiki ya Yehova—Wonyesho Mkubwa Zaidi wa Upendo

(Dak. 15) Mazungumzo.

Kisehemu kutoka kwenye video “Uwe Rafiki ya Yehova​—⁠Wonyesho Mkubwa Zaidi wa Upendo.” Yesu akiwa Mfalme mbinguni.

Onyesha VIDEO. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ni katika njia gani dhabihu ya Yesu ni zawadi?

  • Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunathamini dhabihu aliyotoa?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo la 76-77

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 57 na Sala

Yaliyomo
Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2026 | Februari

Makala ya juma la Aprili 13-19, 2026

8 Kuelewa Maana ya Ubatizo

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki