Jumanne, Aprili 14
Je, Mwamuzi wa dunia yote hatatenda jambo la haki?—Mwa. 18:25.
Wakati ujao wa milele wa mtu hautegemei anakufa wakati gani. Yehova ni Mwamuzi mkamilifu—anafanya maamuzi kwa uadilifu na haki. (Zab. 33:4, 5) Tunaweza kuwa na uhakika kwamba “Mwamuzi wa dunia yote” atatenda jambo la haki. Pia, inafaa kufikia mkataa kwamba wakati ujao wa milele wa mtu hautegemei mahali anapoishi. Yehova hawezi kamwe kuwahukumu mamilioni ya watu kuwa “mbuzi” kwa sababu tu wanaishi katika nchi ambazo hawakuwa na fursa ya kusikia ujumbe wa Ufalme. (Mt. 25:46) Mwamuzi wa dunia yote ambaye ni mwadilifu anawajali watu hao kuliko hata sisi tunavyowajali. Hatujui jinsi Yehova atakavyoongoza mambo wakati wa dhiki kuu. Huenda baadhi ya watu hao watapata nafasi ya kujifunza kumhusu Yehova, kuonyesha imani kwake, na kuchukua msimamo upande wa Yehova atakapojitakasa mwenyewe mbele ya mataifa yote.—Eze. 38:16. w24.05 12 ¶14-15
APRILI 13-19
ISAYA 52-53
Wimbo 18 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
Yesu akienda kuuawa
1. Yesu Alionyesha Upendo Mkubwa!
(Dak. 10)
Yesu angedharauliwa (Isa 53:3; Mt 26:67, 68; w10 11/15 7 ¶2)
Yesu angekubali kuteswa (Isa 53:7; ip-2 205 ¶25)
Upendo ulimchochea Yesu kuwa tayari kuteseka ili kufanya mapenzi ya Yehova na kuondoa dhambi zetu (Isa 53:10-12; Yoh 14:31; 15:13)
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Isa 52:11—Eleza jinsi amri hii ya kinabii ilivyotumika. (it “Vyombo” ¶2)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Isa 53:3-12 (th somo la 10)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mwenye nyumba ajifunze Biblia. (lmd somo la 4 jambo kuu la 4)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Shiriki kweli kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 3 jambo kuu la 3)
6. Kufuatia Upendezi
(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mtu aliyehudhuria Ukumbusho ajifunze Biblia. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)
Wimbo 20
7. Uwe Rafiki ya Yehova—Wonyesho Mkubwa Zaidi wa Upendo
(Dak. 15) Mazungumzo.
Onyesha VIDEO. Kisha waulize wasikilizaji:
Ni katika njia gani dhabihu ya Yesu ni zawadi?
Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunathamini dhabihu aliyotoa?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 76-77